• Malalamiko |
    • Anuani Zetu |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Kilwa District Council
Kilwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Mikakati ya Halmashauri
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Utumishi na Utawala
      • Elimu ya Msingi
      • Mipango na Takwimu
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Maliasili
    • Vitengo
      • Usafi na Mazingira
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ugavi
      • TEHAMA
      • Nyuki
      • Biashara
      • TASAF
      • Lishe
      • Uvuvi
    • Miji Midogo
      • Masoko
      • Kivinje
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Huduma za Uwekezaji
    • Biashara na Viwanda
    • Madini
    • Uvuvi
    • Utalii
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Mikopo kina Mama na Vijana
    • Huduma za Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Itakayo tekelezwa
  • Machapisho
    • Muongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Mifumo
    • PlanRep
    • FFARS
    • Prem
    • Salary Slip Portal

"Tutataifisha Mashamba yasiyoendelezwa'' - Dc kilwa

Posted on: September 2nd, 2018

Kilwa,

Katika kuhakikisha ardhi inawanufaisha wananchi wa wilaya ya Kilwa na taifa kwa jumla.Mkuu wa wilaya hiyo,Christopher Ngubiagai amesema mashamba yaliyotelekezwa na kusababisha mapori wilayani humu yatataifishwa na kugawiwa kwa watu wenye uwezo wa kuyaendeleza.

Ngubiagai ametoa tamko hilo leo katika kijiji cha Marendego alipokuwa anazungumza na wananchi kupitia mkutano wa hadhara,uliofanyika kijijini hapo.

Amesema nijambo lisilokubalika kuona baadhi ya wananchi wilayani humu wakiwa hawana maeneo ya kulima,huku baadhi ya wananchi wamehodhi maeneo makubwa na kushindwa kuyaendeleza.Tena yakiwa yametelekezwa kwa miaka mingi na kusababisha mapori ambayo yamegeuka na kuwa hifadhi zisizo rasimi za wanyama waharibifu wa mazao ya kilimo.

Kufuatia hali hiyo,mkuu huyo wawilaya ya Kilwa mkoani Lindi amewataka wananchi waliotelekeza mashamba yao kwa muda mrefu wasafishe haraka na wahakikishe yanakuwa safi kabla ya mwezi Desemba mwaka huu.Kwasababu kuanzia mwezi huo mashamba yatakayo kutwa hayasafishwa yatagawiwa kwa watu wenye huitaji na wanaoweza kuyaendeleza.

Amewataka viongozi na watendaji wa vijiji waanze kuyabaini na kuorodhesha mashamba yaliyotelekezwa kwamuda mrefu ili ifikapo mwezi huo iwe rahisi kuyagawa.Kwasababu yatakuwa yanajulikana yapo wapi na kwamuda gani yamebaki bila kufanyiwa kazi.

Ngubiagai aliwatoa hofu wananchi kwamba zoezi hilo litatendeka kwa haki bila kupendelea na kumuonea mtu.Huku akiwataka viongozi na watendaji kuwa makini na waongozwe na uadilifu, uaminifu na uzalendo.Nayeyote atayeharibu zoezi hilo kwa masilahi binafsi atakuwa anathibitisha kuwa hasitahili kuwa kiongozi.

Mkuu huyo wa wilaya katika kuonesha hajakurupuka kufikia uamuzi huo alisema amebaini kuwa mashamba mengi yaliyotelekezwa yamehodhiwa na watu wanaoishi nje ya wilaya ya Kilwa.Hata wanapoombwa wawape wanaotaka kuendeleza wanakataa.Huku wengine wakiuza kwa bei kubwa ili yasinunuliwe.

"Ukiuliza unaambiwa shamba lilikuwa la babu wa babu yake,mwenyewe anaishi Temeke.Hapa ameliacha nakugeuka pori linalotunza nguruwe.Kama yupo Temeke achukue aishi nalo hukohuko lakini likibaki Kilwa bila kuendeleza nagawa kwawenyehuitaji,"alisema Ngubiagai.

Mbali na onyo hilo, Ngubiagai amewataka wananchi wilayani humu kutoa ushirikiano na kuwathamini watumishi wa serikali na kuacha mara moja tabia ya kuwazuia wasitimize na kutekeleza majukumu yao.Kwani baadhi yao wanatishia usalama wawatumishi wanapotekeleza majukumu yao.

Alitolea mfano tukio lililotokea juzi,kwamba baadhi ya wananchi waliwafurusha na kuwatishia maisha wataalamu wa idara ya ardhi wa halmashauri ya wilaya hiyo ambao walikuwa wanapima mipaka ya vijiji viwili vilivyokwenye mgogoro wa mipaka.Hata hivyo wanachi wakijiji kimoja kati ya hivyo viwili waliwafurusha wataalamu hao nakusababisha washindwe kuendelea na kazi.

"Tabia hiyo naomba ikome,iwe mwanzo na mwisho.Wapeni ushirikiano na msiporidhika na jambo fulani fuateni na kuzingatia sheria.Siyo kuwatishia maisha na kuwazuia kufanya kazi.Hao ni watoto wawenzenu, nibinadamu kama nyinyi,"alisema kwa hasira Ngubiagai.

Wilaya ya Kilwa inahekta takribani 800,000 za ardhi zinazofaa kwa kilimo.Hata hivyo baadhi ya maeneo yamehodhiwa na watu ambao wameshindwa kuyaendeleza.Hali inayosababisha kuwepo mapori na vichaka hata katikatika ya vijiji,miji midogo ya Kivinje na Masoko na pembeni ya barabara kuu.

Credit - Muungwana Blog

Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU UTOAJI WA MIKOPO KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 04, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 11, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI. April 25, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MAKALA APONGEZA JITIHADA ZA KURUDISHA MAWASILIANO SOMANGA

    April 10, 2025
  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa Mkono wa Eid kwa watoto wenye mahitaji Maalum Shule ya Msingi Mtanga Wilayani Kilwa.

    March 31, 2025
  • IDARA YA MAENDELEO YA JAMII YATOA MSAADA WA TELEVISHENI KWA GEREZA LA KILWA MASOKO

    April 28, 2025
  • MARAFIKI WA ELIMU WAWASILISHA TAARIFA YA UFUATILIAJI WA MAKUZI YA AWALI YA MTOTO KWA WADAU WA ELIMU KILWA.

    April 28, 2025
  • Tazama Zote

Video

Mkuu wa Wilaya ya Kilwa Akipokea Mwenge wa Uhuru.
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • TARURA GPN
  • Watumishi Portal
  • MIKOPO 10%
  • Mikopo ya Wanawake na Vijana
  • Huduma za Elimu

Tovuti Muhimu

  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ikulu
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu
  • Lindi

Idadi ya Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani Zetu

    Kilwa Masoko

    Anuani ya Posta: 160

    Simu: 0672365354

    Simu: 0672581557

    Barua pepe: ded@kilwadc.go.tz /ictsupport@kilwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Kanuni Binafsi
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa