Timu ya UMITASHUMTA ya Wilaya ya Kilwa yaagwa kuelekea mashindano ya ngazi ya mkoa baada ya maandalizi ya Kimichezo ya siku 6 kuanzia tarehe 18 hadi 22 mei 2025 katika shule ya msingi Ukombozi, ghafla hiyo fupi imefanywa Tarehe 22 Mei 2025 na mashindano hayo ya kimkoa yatafanyika kuanzia tarehe 23 hadi 26 Mei 2026 Mkoani Lindi.
Akimuwakilisha Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa Ndg. Omary Mkuwili amewataka wanamichezo hao kuzingatia nidhamu, mshikamano na uzalendo katika mashindano hayo ili waweze kushinda mashindano hayo na kuahikikisha wanaiwqkilisha vizuri Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa.
Kaimu Afisa Elimu Msingi, Bi. Amina Mkadamu, amewataka walimu wa michezo na wachezaji kuwa na mshikamano na kutoa ushirikiano wa karibu ili kuhakikisha timu ya Wilaya ya Kilwa inafanya vizuri na kurudi na ushindi.
Kwa upande wake, Afisa Utamaduni, Sanaa na Michezo wa Wilaya, Bi. Veneranda Maro, amewahimiza kucheza kwa nidhamu na kufuata taratibu zote za mashindano ili kulinda heshima ya wilaya ya Kilwa.
Kilwa Masoko
Anuani ya Posta: 160
Simu: 0672365354
Simu: 0672581557
Barua pepe: ded@kilwadc.go.tz /ictsupport@kilwadc.go.tz
Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa