• Malalamiko |
    • Anuani Zetu |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Kilwa District Council
Kilwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Mikakati ya Halmashauri
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Utumishi na Utawala
      • Elimu ya Msingi
      • Mipango na Takwimu
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Maliasili
    • Vitengo
      • Usafi na Mazingira
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ugavi
      • TEHAMA
      • Nyuki
      • Biashara
      • TASAF
      • Lishe
      • Uvuvi
    • Miji Midogo
      • Masoko
      • Kivinje
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Huduma za Uwekezaji
    • Biashara na Viwanda
    • Madini
    • Uvuvi
    • Utalii
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Mikopo kina Mama na Vijana
    • Huduma za Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Itakayo tekelezwa
  • Machapisho
    • Muongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Mifumo
    • PlanRep
    • FFARS
    • Prem
    • Salary Slip Portal

Watumishi Idara ya Afya wapatiwa semina elekezi

Posted on: July 7th, 2018

Kilwa

Watumishi wametakiwa kufanya kazi kwa kuzingatia Kanuni za Maadili ya utendaji na kitaaluma katika utumishi wa umma.

Wito huo umetolewa na Afisa utumishi Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa Ndg. Ally Ligalawike alipokua akizungumza na Watumishi  katika Semina elekezi  ya Mafunzo kwa Watumishi wapya iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa  Hospitali ya Kinyonga Mjini Kilwa Kivinje.

Ligalawike amesema iwapo watafuata misingi na kanuni zilizowekwa katika utumishi wa umma basi watafanya kazi bila shaka na wasiwasi wowote.

”Katika utuimishi wa umma kuna kanuni na Sheria ambazo zinatuongoza kama walivyoelezea wawezeshaji waliopita  kwahiyo kama utakua unazikiuka hizo kanuni na maadili basi moja kwa moja utaadhibiwa kutokana na sheria inavyosema na sidhani kama utaweza kuwa huru au kujisikia vizuri kama utakua unapewa Onyo mara kwa mara juu ya mienendo yako katika utumishi lazima utakua mtu wa wasiwasi” alisema Ligalawike

Pia amewataka watumishi hao kuwa na heshima na nidhamu kwa watu wote na kuwahudumia bila kujali itikadi zao

”Wengi wetu hapa ni vijana na kama mnavyojua vijana kuna maneno Fulani ambayo tunapenda kuyatumia, sitarajii kusikia tunatumia maneno ya mtaani sehemu ya kazi Mfano anakuja mgonjwa unaanza kukamkaribisha kwa salamu za vijiweni oi niaje? Au kaja mtu kavalia suti nzuri kama rafiki yangu hapo ukaona yes! huyu ndiye wa kuanza kumpa huduma ukawaacha wengine ambao amewakuta  katika utaratibu mambo hayo hakuna” alisisitiza Ligalawike 

Afisa utumishi Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa Ndg. Ally Ligalawike akizungumza na Watumishi  kutoka Idara ya Afya katika Semina elekezi  ya Mafunzo kwa Watumishi wapya iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa  Hospitali ya Kinyonga Mjini Kilwa Kivinje (Picha: Ally Ruambo)

 Aidha amewataka kuzingatia Mavazi ambayo Mtumishi wa umma ameruhusiwa kuvaa na kuheshimu pamoja na kutunza mali na siri za ofisi.

“Kuna taarifa ambazo zinatakiwa kuwa wazi ili wananchi wazijue kama vile mapato na matumizi ya vituo vyetu vya kutolea Huduma na kuna Taarifa zingine zinabaki kuwa siri ya ofisi, ni kinyume na sheria na kanuni za utumishi wa Umma kuvujisha siri za ofisi kwahiyo naomba muwe makini sana na suala hili” alihitimisha ligalawike .

Akizungumza kwa niaba ya Watumishi waliohudhuria mafunzo hayo Muhasibu msaidizi kituo cha afya Masoko Nuru Mwamakula amesema wanashukuru kwa mafunzo waliyoyapata kwani yamewaongezea uwezo zaidi katika utekelezaji wao wa majukumu yao ya kila siku.

“Mimi binafsi na wenzangu tunashukuru kwa mafunzo kwani haya mafunzo yametutoa sehemu moja na kutupeleka sehemu nyingine ambayo ni bora zaidi, kuna mambo ambayo yalikua yanafanyika labda kwa kuto kujua lakini kwa sasa naimani hayataweza kujitokeza tena

Mimi binafsi muda mrefu sana nimekua nikifanya kazi katika taasisi binafsi kwahiyo kuna mambo ambayo nilitoka  nayo na kuja nayo huku bila kujua kuwa utaratibu ni tofauti kidogo kwa kua nilikua sifahamu lakini kwa mafunzo haya sasa nimekua mpya” alisema Nuru


Muhasibu msaidizi kituo cha afya Masoko Bw. Nuru Mwamakula akizungumza  katika Semina elekezi  ya Mafunzo kwa Watumishi wapya iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa  Hospitali ya Kinyonga Mjini Kilwa Kivinje (Picha: Ally Ruambo)

Awali akizungumza na watumishi Katibu wa Afya Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa Bw. Maongezi amewataka watumishi kuwa wawazi pindi wapatapo changamoto katika maeneo yao ya kazi na kuwataka kufuata ngazi katika kuwasilisha matatizo yao.

“Hili ni jambo muhimu sana ndugu zangu msikae na matatizo sisi viongozi tupo tuelezeni na tutawasaidia ila tu niwakumbushe kufuata utaratibu. Kuna wengine wakiwa na jambo lao moja kwa moja wanaenda ngazi za juu mwisho wa siku shauri linarudishwa chinimkwa kua sisi ndio wa kwanza kuyajibia, kwahiyo tufuate utaratibu” alisema Maongezi

Pia amewapongeza watumishi hao wa utendaji wao wa kazi kwani kwa  muda  mfupi ambao wameajiriwa matokeo Chanya yameanza kuonekana katika vituo vyao vya kazi.

“Kwa hili niwapongeze kwa muda mfupi ambao tumekuwa pamoja katika utendaji tumeona mabadiliko kwahiyo naomba muendelee na spidi hiyo hiyo na ikiwezekana muzidishe zaidi” alisema Maongezi

Katibu wa Afya Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa Bw. Maongezi akizungumza na Watumishi  kutoka Idara ya Afya katika Semina elekezi  ya Mafunzo kwa Watumishi wapya iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa  Hospitali ya Kinyonga Mjini Kilwa Kivinje (Picha: Ally Ruambo)

Kwa upande wake Katibu wa Hospitali ya wilaya ya Kilwa Bi. Zabib Uledi amewataka watumishi hao kutoshiriki katika vitendo viovu ikiwemo utumiaji wa madawa ya kulevya, Pombe kupindukia, uasharati pamoja na vitendo vya rushwa.

Katibu wa Hospitali ya wilaya ya Kilwa Bi. Zabib akitoa maelekezo kwa Watumishi  katika Semina elekezi  ya Mafunzo kwa Watumishi wapya iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa  Hospitali ya Kinyonga Mjini Kilwa Kivinje (Picha: Ally Ruambo)

Zaidi ya Watumishi kumi na tano  kutoka vituombalimbali  vya Afya wakiwemo Wahasibu , Wataalamu wa Maabara na Wauguzi  wamepatiwa mafunzo mbalimbali ikiwemo Haki na wajibu wa Mtumishi,Majukumu, Kanuni za Maadili ya utendaji na kitaaluma katika utumishi wa umma, nidhamu, usiri, utunzaji nyaraka, mavazi, na mengine mengi.

Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU UTOAJI WA MIKOPO KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 04, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 11, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI. April 25, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • BANDARI YA UVUVI KILWA KUKAMILIKA MWEZI JUNI 2025

    May 08, 2025
  • KAMATI YA SIASA YA CCM MKOA WA LINDI YAIPONGEZA KILWA KWA UTEKELEZAJI WA ILANI

    May 07, 2025
  • KILWA YAPIGA HATUA KATIKA KUTOKOMEZA UKATILI WA KIJINSIA DHIDI YA WANAWAKE NA WATOTO

    May 06, 2025
  • WANANCHI, WANAFUNZI NA WATUMISHI KILWA WAJITOKEZA KWA MAZOEZI YA PAMOJA UWANJA WA MWENGE/TAIFA

    May 03, 2025
  • Tazama Zote

Video

Mkuu wa Wilaya ya Kilwa Akipokea Mwenge wa Uhuru.
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • TARURA GPN
  • Watumishi Portal
  • MIKOPO 10%
  • Mikopo ya Wanawake na Vijana
  • Huduma za Elimu

Tovuti Muhimu

  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ikulu
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu
  • Lindi

Idadi ya Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani Zetu

    Kilwa Masoko

    Anuani ya Posta: 160

    Simu: 0672365354

    Simu: 0672581557

    Barua pepe: ded@kilwadc.go.tz /ictsupport@kilwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Kanuni Binafsi
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa