Kijiji cha Njinjo wilayani Kilwa kimeanza ujenzi wa mnada wa Mifugo ambao hadi kukamilika kwake kunatarajiwa kugharimu kiasi cha Milioni 106 ambapo kwa wastani Ng'ombe 1000, Mbuzi na Kondoo 40 huuzwa kwa mwezi.
Awali msimamizi wa mradi ndugu Abdallah Masaki amesema ujenzi wa mradi huu umepangwa kufanyika kwa awamu mbili ambapo awamu ya kwanza itahusisha ujenzi wa ukuta tofali wenye ukubwa wa mita za mraba 5,000 , mageti na pakilio na awamu ya pili itahusisha ujenzi wa vyoo, kibanda cha mlinzi na mtoza ushuru pamoja na uwekaji wa taa ambapo ujenzo wa uzio na mageti umegharimu Shilingi Milioni 74 na awamu pili utaanza mwaka wa fedha 2025/2026 kwa bajeti iliyopangwa ya shilingi Milioni 32 na inakadiriwa kuwa ujenzi wa mnada huu hadi kukamilika kwake utagharimu Milioni 106 .
Mradi huu unatajwa kuwa na faida kadhaa ikiwemo kuongeza mapato ya kijiji, Halmashauri na serikali kuu kupitia ada na tozo , kuwepo kwa soko la uhakika la mifugo kutokana na ushindani wa wanunuzi, kusaidia katika udhibiti wa magonjwa ya wanyama na kuzuia upotevu wa mifugo .
Kiongozi wa Mbio za Mwenge Ndugu Ismail Ali Ussi amepongeza Kijiji na Halmashauri kwa kubuni mradi huo mkubwa na wenye tija kwa wananchi .
Kwasababu ya ubunifu wa mradi na tija yake kwa jamii pamoja na kuzingatia vigezo kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru kitaifa ameridhia kuweka jiwe la msingi mradi huo .
Aidha, ametumia fursa hiyo kuwasisitiza wananchi kujitokeza kwenda kupiga kura kuchavua viongozi wanaowahitaji muda utakapofika.
Kilwa Masoko
Anuani ya Posta: 160
Simu: 0672365354
Simu: 0672581557
Barua pepe: ded@kilwadc.go.tz /ictsupport@kilwadc.go.tz
Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa