• Malalamiko |
    • Anuani Zetu |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Kilwa District Council
Kilwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Mikakati ya Halmashauri
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Utumishi na Utawala
      • Elimu ya Msingi
      • Mipango na Takwimu
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Maliasili
    • Vitengo
      • Usafi na Mazingira
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ugavi
      • TEHAMA
      • Nyuki
      • Biashara
      • TASAF
      • Lishe
      • Uvuvi
    • Miji Midogo
      • Masoko
      • Kivinje
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Huduma za Uwekezaji
    • Biashara na Viwanda
    • Madini
    • Uvuvi
    • Utalii
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Mikopo kina Mama na Vijana
    • Huduma za Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Itakayo tekelezwa
  • Machapisho
    • Muongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Mifumo
    • PlanRep
    • FFARS
    • Prem
    • Salary Slip Portal

Vijiji 11 vyakabidhiwa Mtambo wa kukaushia Mbao

Posted on: November 1st, 2018

Mkuu wa mkoa wa Lindi Mhe. Godfrey Zambi  amewataka   wananchi wanaoishi katika vijiji vinavyomiliki Misitu  kuweka mipango endelevu  ya kuhifadhi Misitu hiyo.

Wito huo ameutoa leo Novemba Mosi, katika Hafla fupi ya kukabidhi Mtambo wa kukaushia Mbao wenye thamani ya Milioni Mia Moja Ishirini  kwa Vijiji Kumi na moja vinavyomiliki misitu, Hafla iliyofanyika katika viunga vya Halmashauri ya wilaya ya Kilwa.

Zambi amewataka wanavijiji hao kuhifadhi misitu hiyo kwa manufaa ya kizazi kilichopo sasa na kizazi kitakacho kuja.

“Msije mkaingiwa na tamaa mkafyeka Misitu yote kwa ajili ya kuuza mbao na matumizi mengine mpaka vizazi vijavyo vikaja kusikia historia tu kuwa hapa zamani kulikuwa na msitu mkubwa” alisema Zambi

Pia Mhe. Zambi amewataka Viongozi ambao wanaongoza vijiji ambavyo vinamiliki Misitu kuwa waaminifu kwa wanainchi wanao waongoza kwa kutumia vizuri dhamana waliyopewa kwa kufanya kazi kwa bidii , uaminifu na uwazi

Zambi amesema kuna baadhi ya viongozi wa Vijiji ambao sio waaminifu wamekuwa wakivuna Miti na kuuza mbao kwa maslahi yao binafsi kitu ambacho ni kinyume na maadili na kuahidi kwa chukulia hatua za kisheria wote watakao bainika kufanya vitendo hivyo.

“Kuna baadhi ya vijiji tumewakamata na kuwaweka ndani viongozi wao, wanavuna mboa na kuziuza kwa maslahi yao binafsi na Kijiji hakifaidiki na chochote. Serikali haiwezi kuvifumbia macho vitendo hivi, tutawakamata na kuwafikisha sehemu husika” alisisitiza Zambi

Aidha Zambi amevitaka vijiji hivyo kuvuna Miti ambayo imekomaa kwa ajili ya matumizi na kuwataka wananchi kuwa mstari wa mbele kuhakikisha wanakabiliana na wavamizi wanao vuna misitu kinyume na Utaratibu.

“Angalieni mfano mzuri kijiji cha Nanjirinji wametunza misitu na wamefaidika, wamejenga Ofisi ya kijiji wameanzisha mradi wa nyumba ya kulala wageni, wana wasaidia wanafunzi ambao wanafaulu kuendelea na masomo lakini pia wana wasaidia wamama wajawazito igeni mfano huu” alihitimisha Zambi

Mkuu wa mkoa wa Lindi Mhe. Godfrey Zambi akiwasha Mtambo wa kukaushia Mbao kuashiria kuanza kutumika rasmi kwa Mtambo huo katika Hafla fupi iliyofanyika katika viunga vya Halmashauri ya wilaya ya Kilwa (Picha na: Ally Ruambo)

Awali akizungumza katika Hafla hiyo Mkuu wa wilaya ya Kilwa Mhe. Christopher Ngubiagai  amevitaka Vijiji kuendelea kutunza Misitu kwa kupanda Miti mingine baada ya kuvuna na kuzielekeza pesa katika shughuli za kimaendeleo baada ya mauzo.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya kilwa Bw. Hatibu Ramadhani ameishukuru taasisi ya Mipingo kwa juhudi wanazofanya katika kuhifadhi misitu na misaada wanayoendelea kuipatia Halmashauri ya wilaya ya kilwa na kuahidi kuendelea kutoa ushirikiano wa hali na mali.

Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU UTOAJI WA MIKOPO KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 04, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 11, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI. April 25, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • BANDARI YA UVUVI KILWA KUKAMILIKA MWEZI JUNI 2025

    May 08, 2025
  • KAMATI YA SIASA YA CCM MKOA WA LINDI YAIPONGEZA KILWA KWA UTEKELEZAJI WA ILANI

    May 07, 2025
  • KILWA YAPIGA HATUA KATIKA KUTOKOMEZA UKATILI WA KIJINSIA DHIDI YA WANAWAKE NA WATOTO

    May 06, 2025
  • WANANCHI, WANAFUNZI NA WATUMISHI KILWA WAJITOKEZA KWA MAZOEZI YA PAMOJA UWANJA WA MWENGE/TAIFA

    May 03, 2025
  • Tazama Zote

Video

Mkuu wa Wilaya ya Kilwa Akipokea Mwenge wa Uhuru.
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • TARURA GPN
  • Watumishi Portal
  • MIKOPO 10%
  • Mikopo ya Wanawake na Vijana
  • Huduma za Elimu

Tovuti Muhimu

  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ikulu
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu
  • Lindi

Idadi ya Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani Zetu

    Kilwa Masoko

    Anuani ya Posta: 160

    Simu: 0672365354

    Simu: 0672581557

    Barua pepe: ded@kilwadc.go.tz /ictsupport@kilwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Kanuni Binafsi
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa