Katika kuadhimisha Miaka 52 ya Siku ya Mazingira Duniani yanayofanyika kila tarehe 05 Mwezi Juni, Mkuu wa Wilaya ya Kilwa Mhe Mohamed Nyundo ameitaka jamii wilayani Kilwa kushirikiana ipasavyo katika utunzaji wa Mazingira ikiwemo kuachana na matumizi ya mifuko ya plastiki inayopelekea uharibufu wa mazingira kwa kiasi kikubwa.
Ametoa wito huo tarehe 05 Juni 2025 katika maadhimisho ya siku ya Mazingira Duniani yaliyobeba kauli mbiu ya "Mazingira yetu ya Tanzania ijayo tuwajibike sasa, dhibiti matumizi ya plastiki" maadhimisho hayo yamefanyika Kiwanja cha Mkapa Kilwa Masoko ambapo yamemaliziwa na shughuli za usafi wa mazingira uliofanyika kwa siku 5 kuanzia tarehe 01 hadi 05 June 2025 kwa ushirikiano kati ya Watumishi na wananchi katika Mazingira ya Fukwe za bahari wilaya humo.
Pia Mhe. Nyundo amevitaka Vikundi vya usimamizi wa Fukwe za Bahari Kilwa (BMU) kuratibu utengenezaji wa Virabu maalum vitakavyohusisha Watumishi,wanafunzi na Wananchi kwaajili ya kutekeleza shughuli za utunzaji wa mazingira hususani katika fukwe hizo za bahari lengo ikiwa ni kuhakikisha mazingira ya fukwe za bahari Wilayani Kilwa zinakuwa safi.
Nae Ndg. Abushiri Mbwana niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa ametoa pongezi kwa watumishi na wananchi wilayani humo kwa muamko walioonyesha katika kushiriki zoezi la usafi wa kuondoa taka za plastiki katika maeneo ya fukwe za bahari Pia amewaomba kuendelea kujitoa katika shughuli za utunzaji wa mazingirana kwaajili ya kuimarisha usafi Wilaya Kilwa.
Akiwasilisha Risala iliyoandaliwa na kitengo cha Udhibiti wa taka ngumu na Usafi, Afisa Mazingira wilayani Kilwa Ndg. Paul Hilari amesema kuwa wamekuwa wakitumia njia mbalimbali katika kudhibiti matumizi ya vitu vya pastiki kwa kutoa elimu kwa jamii juu ya madhara ya plastiki, kutumia wadau wa utunzaji wa mazingira ikiwemo mmiliki wa kiwanda cha kuchakata plastiki aitwae (Nuru Mohamed) katika kutokomeza taka hizo na kuwa na utaratubu wa kufanya usafi kilwa jumamosi ya Mwisho wa Mwezi.
Mwisho Ndg. Hilari ameitaka jamii wilayani humo kuwaunga mkono wadau wa Uhifadhi wa mazingira wanaotumia taka za plastiki kuzichakata kama malighafi Viwandani kwani watasaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza uchafuzi wa mazingira.
Kilwa Masoko
Anuani ya Posta: 160
Simu: 0672365354
Simu: 0672581557
Barua pepe: ded@kilwadc.go.tz /ictsupport@kilwadc.go.tz
Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa