• Malalamiko |
    • Anuani Zetu |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Kilwa District Council
Kilwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Mikakati ya Halmashauri
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Utumishi na Utawala
      • Elimu ya Msingi
      • Mipango na Takwimu
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Maliasili
    • Vitengo
      • Usafi na Mazingira
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ugavi
      • TEHAMA
      • Nyuki
      • Biashara
      • TASAF
      • Lishe
      • Uvuvi
    • Miji Midogo
      • Masoko
      • Kivinje
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Huduma za Uwekezaji
    • Biashara na Viwanda
    • Madini
    • Uvuvi
    • Utalii
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Mikopo kina Mama na Vijana
    • Huduma za Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Itakayo tekelezwa
  • Machapisho
    • Muongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Mifumo
    • PlanRep
    • FFARS
    • Prem
    • Salary Slip Portal

Waziri wa Maji na Umwagiliaji aitangazia neema Kilwa

Posted on: July 25th, 2018

KIlwa,

Waziri wa maji na umwagiliaji Mheshimiwa Profesa Makame Mbarawa amesema Serikali ipo mbioni kuanzisha Mradi mkubwa wa maji katika Mto Mavuji Wilayani Kilwa.

Ameyasema hayo alipokuwa akizungumza na Wakuu wa Idara na Vitengo wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa katika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kilwa ikiwa ni muendelezo wa ziara yake katika Mkoa wa Lindi.

Profesa Mbarawa Amesema mradi wa Maji utakaoanzishwa utakuwa suruhusho la tatizo la upatikanaji wa maji katika Wilaya ya Kilwa Hasa katika kata ya Pande na Lihimalyao ambako kuna matatizo ya maji.

Amesema mchakato wa kuanzisha mradi huo umekwisha anza na upo katika hatua za mwishoni na muda si mrefu utatekelezwa.

“Mradi huu unaweza ukachukuwa muda mrefu kidogo kukamilika laikini tuna amini pindi utakapo kamilika utakuwa umesaidia kutatua tatizo la maji katika baadhi ya vijiji hapa Wilayani Kilwa Hasa katika kata ya pande na Lihimalyao ambapo vyanzo vingi vimekua vikitoa maji yenye Chumvi, kwahiyo tuendelee kusimamia hii miradi ambayo tunayo kwa umakini mkubwa ili wananchi waendelee kupata huduma ya maji yaliyo safi na salama” alisema Profesa Mbarawa

Aidha amemtaka Meneja wa Mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingira Kilwa Masoko  Mhandisi Issa Banda kuhakikisha huduma ya maji inaimarika na wananchi wanafaidika na huduma hiyo pamoja na kuongeza mapato kutoka milioni ishirini na moja inayopatikana sasa hadi milioni arobaini na tano.

Kwa upande wake Meneja wa Mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingira Kilwa Masoko  Mhandisi Issa Banda amesema Mamlaka ya maji Kilwa inakabiriwa na changamoto mbalimbali ikiwemo Madeni sugu kwa baadhi ya Taasisi za serikali, ukosefu wa gari la mfumo wa Maji taka, uchakavu wa miundo mbinu pamoja na Kukosa umeme wa uhakika hali ambayo ipelekea kuongeza kwa saa kadhaa kupandisha maji katika Matenki kwa ajili ya kusambaza kwa Wananchi.

“Sanjari na mafanikio Mheshimiwa waziri tuna changamoto ya Madeni sugu kutoka katika taasisi mbalimbali za serikali, laikini pia kuna kiasi cha maji ambacho kinapotea kutoaka na uchakavu wa miundo mbinu ambayo tunaitumia.

Lakini tatizo linguine ni ukosefu wa umeme wa uhakika ambao tunaweza kutumia katika shughuli zetu za kila siku, siku nyingine umeme unakuwa mdogo kwa maana ya Low voltage kitu ambacho kinakuwa kinaturudisha nyuma, Mheshimiwa tunaomba utusaidie kupata jenereta lenye uwezo mkubwa ili liweze kutusaidia” alihitimisha Banda   

Awali akisoma taarifa kwa Mheshimiwa Waziri Kaimu Mhandisi wa Maji Wilaya ya Kilwa Bw. Badi Mussa amemuomba Waziri kuongeza idadi ya watumishi katika idara hiyo kwani kwa sasa watumishi ambao wapo ni wachache.

Kaimu Mhandisi wa Maji Wilaya ya Kilwa Bw. Badi Mussa akisoma taarifa kwa Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mheshimiwa Profesa Makame Mbarawa alipoitembelea Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa (Picha: Ally Ruambo).

Akiwa Wilayani Kilwa Profesa Mbarawa alitembelea miradi mbalimbali ikiwemo chanzo cha maji kilichopo katika kijiji cha Mpara.

Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU UTOAJI WA MIKOPO KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 04, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 11, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI. April 25, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MAKALA APONGEZA JITIHADA ZA KURUDISHA MAWASILIANO SOMANGA

    April 10, 2025
  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa Mkono wa Eid kwa watoto wenye mahitaji Maalum Shule ya Msingi Mtanga Wilayani Kilwa.

    March 31, 2025
  • IDARA YA MAENDELEO YA JAMII YATOA MSAADA WA TELEVISHENI KWA GEREZA LA KILWA MASOKO

    April 28, 2025
  • MARAFIKI WA ELIMU WAWASILISHA TAARIFA YA UFUATILIAJI WA MAKUZI YA AWALI YA MTOTO KWA WADAU WA ELIMU KILWA.

    April 28, 2025
  • Tazama Zote

Video

Mkuu wa Wilaya ya Kilwa Akipokea Mwenge wa Uhuru.
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • TARURA GPN
  • Watumishi Portal
  • MIKOPO 10%
  • Mikopo ya Wanawake na Vijana
  • Huduma za Elimu

Tovuti Muhimu

  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ikulu
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu
  • Lindi

Idadi ya Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani Zetu

    Kilwa Masoko

    Anuani ya Posta: 160

    Simu: 0672365354

    Simu: 0672581557

    Barua pepe: ded@kilwadc.go.tz /ictsupport@kilwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Kanuni Binafsi
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa