• Malalamiko |
    • Anuani Zetu |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Kilwa District Council
Kilwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Mikakati ya Halmashauri
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Utumishi na Utawala
      • Elimu ya Msingi
      • Mipango na Takwimu
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Maliasili
    • Vitengo
      • Usafi na Mazingira
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ugavi
      • TEHAMA
      • Nyuki
      • Biashara
      • TASAF
      • Lishe
      • Uvuvi
    • Miji Midogo
      • Masoko
      • Kivinje
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Huduma za Uwekezaji
    • Biashara na Viwanda
    • Madini
    • Uvuvi
    • Utalii
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Mikopo kina Mama na Vijana
    • Huduma za Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Itakayo tekelezwa
  • Machapisho
    • Muongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Mifumo
    • PlanRep
    • FFARS
    • Prem
    • Salary Slip Portal

WATUMISHI AJIRA MPYA KILWA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI

Posted on: September 22nd, 2025

Watumishi wapya wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa yamepatiwa mafunzo elekezi yenye lengo la kuwaongezea uelewa wa majukumu yao katika utumishi wa umma. Mafunzo hayo yamefanyika tarehe 22 Septemba 2025 katika ukumbi wa Chuo cha Maendeleo ya Wananchi (FDC) Kilwa.


Akifungua mafunzo hayo, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa Ndg. Hemed Magaro amewataka watumishi hao wapya kutumia nafasi waliyoipata kwa bidii na uadilifu.


“Nawapongeza kwa kupata ajira hizi, ni nafasi ya heshima na dhamana kubwa kwa ajili ya kuwahudumia wananchi. Ni wajibu wenu kuhakikisha mnafanya kazi kwa kuzingatia sheria, kanuni na maadili ya Utumishi wa Umma. Serikali inatarajia kuona matokeo chanya kupitia mchango wenu,” amesema Ndg. Magaro.


Kwa upande wake, Afisa Utumishi wa Wilaya ya Kilwa Ndg. Msena Bina amewasisitiza watumishi hao kuzingatia nidhamu na uwajibikaji katika maeneo yao ya kazi ili kuongeza ufanisi wa utoaji huduma kwa wananchi.


Washiriki yamepatiwa elimu kuhusu maadili ya utumishi wa umma, kanuni za kazi za serikali za mitaa, misingi ya maadili ya utendaji kazi, uwajibikaji, na utoaji wa huduma bora kwa wananchi. Aidha yamefundishwa mada maalum kuhusu makosa na adhabu katika utumishi wa umma, elimu ya afya ikiwemo Ukimwi mahala pa kazi, pamoja na masuala ya pensheni kwa watumishi wa umma.


Akitoa mafunzo hayo, mwezeshaji kutoka Chuo cha Utumishi Mtwara Bwana. Gasper Kinsinza katika mada ya Makosa na Adhabu katika Utumishi wa Umma, amesisitiza umuhimu wa watumishi kufahamu taratibu na kanuni zinazowaongoza ili kuepuka makosa yanayoweza kusababisha hatua za kinidhamu.


Naye mwezeshaji kutoka Mfuko wa Hifadhi ya jamii kwa watumishi wa umma (PSSSF) Ndg. Yunus Buheti amewasihi washiriki kuzingatia mafunzo waliyoyapata na kuyatekeleza kwa ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku.


Lengo kuu la mafunzo hayo ni kuhakikisha watumishi wapya wanayatekeleza majukumu yao kwa weledi, kuzingatia sheria na taratibu, na kuongeza ufanisi katika utoaji huduma ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI HALMASHAURI YA WILAYA YA KILWA September 03, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU UTOAJI WA MIKOPO KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 04, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI AJIRA MPYA KILWA WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI

    September 22, 2025
  • CRDB KILWA YAKABIDHI MEZA NA VITI SHULE YA SEKONDARI MAVUJI

    September 20, 2025
  • KILWA YAADHIMISHA SIKU YA USAFISHAJI WA MAZINGIRA DUNIANI KWA KAMPENI YA USAFI WA PAMOJA

    September 20, 2025
  • MAAFISA BAJETI KILWA WAPIGWA MSASA KUIMARISHA UANDAAJI BORA WA BAJETI

    September 19, 2025
  • Tazama Zote

Video

Mkuu wa Wilaya ya Kilwa Akipokea Mwenge wa Uhuru.
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • TARURA GPN
  • Watumishi Portal
  • MIKOPO 10%
  • Mikopo ya Wanawake na Vijana
  • Huduma za Elimu

Tovuti Muhimu

  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ikulu
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu
  • Lindi

Idadi ya Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani Zetu

    Kilwa Masoko

    Anuani ya Posta: 160

    Simu: 0672365354

    Simu: 0672581557

    Barua pepe: ded@kilwadc.go.tz /ictsupport@kilwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Kanuni Binafsi
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa