• Malalamiko |
    • Anuani Zetu |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Kilwa District Council
Kilwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Mikakati ya Halmashauri
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Utumishi na Utawala
      • Elimu ya Msingi
      • Mipango na Takwimu
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Maliasili
    • Vitengo
      • Usafi na Mazingira
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ugavi
      • TEHAMA
      • Nyuki
      • Biashara
      • TASAF
      • Lishe
      • Uvuvi
    • Miji Midogo
      • Masoko
      • Kivinje
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Huduma za Uwekezaji
    • Biashara na Viwanda
    • Madini
    • Uvuvi
    • Utalii
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Mikopo kina Mama na Vijana
    • Huduma za Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Itakayo tekelezwa
  • Machapisho
    • Muongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Mifumo
    • PlanRep
    • FFARS
    • Prem
    • Salary Slip Portal

WATAALAMU WA ELIMU RUFIJI WAJIFUNZA MBINU BORA ZA KUONGEZA UFAHULU WILAYANI KILWA.

Posted on: March 13th, 2025

Jopo la Wataalamu wa Elimu kutoka Wilaya ya Rufiji wamefanya ziara maalumu katika Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa kwa lengo la kubadilishana uzoefu na mbinu za kuboresha viwango vya ufahulu kwa wanafunzi wa Elimu ya Sekondari katika maeneo yao. Ziara hiyo imewakutanisha Maafisa Elimu ngazi ya Wilaya na Kata, Walimu Wakuu na Walimu wa Taaluma wa Shule za Sekondari kutoka Wilaya ya Kilwa na Rufiji ambapo wamejadili Mikakati iliyosaidia kuongeza ufaulu katika Shule za Sekondari wilayani Kilwa. Ziara hiyo imefanyika leo Tarehe 13/03/2025 katika Shule ya Sekondari Kilwa.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Afisa Elimu Taaluma Wilaya ya Kilwa Ndg. Flavian Bujiku ameeleza kuwa, moja ya siri ya mafanikio yao katika kuongeza ufaulu wa wanafunzi katika Shule za Sekondari Wilayani Kilwa ni ushirikiano mzuri kati ya Viongozi wa Halmashauri na Walimu, jambo ambalo limeleta Motisha na kuongeza uwajibikaji katika kazi. Pia Ndg. Bujiku amesema kuwa hatua Madhubuti walizozichukua katika kuhakikisha wanafuta daraja sifuri katika shule nyingi wilayani Kilwa ni Uanzishaji wa kambi za masomo mashuleni ambazo zimesaidia kuongeza muda wa kujifunza na kufanya mazoezi ya Mitihani kwa muda mwingi.

Kwa upande wao Walimu Wakuu na walimu wa taaluma Wilaya ya Kilwa wamesema mbinu nyingine wanazozitumia ni pamoja na kuwaelimisha wazazi kuhusu umuhimu wa kuhakikisha watoto wanapata chakula shuleni, hatua inayochangia kuboresha afya na umakini wa wanafunzi darasani. Pia Waalimu hao wamesema mbali na mbinu hizo pia walimu wanajitoa kwa dhati kuhakikisha wanafunzi wanaelewa masomo yao.

Kwa upande wake Afisa Elimu Sekondari Wilaya ya Rufiji Bi. Theresia Charles amewashukuru Walimu na Maafisa Elimu wa Wilaya ya Kilwa kwa kuwapa mbinu madhubuti za kuinua ufaulu kwa wanafunzi na kuwataka waalimu wa Wilaya ya Rufiji kutumia maarifa na mbinu walizozipata kutoka kwa waalimu wenzao ili kuboresha ufaulu katika Wilaya yao.

Kwasasa Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa imepiga hatua kubwa katika kuhakikisha inatokomeza daraja sifuri katika shule za sekondari kama vile Shule ya Sekondari Kivinje, Shule ya Sekondari Miguruwe, Shule ya Sekondari Ilulu na Shule ya Sekondari ya Kiislam Kilwa.

Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU UTOAJI WA MIKOPO KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 04, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 11, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI. April 25, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MAKALA APONGEZA JITIHADA ZA KURUDISHA MAWASILIANO SOMANGA

    April 10, 2025
  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa Mkono wa Eid kwa watoto wenye mahitaji Maalum Shule ya Msingi Mtanga Wilayani Kilwa.

    March 31, 2025
  • IDARA YA MAENDELEO YA JAMII YATOA MSAADA WA TELEVISHENI KWA GEREZA LA KILWA MASOKO

    April 28, 2025
  • MARAFIKI WA ELIMU WAWASILISHA TAARIFA YA UFUATILIAJI WA MAKUZI YA AWALI YA MTOTO KWA WADAU WA ELIMU KILWA.

    April 28, 2025
  • Tazama Zote

Video

Mkuu wa Wilaya ya Kilwa Akipokea Mwenge wa Uhuru.
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • TARURA GPN
  • Watumishi Portal
  • MIKOPO 10%
  • Mikopo ya Wanawake na Vijana
  • Huduma za Elimu

Tovuti Muhimu

  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ikulu
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu
  • Lindi

Idadi ya Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani Zetu

    Kilwa Masoko

    Anuani ya Posta: 160

    Simu: 0672365354

    Simu: 0672581557

    Barua pepe: ded@kilwadc.go.tz /ictsupport@kilwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Kanuni Binafsi
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa