• Malalamiko |
    • Anuani Zetu |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Kilwa District Council
Kilwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Mikakati ya Halmashauri
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Utumishi na Utawala
      • Elimu ya Msingi
      • Mipango na Takwimu
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Maliasili
    • Vitengo
      • Usafi na Mazingira
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ugavi
      • TEHAMA
      • Nyuki
      • Biashara
      • TASAF
      • Lishe
      • Uvuvi
    • Miji Midogo
      • Masoko
      • Kivinje
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Huduma za Uwekezaji
    • Biashara na Viwanda
    • Madini
    • Uvuvi
    • Utalii
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Mikopo kina Mama na Vijana
    • Huduma za Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Itakayo tekelezwa
  • Machapisho
    • Muongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Mifumo
    • PlanRep
    • FFARS
    • Prem
    • Salary Slip Portal

Health


District Medical Officer(DMO)

IDARA YA AFYA

Utangulizi.

Huduma za Afya katika Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa hutolewa kwa ushirikiano kati ya Serikali na wadau wengine kwa maana ya watu na mashirika binafsi (Public Private Partnership) chini ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kilwa zikisimamiwa na Ofisi ya Mganga Mkuu wa Halmashauri.


VITUO VYA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA.

Huduma ya Afya Wilayani hutolewa katika ngazi mbalimbali za matibabu katika jumla ya Vituo 55, Hospitali 2, moja ya Serikali (Hospitali ya Wilaya) na nyingine ya Shirika la Dini (Hospitali ya Kipatimu) ambayo vilevile hutoa huduma kwa mkataba na Halmashauri ya Wilaya kwa watoto na Mama wajawazito (Service Agreement), Vituo vya Afya 5 vya serikali, Zahanati 48 kati ya hizo Zahanati 1 ni ya Shirika la dini na 1 ni ya binafsi. Zahanati 14 ziko katika hatua mbalimbali za ujenzi.

HALI YA WATUMISHI WA KADA ZA AFYA WILAYANI

Halmasshauri ya Wilaya ya Kilwa ina jumla ya watumishi 335 wa kada mbalimbali za Afya (sawa 25%) kati ya 1315 wanaohitajika kukidhi ikama ya watumishi kwa mujibu wa Mwongozo wa Ikama wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto (2014-2019). Kati ya watumishi waliopo 335, Watumishi wenye ujuzi (Skilled Personal) ni 158 sawa na 47%. Watumishi 177 ni wale wasio na ujuzi (Unskilled personnel) sawa na asilimia 53%. Aidha athari ya upungufu wa watumishi huonekana sana katika ngazi za chini za vituo vya huduma hususani Zahanati ambako vituo vingi vina watumishi aidha mmoja au wawili.

MAJUKUMU YA IDARA

  • Kuratibu masuala yote yahusuyo Afya,kwa maana ya kinga na tiba.
  • Kuandaa mpango kabambe (CCHP) na kusimamia utekelezaji wake.
  • Kutoa ushauri wa kuboresha huduma za Afya katika Wilaya ikiwemo na usimamizi elekezi na kufuatilia utendaji wa vituo vyote vya kutolea huduma.
  • Kushirikiana Wajumbe wa Halmashauri katika kuandaa Mpango wa Halmashauri.
  • Kuandaa na kuwasilisha mapendekezo ya Idara juu ya fedha,mtazamo na malengo yaliyopendekezwa(vipaumbele).
  • Kuratibu na kuhakikisha watoto wanapata chanjo.
  • Kuhakikisha mali za Halmashauri na zinazomilikiwa na Idara zipo katika hali nzuri.
  • Kudumisha uhusiano mzuri wa huduma za Afya kwa watoa huduma binafsi na wadau kutoa tafsiri ya sera za afya.
  • Kuandaa na kuwasilisha taarifa za shughuli mbalimbali za mwaka.

JITIHADA ZINAZOCHUKULIWA KATIKA KUPAMBANA NA UKIMWI

Mapambano dhidi ya ugonjwa hatari wa UKIMWI yanaendelea. Wilaya kwa kushirikiana na wadau  mbalimbali wa Afya wanatekeleza na kutoa elimu ya  kinga, upimaji wa hiari na ushauri nasaha, matibabu kwa wanaoishi na VVU na kutoa huduma ya chakula kwa wagonjwa wa UKIMWI, huduma hii hutegemea uwepo wa bajeti. Pia kuna vikundi 15 vya wanaoishi na VVU na kati ya hivyo vikundi 5 ni vya watoto chini ya miaka 14 vilivyopo kituo cha AfyaTingi na Masoko pamoja na Hospital ya Wilaya na Shirika la dini.

Takwimu za maambukizi ya UKIMWI Kimkoa zinaonyesha kuwa kiwango cha maambukizi ya virusi vya UKIMWI katika Wilaya ya Kilwa kimepungua kutoka 2.8% mwaka 2007 hadi 2.1% kwa sasa (2016).

 

VIFO VITOKANAVYO NA UZAZI

Kwa kipindi cha mwezi Julai hadi  Desemba 2016Jumla ya akina mama 3,257 walijifungua. Kati ya hao 2,801 walijifungua katika vituo vya kutolea huduma za afya.Vifo vya akina mama wajawazito na baada ya kujifungua ni 10.Vifo  hivi vimesababishwa na sababu mbalimbali zikiwemo, kina mama kuchelewa kufika katika vituo vya huduma, kifafa cha mimba na upungufu wa damu.

HALI YA UPATIKANAJI WA DAWA NA VIFAA TIBA

 

Jedwali linaloonyesha manunuzi ya dawa na vifaa tiba kwa miezi sita (Julai- Desemba 2016). Katika kipindi rejea cha taarifa jumla ya Tsh 290,337,835 zilitumika kutoka vyanzo mbalimbali vya fedha kununulia dawa na vifaa tiba kwa vituo 53 vya kutolea huduma ya Afya. Pamoja na jitihada hizo bado kuna changamoto ya kukosekana kwa baadhi ya dawa na vifaa tiba muhimu (Out of Stock) katika Bohari ya Madawa (MSD)

Chanzo cha pesa
Receipt in Kind (Ruzuku serikali kuu)
Fedha za Wafadhiri ( Basket Fund)
Fedha za uchangiaji (DRF, User fees)
            CHF
Jumla
Kiasi cha pesa
98,156,255.88
159,014,900
21,163,980
12,002,700
290,337,835

 

HUDUMA ZA CHANJO WILAYANI

Huduma za chanjo hutolewa kwa watoto wenye umri chini ya miaka 5 na akina mama wajawazito na wale walio katika umri wa kuzaa. Chanjo zinazotolewa vituoni ni aina saba ambazo zinakinga magonjwa yafuatayo, Kifua Kikuu, Pepopunda, Dondakoo, Kifaduro, Homa ya INI, Homa ya uti wa mgongo, Surua, Kichomi na kuhara kunakosababishwa na Rotavirus. Kwa Wilaya yetu, vituo 52 kati ya 55 vinatoa huduma ya chanjo. Kwa vituo visivyotoa huduma ya chanjo, wanapata huduma kwa njia za huduma mkoba (Out reach services).

Kwa kipindi cha Juni hadi Disemba 2016 kulikuwepo na chanjo  za kutosha isipokuwa chanjo ya kukinga ugonjwa wa surua na kifua kikuu, kutokana upungufu wa chanjo hizo kwa ngazi ya Taifa na Mkoa. Walengwa wa chanjo ni kama ifuatavyo; Walengwa kwa mwaka ilikadiriwa kuwa watoto 8,002. Lengo kwa mwezi ni kuchanja watoto  667. Lengo la kitaifa ilikuwa kufikia zaidi ya 90% na Wilaya ya Kilwa imevuka lengo kwa chanja kwa asilimia 98.

 

MFUKO WA AFYA YA JAMII (CHF)

Wilaya ya Kilwa inatekeleza agizo la Serikali, Sheria ya Mfuko wa Afya ya Jamii ya Mwaka 2001 (CHF Act 2001) inayotaka kila mwanajamii kujiunga kwa hiari na mfuko wa Afya ya Jamii ambapo Wilaya imeanza kutekeleza mpango huu kuanzia mwaka 2006. Tangu mwaka huo viongozi wa Wilaya kwa kushirikiana na wataalam wa Halmashauri ya Wilaya hususani Idara ya Afya imekuwa ikitoa elimu kwa wananchi juu ya faida ya kujiwekea bima ya Afya kabla ya kuugua.

Mfuko wa Afya ya Jamii unalenga kuwa na wanachama wa aina nne ambao ni:-

  • Uanachama wa Kaya, ambapo kila kaya kunakuwa na wanufaika 06 yaani mkuu wa kaya na wategemezi 05.
  • Uanachama wa makundi, ambapo vikundi mbalimbali vinaamua kujiunga na huduma hii, mfano vikundi vya madereva wa pikipiki (Bodaboda), vikundi vya ufugaji n.k.
  • Uanachama wa wanafunzi, ambao wanajiunga 05 kwa kila kikundi na kusajiliwa kama kaya.
  • Kupitia Mradi wa Tumaini la Mama unaofadhiliwa na Shirika la Maendeleo la Ujerumani (GIZ) kwa kushirikiana na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto ambapo kila Mama mjamzito analipiwa Tshs 10,000 kwa ajili ya wategemezi wake wanne (4) ili kujiunga na CHF.

 

MPANGO WA MATOKEO MAKUBWA SASA (BRN)

Mpango wa  matokeo makubwa sasa (BRN) ni mkakati wa kitaifa wenye lengo la kuhakikisha kwamba vituo vyote vya kutolea huduma za afya nchini vinakuwa na hadhi ya nyota walao 3 ifikapo Juni 2018. Katika Wilaya ya  Kilwa vituo 55 viko katika mpango wa BRN kwa mgawanyiko ufuatao (Hospitali 2, vituo vya Afya 5 na Zahanati 48). Mikakati mbalimbali inafanyika ikiwemo, mafunzo kazini na vikao mbalimbali kwa watoa huduma za Afya juu ya umuhimu wa BRN pamoja na kutoa tafsiri ya viashiria vinavyotumika kupima ubora wa huduma zitolewazo vituoni. Aidha Simamizi Elekezi za Kitaifa, Mkoa na Kiwilaya zinaendelea kufanyika  ili kuelekeza ni vigezo na viashiria gani hupelekea kituo kupata nyota kuanzia 1 na kuendelea.

MPANGO WA TATHIMINI SHIRIKISHI YA KIJAMII YA HUDUMA ZA AFYA (Community Scorecard).

Huu ni mpango wa Majaribio ufanywao kwa ushirikiano kati ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto na Shirika la Maendeleo la Ujerumani (GIZ) katika kuhakikisha wanajamii wanashirikishwa katika kutathimini ubora wa huduma za Afya ili kubaini changamoto zilizopo na kisha kuweka mikakati na mipango kazi ya kutatua changamoto hizo kwa kupitia jamii husika.  Wilaya ya Kilwa ni miongoni mwa wilaya 6 za majiribio nchini katika Mikoa minne ya Lindi (Kilwa), Mtwara (Nanyumbu na Newala), Mbeya (Busokelo) na Tanga (Handeni na Bumbuli). Mradi huu unatekelezwa katika vijiji vya Mchakama, Kiwawa na Mandawa kwa wilaya ya Kilwa tangu mwaka 2016.

Lengo la mradi huu niKuongeza dhana ya ushirikishwaji na uwajibikaji kwa watoa huduma na wapokea huduma katika vituo vya huduma za Afya na kuondoa dhana ya kwamba kituo cha huduma za Afya ni mali ya  Serikali.

 Changamoto

  • Upungufu mkubwa wa watumishi wa kada za Afya hasa waganga na wauguzi
  • Upungufu wa miundombinu (majengo ya huduma,nyumba za watumishi,)
  • Upungufu wa dawa na vifaa tiba muhimu usababishwao na ufinyu wa bajeti na  changamoto za bohari ya madawa

 

 

 

Mikakati

  • Kuendelea kuomba watumishi kupitia bajeti ya Halmashauri kulingana na mahitaji.
  • Kuendelea kujenga zahanati 14 ambazo zipo katika hatua mbalimbali za ujenzi pamoja na kujenga kituo kipya cha Afya katika kata ya Chumo.
  • Kutumia vyanzo vingine vya mapato (mapato ya ndani, CHF, Papo kwa Papo) kununua dawa nje ya mfumo wa MSD
  • Kuhakikisha tunasimamia ukusanyaji mapato katika vituo vya kutolea huduma.

Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU UTOAJI WA MIKOPO KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 04, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 11, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI. April 25, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WAZIRI MKUU MAJALIWA AWASILI KILWA KUKAGUA ATHARI ZA MVUA NZITO

    April 16, 2025
  • AFO YAJA YA MRADI WA KUREJESHA MATUMBAWE HAI KILWA

    April 15, 2025
  • TANGAZO LA AWAMU YA PILI YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA WAPIGA KURA

    April 15, 2025
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA KILWA NA SEKTA BINAFSI KUJADILI KUJENGA MAENDELEO KWA PAMOJA

    April 14, 2025
  • Tazama Zote

Video

Mkuu wa Wilaya ya Kilwa Akipokea Mwenge wa Uhuru.
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • TARURA GPN
  • Watumishi Portal
  • MIKOPO 10%
  • Mikopo ya Wanawake na Vijana
  • Huduma za Elimu

Tovuti Muhimu

  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ikulu
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu
  • Lindi

Idadi ya Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani Zetu

    Kilwa Masoko

    Anuani ya Posta: 160

    Simu: 0672365354

    Simu: 0672581557

    Barua pepe: ded@kilwadc.go.tz /ictsupport@kilwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Kanuni Binafsi
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa