• Malalamiko |
    • Anuani Zetu |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Kilwa District Council
Kilwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Mikakati ya Halmashauri
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Utumishi na Utawala
      • Elimu ya Msingi
      • Mipango na Takwimu
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Maliasili
    • Vitengo
      • Usafi na Mazingira
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ugavi
      • TEHAMA
      • Nyuki
      • Biashara
      • TASAF
      • Lishe
      • Uvuvi
    • Miji Midogo
      • Masoko
      • Kivinje
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Huduma za Uwekezaji
    • Biashara na Viwanda
    • Madini
    • Uvuvi
    • Utalii
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Mikopo kina Mama na Vijana
    • Huduma za Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Itakayo tekelezwa
  • Machapisho
    • Muongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Mifumo
    • PlanRep
    • FFARS
    • Prem
    • Salary Slip Portal

Umasikini Siyo Sifa , Tusibweteke –Ngubiagai

Posted on: April 19th, 2021

Umasikini Siyo Sifa , Tusibweteke –Ngubiagai

Mkuu wa Wilaya ya Kilwa Mhe.Christopher Ngubiagai , ametoa wito kwa wananchi wa Wilaya ya Kilwa kutobweteka na miradi inayosimamiwa na mpango wa kunufaisha kaya masikini Tanzania-TASAF kwani mpango huo ni kwa kaya masikini tu.

Mhe.Ngubiagai ameyasema hayo katika ufunguzi wa semina ya siku moja kwa Waheshimiwa madiwani ,waratibuwa TASAF pamoja na  wakuu wa idara katika Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa.

 Katika semina hiyo, Mhe.Ngubiagai aliwataadharisha pia waratibu watakaohusika katika zoezi la utambuzi wa kaya masikini kutenda haki ili watakaopatikana wawe kweli ni walengwa badala ya kuingiza watu wasiokuwa na sifa. ‘’Ndugu zangu mmeaminiwa , naombeni mkatende haki huko muendako, msionee wala kumpendelea mtu’’ aliongeza Mhe.Mkuu wa Wilaya

Kwa upande wake Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa TASAF Bi. Janeth Madulu, amesema katika awamu hii ya pili ya TASAF awamu ya tatu vijiji vyote tisini katika Wilaya ya Kilwa vitafikiwa na wahitaji wote wataingizwa katika mpango. Mwakilishi huyo aliwaeleza washiriki kuwa ,katika mipango ya awali ya TASAF imepata manufaa makubwa ikiwa ni pamoja na kupunguza kiwango cha umasikini Tanzania bara na Visiwani kwa asilimia sabini jambo ambalo ni hatua kubwa katika utekelezaji.

‘’Kila mwaka tumekuwa tukiwandoa baadhi ya kaya katika orodha ya wanufaika katika mpango wa TASAF , hii ni kutokana na kuhitimu katika hatua za awali’’ , Bi. Janeth Madulu aliongeza kuwa hawa wahitimu ni wale ambao wamefanikiwa kuondoka katika viwango vya chini vya umasikini.

Aliongeza kuwa awamu hii inalenga kufikia kaya milioni moja, laki nne na elfu hamsini ambapo Zaidi ya wanufaika milioni saba wanatarajiwa kufikiwa nchi nzima , hii ni katika Halmashauri zote 184 za Tanzania Bara pamoja na Pemba na Unguja.

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa ambaye pia ni diwani wa kata ya Miguruwe Mhe.Farida Kikoleka amewashauri wasimamizi wa TASAF katika ngazi ya Wilaya kuzingatia upatikanaji wa mitandao ya simu kwani mpaka sasa Zaidi ya vijiji kumi katika Wilaya ya Kilwa havina mawasiliano ya aina yoyote ya simu na hivyo inawawia vigumu kuwafikia wanufaika kwa njia ya simu.

‘’Nakubaliana na mpango wenu wa kuwahudumia wanufaika kwa njia ya mitandao kwa kuwatumia hela kwenye simu zao , lakini Wilaya yetu bado ina changamoto ya mawasiliano, hivyo tafuteni njia mbadala ya kuwafikia wanufaika wanaoishi katika maeneo haya ili kupunguza malalamiko ya wananchi’’ aliongeza Mhe.Kikoleka .

Mratibu wa TASAF katika halmashauri ya Wilaya ya Kilwa Bi. Mwanaidi Salu amesema mpaka sasa Zaidi ya kaya elfu nne zinahudumiwa katika Halmashauri ya Wilaya Kilwa ambapo Zaidi ya shilingi milioni mia sita(600,000,000) zinatolewa kwa wanufaika kwa kila mwaka.

Wilaya ya Kilwa  ina jumla ya tarafa sita, kata ishirini na tatu, vijiji tisini na vitongoji 351.

Katika awamu ya kwanza wa utekelezaji wa mpango wa kupunguza umasikini nchini Tanzania –TASAF vijiji vilivyofikiwa katika Wilaya ya Kilwa ni 52 kati ya vijiji ambapo vijiji 38 havikuwa kwenye mpango wa awali kutokana na sababu mbali mbali.

Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU UTOAJI WA MIKOPO KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 04, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 11, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI. April 25, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MAKALA APONGEZA JITIHADA ZA KURUDISHA MAWASILIANO SOMANGA

    April 10, 2025
  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa Mkono wa Eid kwa watoto wenye mahitaji Maalum Shule ya Msingi Mtanga Wilayani Kilwa.

    March 31, 2025
  • IDARA YA MAENDELEO YA JAMII YATOA MSAADA WA TELEVISHENI KWA GEREZA LA KILWA MASOKO

    April 28, 2025
  • MARAFIKI WA ELIMU WAWASILISHA TAARIFA YA UFUATILIAJI WA MAKUZI YA AWALI YA MTOTO KWA WADAU WA ELIMU KILWA.

    April 28, 2025
  • Tazama Zote

Video

Mkuu wa Wilaya ya Kilwa Akipokea Mwenge wa Uhuru.
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • TARURA GPN
  • Watumishi Portal
  • MIKOPO 10%
  • Mikopo ya Wanawake na Vijana
  • Huduma za Elimu

Tovuti Muhimu

  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ikulu
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu
  • Lindi

Idadi ya Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani Zetu

    Kilwa Masoko

    Anuani ya Posta: 160

    Simu: 0672365354

    Simu: 0672581557

    Barua pepe: ded@kilwadc.go.tz /ictsupport@kilwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Kanuni Binafsi
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa