• Malalamiko |
    • Anuani Zetu |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Kilwa District Council
Kilwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Mikakati ya Halmashauri
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Utumishi na Utawala
      • Elimu ya Msingi
      • Mipango na Takwimu
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Maliasili
    • Vitengo
      • Usafi na Mazingira
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ugavi
      • TEHAMA
      • Nyuki
      • Biashara
      • TASAF
      • Lishe
      • Uvuvi
    • Miji Midogo
      • Masoko
      • Kivinje
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Huduma za Uwekezaji
    • Biashara na Viwanda
    • Madini
    • Uvuvi
    • Utalii
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Mikopo kina Mama na Vijana
    • Huduma za Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Itakayo tekelezwa
  • Machapisho
    • Muongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Mifumo
    • PlanRep
    • FFARS
    • Prem
    • Salary Slip Portal

TIMU YA WASICHANA KILWA "KILWA PRINCESS" YAZINDULIWA RASMI NA KUFANYA HARAMBEE KWA WADAU

Posted on: September 6th, 2025

Katika kuendeleza vipaji vya michezo kwa wasichana wilayani Kilwa, timu ya wasichana "Kilwa Princess" imezinduliwa rasmi na kufanya harambee maalum ya kuchangisha fedha na vifaa ili kuiwezesha timu hiyo kufikia mafanikio ya juu katika tasnia ya michezo.


Hafla hiyo imefanyika katika ukumbi wa Mashujaa Business Centre, ambapo mgeni rasmi alikuwa Katibu Tawala wa Wilaya ya Kilwa, Ndg. Yusuf Mwinyi, aliyemuwakilisha Mkuu wa Wilaya.


Akizungumza katika hafla hiyo, Katibu Mkuu Ndg, Juma Muhando ameeleza mafanikio ya awali ya timu hiyo huku akiiomba serikali na wadau wa michezo kuisaidia timu kwa mahitaji muhimu ikiwemo vifaa vya kufanyia mazoezi kwa vile jezi za michezo, mipira, pamoja na bajeti kwa ajili ya safari za kimichezo ili kuiwezesha kushiriki mashindano mbalimbali kitaifa na kimataifa.


Kwa upande wake, Katibu Tawala Ndg. Yusuf Mwinyi, amesema kuwa serikali iko tayari kuiunga mkono timu hiyo , ikiwa ni sehemu ya juhudi katika kuinua michezo kwa wasichana na vijana kwa ujumla. Pia ametoa wito kwa wadau wa michezo, mashirika binafsi, taasisi za kijamii, na watu binafsi kujitokeza kwa wingi ili kusaidia timu hiyo chipukizi.


Naye Afisa Utamaduni, Sanaa na Michezo wa Wilaya ya Kilwa, Bi. Veneranda Maro, ameipongeza timu ya Kilwa Princess kwa uthubutu wao wa kujitokeza na kuanzisha timu hiyo ya wasichana, hatua aliyosema ni muhimu kwa maendeleo ya michezo ya wanawake nchini. Amewahimiza wachezaji kuzingatia nidhamu, bidii, na kujituma zaidi ili kufikia viwango vya juu vya kitaifa na kimataifa.


Katika harambee hiyo, michango mbalimbali ilitolewa, ikiwemo fedha taslimu na vifaa vya michezo, huku baadhi ya wadau wakiahidi kuendelea kutoa msaada wa mara kwa mara kwa timu hiyo.


Kilwa Princess ni moja ya timu ya wasichana wilayani Kilwa ambayo imeanzishwa kwa lengo la kuibua, kukuza na kuendeleza vipaji vya michezo miongoni mwa wasichana, pamoja na kuwapa nafasi ya kushiriki katika maendeleo ya kijamii kupitia michezo hiyo

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI HALMASHAURI YA WILAYA YA KILWA September 03, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU UTOAJI WA MIKOPO KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 04, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • DED KILWA AKABIDHI PIKIPIKI KWA MAAFISA MAENDELEO YA JAMII ILI KUIMARISHA UTOAJI WA HUDUMA KWA WANANCHI

    September 09, 2025
  • TIMU YA WASICHANA KILWA "KILWA PRINCESS" YAZINDULIWA RASMI NA KUFANYA HARAMBEE KWA WADAU

    September 06, 2025
  • MSAJILI WA VYAMA VYA SIASA AWAPIGA MSASA VIONGOZI WA VYAMA VYA SIASA KILWA

    September 01, 2025
  • WAJIBU INSTITUTE NA PPRA WATOA MAFUNZO KWA MAKUNDI MAALUM JUU YA FURSA ZA UNUNUZI WA UMMA

    September 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

Mkuu wa Wilaya ya Kilwa Akipokea Mwenge wa Uhuru.
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • TARURA GPN
  • Watumishi Portal
  • MIKOPO 10%
  • Mikopo ya Wanawake na Vijana
  • Huduma za Elimu

Tovuti Muhimu

  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ikulu
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu
  • Lindi

Idadi ya Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani Zetu

    Kilwa Masoko

    Anuani ya Posta: 160

    Simu: 0672365354

    Simu: 0672581557

    Barua pepe: ded@kilwadc.go.tz /ictsupport@kilwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Kanuni Binafsi
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa