• Malalamiko |
    • Anuani Zetu |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Kilwa District Council
Kilwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Mikakati ya Halmashauri
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Utumishi na Utawala
      • Elimu ya Msingi
      • Mipango na Takwimu
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Maliasili
    • Vitengo
      • Usafi na Mazingira
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ugavi
      • TEHAMA
      • Nyuki
      • Biashara
      • TASAF
      • Lishe
      • Uvuvi
    • Miji Midogo
      • Masoko
      • Kivinje
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Huduma za Uwekezaji
    • Biashara na Viwanda
    • Madini
    • Uvuvi
    • Utalii
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Mikopo kina Mama na Vijana
    • Huduma za Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Itakayo tekelezwa
  • Machapisho
    • Muongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Mifumo
    • PlanRep
    • FFARS
    • Prem
    • Salary Slip Portal

Wakulima wafurahia Mfumo , Ufuta Tsh.2815/= kwa kilo

Posted on: June 24th, 2018

Wakulima wa zao la ufuta Wilayani Kilwa wameipongeza Halmashauri ya Wilaya Kilwa na Mkoa wa Lindi kwa ujumla kwa kuanzisha mfumo mpya wa Mnada katika ununuzi wa zao hilo.

Akizungumza kwa niaba ya Wakulima, Mwenyekiti wa Chama cha Msingi cha Kibaoni Amcos Bw. Adam Chumi amesema wamefurahishwa sana na uamuzi wa Halmashauri na Mkoa wa kuanzisha  mfumo wa Mnada.

Adam amesema mifumo ambayo ilikua inatumika katika ununuzi Ufuta ilikuwa inawakandamiza  sana na haikuwa na tija kwao hali ambayo ilikuwa inawakatisha tamaa ya kuendelea na kilimo cha ufuta.

”Tunaishukuru sana Halmashauri yetu kwa kuunga Mkono wazo la kutumia Mfumo wa mnada katika uuzaji wa ufuta kwa sababu lina tija kwetu sisi kama wakulima.

Kwa miaka yote ambayo tumekuwa tunalima ufuta hatujawahi kuuza kilo ikazidi Shilingi 2000 lakini kama mlivyoona pale kwenye Mnada kuwa Ufuta utanunuliwa kwa Shilingi 2815 kwa Kilo jambo ambalo tulikuwa tunaliota miaka mingi.

Mwaka jana mimi na wenzangu wachache tuligoma kuuza Ufuta wetu kwa Shilingi 1650 kwa Kilo, tulikaa nao sana mwishoni tukauza kwa Shilingi 1850 kwa Kilo sasa unaweza kuona mwenyewe mabadiliko yaliyoletwa na huu mfumo”. Alisema Adam

Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2018 Bw. Charles Kabeho akifungua Bahasha za Barua za maombi kujua kampuni iliyoshinda kununua Ufuta Wilayani Kilwa. (Picha :Ally Ruambo)

Aidha Adam ameupongeza mfumo  jinsi unavyo fanya malipo ambapo mkulima anaingiziwa pesa katika akaunti yake  baada ya mnada.

“Awali Mfanyabiashara alikua anakulipa fedha tasilimu mkononi jambo ambalo kwa usalama halikuwa zuri lakini pia wengi wao walikua wanakuja na Mizani ambazo zimechezewa swala ambalo lilikua linaongeza unyonyaji kwa mkulima” aliongeza Adam

Kiongozi wa mbio za Mwenge wa Uhuru 2018 Bw. Charles Kabeho (Kushoto) akizungumza na Wananchi wakati wa uzinduizi wa Mradi wa uuzaji wa zao la Ufuta kwa njia ya Mnada Wilayani Kilwa, Kutoka kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Kilwa Mhe. Christopher Ngubiagai (Picha:Ally Ruambo) 

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa Ndg. Zablon Bugingo amewataka Wakulima kutumia fedha zao kwa nidhamu ili ziweze kuwasaidia kuboresha maisha yao  na kuwakumbusha kuweka akiba kwa ajili ya maandalizi ya msimu ujao

“Fedha ambazo mtazipata msizifuje, zitumieni kwa nidhamu ya hali ya juu na mkumbuke kuwa kuna msimu mwingine ambao nao unahitaji maandalizi ya mapema, Sitarajii kusikia kuna mkulima ametumia pesa zote akakosa hata pesa ya akiba ambayo itamuwezesha kugharamia gharama za kuanzisha tena kilimo msimu ujao” alisema Bugingo.

Mnada wa uuzaji wa Ufuta katika kijiji cha Zinga Kibaoni wilayani Kilwa ni miongoni mwa Miradi iliyozinduliwa na mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2018.

Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU UTOAJI WA MIKOPO KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 04, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 11, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI. April 25, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • DC KILWA AITAKA JAMII KUDHIBITI UTUMIAJI WA PLASTIKI ILI KUYALINDA MAZINGIRA.

    June 05, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAKIMBIZWA KILOMETA 173 NA KUTEMBELEA MIRADI 13 YENYE THAMANI YA TSH BILIONI 11 WILAYANI KILWA.

    May 31, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAWEKA JIWE LA MSINGI ZAHANATI YA NJINJO KILWA.

    May 31, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAWEKA JIWE LA MSINGI KWENYE MRADI WA UJENZI WA MNADA WA MIFUGO KILWA

    May 31, 2025
  • Tazama Zote

Video

Mkuu wa Wilaya ya Kilwa Akipokea Mwenge wa Uhuru.
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • TARURA GPN
  • Watumishi Portal
  • MIKOPO 10%
  • Mikopo ya Wanawake na Vijana
  • Huduma za Elimu

Tovuti Muhimu

  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ikulu
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu
  • Lindi

Idadi ya Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani Zetu

    Kilwa Masoko

    Anuani ya Posta: 160

    Simu: 0672365354

    Simu: 0672581557

    Barua pepe: ded@kilwadc.go.tz /ictsupport@kilwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Kanuni Binafsi
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa