• Malalamiko |
    • Anuani Zetu |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Kilwa District Council
Kilwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Mikakati ya Halmashauri
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Utumishi na Utawala
      • Elimu ya Msingi
      • Mipango na Takwimu
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Maliasili
    • Vitengo
      • Usafi na Mazingira
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ugavi
      • TEHAMA
      • Nyuki
      • Biashara
      • TASAF
      • Lishe
      • Uvuvi
    • Miji Midogo
      • Masoko
      • Kivinje
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Huduma za Uwekezaji
    • Biashara na Viwanda
    • Madini
    • Uvuvi
    • Utalii
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Mikopo kina Mama na Vijana
    • Huduma za Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Itakayo tekelezwa
  • Machapisho
    • Muongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Mifumo
    • PlanRep
    • FFARS
    • Prem
    • Salary Slip Portal

UFUGAJI NYUKI KWA MAENDELEO ENDELEVU KILWA

Posted on: June 17th, 2025

Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa kupitia Kitengo cha Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira imeendelea kutoa mafunzo ya kitaalamu kuhusu ufugaji nyuki, sambamba na kufanya ukaguzi wa mizinga katika misitu ya mikoko iliyoko katika maeneo ya ukanda wa pwani. Zoezi hili ni sehemu ya mkakati mpana unaolenga kukuza uchumi wa wananchi kupitia shughuli za ufugaji nyuki huku mazingira ya baharini na misitu ya mikoko yakihifadhiwa kwa njia endelevu.


Mafunzo haya yanawajengea uwezo wananchi kuhusu mbinu bora za ufugaji nyuki kwa kutumia teknolojia rafiki kwa mazingira, pamoja na kuwaelimisha juu ya umuhimu wa nyuki katika utunzaji wa mfumo wa ikolojia, hasa katika maeneo ya mikoko ambayo ni mazalia muhimu ya samaki na viumbe hai wa baharini.


Kwa mujibu wa maafisa kutoka Kitengo cha Maliasili, zoezi la ukaguzi wa mizinga lina lengo la kuhakikisha kuwa vifaa vya kufugia nyuki vinaendana na viwango vya kitaalamu na havileti madhara kwa mazingira. Aidha, hatua hii inalenga kuimarisha uzalishaji wa asali na bidhaa nyingine zitokanazo na nyuki, hivyo kuwa chanzo cha kipato kwa kaya za vijijini.


Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa imekuwa mstari wa mbele katika kusisitiza ushirikiano baina ya jamii na taasisi za serikali katika utekelezaji wa miradi ya uhifadhi wa mazingira. Kwa mantiki hiyo, Kitengo cha Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira kinatoa wito kwa wadau wote  ikiwemo mashirika yasiyo ya kiserikali, sekta binafsi na wananchi – kushiriki kikamilifu katika kuendeleza elimu ya ufugaji nyuki kwa lengo la kuifikisha kwa jamii pana zaidi.


Mradi huu unatarajiwa kuchangia katika utekelezaji wa malengo ya maendeleo endelevu hususan Malengo ya kutokomeza Umaskini,13 Kuchukua Hatua Dhidi ya Mabadiliko ya Tabianchi na Kuhifadhi Mazingira ya Ardhi.


Juhudi hizi ni ushahidi wa dhamira ya Halmashauri ya Kilwa katika kuunganisha maendeleo ya kijamii na kiuchumi na ajenda ya utunzaji wa mazingira, kwa manufaa ya sasa na ya vizazi vijavyo.

Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU UTOAJI WA MIKOPO KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 04, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 11, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI. April 25, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI LINDI WATAKIWA KUTUMIA FURSA YA USHIRIKI WA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA KUJIFUNZA

    June 22, 2025
  • WADAU MBALIMBALI KATIKA BANDA LA MKOA WA LINDI KWENYE MAADHIMISHO YA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA DODOMA

    June 21, 2025
  • MADIWANI KILWA WAAGWA KWA HAFLA YA HESHIMA

    June 19, 2025
  • HONGERA HALMASHAURI YA WILAYA YA KILWA KWA KUPATA HATI SAFI YA CAG

    June 19, 2025
  • Tazama Zote

Video

Mkuu wa Wilaya ya Kilwa Akipokea Mwenge wa Uhuru.
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • TARURA GPN
  • Watumishi Portal
  • MIKOPO 10%
  • Mikopo ya Wanawake na Vijana
  • Huduma za Elimu

Tovuti Muhimu

  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ikulu
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu
  • Lindi

Idadi ya Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani Zetu

    Kilwa Masoko

    Anuani ya Posta: 160

    Simu: 0672365354

    Simu: 0672581557

    Barua pepe: ded@kilwadc.go.tz /ictsupport@kilwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Kanuni Binafsi
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa