Waziri wa Ujenzi, Mhe. Abdallah Ulega, amefanya ziara ya kikazi ya kukagua maendeleo ya ujenzi na ukarabati wa miradi ya madaraja katika Wilaya ya Kilwa, katika ziara yake ya ukaguzi wa mradi ya madaraja Mkoa wa Lindi, ikiwa ni sehemu ya juhudi za serikali kurejesha miundombinu iliyoharibiwa na mvua zilizonyesha katika kipindi kilichopita.
Katika ziara hiyo, Mhe. Ulega alipata fursa ya kukagua maendeleo ya mradi wa ujenzi wa daraja la Somanga na Matandu ambapo ametoa maagizo kwa wakandarasi kuhakikisha kuwa ujenzi wa miundombinu hiyo unakamilika ifikapo Septemba 24, 2025, ili kuwezesha upatikanaji wa huduma za usafirishaji kwa wananchi bila vikwazo.
“Ninawataka wakandarasi wote kuhakikisha kuwa mradi huu unakamilika kwa ubora unaostahili na kwa muda uliopangwa, ili kurahisisha huduma za usafiri na kuinua maendeleo ya kiuchumi katika maeneo haya,” amesema Mhe. Ulega.
Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Kilwa, Mhe. Mohamed Nyundo, ameishukuru serikali ya Awamu ya Sita kwa juhudi zake za kuhakikisha kuwa miundombinu iliyoharibika inarejeshwa katika hali yake ya awali. Ambapo amebainisha ukamilishaji wa miradi hiyo utaleta manufaa makubwa kwa wananchi na kuimarisha uchumi wa eneo hilo
Kilwa Masoko
Anuani ya Posta: 160
Simu: 0672365354
Simu: 0672581557
Barua pepe: ded@kilwadc.go.tz /ictsupport@kilwadc.go.tz
Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa