• Malalamiko |
    • Anuani Zetu |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Kilwa District Council
Kilwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Mikakati ya Halmashauri
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Utumishi na Utawala
      • Elimu ya Msingi
      • Mipango na Takwimu
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Maliasili
    • Vitengo
      • Usafi na Mazingira
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ugavi
      • TEHAMA
      • Nyuki
      • Biashara
      • TASAF
      • Lishe
      • Uvuvi
    • Miji Midogo
      • Masoko
      • Kivinje
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Huduma za Uwekezaji
    • Biashara na Viwanda
    • Madini
    • Uvuvi
    • Utalii
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Mikopo kina Mama na Vijana
    • Huduma za Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Itakayo tekelezwa
  • Machapisho
    • Muongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Mifumo
    • PlanRep
    • FFARS
    • Prem
    • Salary Slip Portal

SERIKALI YASAINI MIKATABA UJENZI WA MADARAJA 13 YALIYOHARIBIWA NA MVUA LINDI. BILIONI 140 KUTUMIKA

Posted on: October 7th, 2024

Serikali imesaini mikataba mitano itakayowezesha kuanza ujenzi wa madaraja 13 katika sehemu za barabara zilizoathiriwa na Mvua za El-Nino na Kimbunga Hidaya katika Mkoa wa Lindi ambapo jumla ya Shilingi Bilioni 140 zitatumika katika utekelezaji huo.


Akizungumza mara baada ya kushuhudia utiaji saini mikataba hiyo Wilayani Kilwa Mkoani Lindi leo Oktoba 07, 2024, Waziri wa Ujenzi Innocent Bashungwa amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutambua ukubwa wa athari ya miundombinu ya madaraja na makalvati katika Mkoa wa Lindi na kutenga kiasi hicho cha fedha kwa ajili ya kurudisha upya miundombinu hiyo.


“Dhamira ya Mheshimiwa Rais katika Mkoa wa Lindi ni kujenga upya madaraja yaliyoathiriwa katika maeneo yote ili mvua zitakapoanza kunyesha wananchi watakuwa salama na mawasiliano ya barabara yanakuwa ya uhakika”, amesema Bashungwa.


Amesema ujenzi wa madaraja hayo utatekelezwa katika barabara kuu ya Malendego – Nangurukuru – Lindi – Mingoyo na barabara za Mkoa za Nangurukuru – Liwale, Kiranjeranje – Namichiga, Liwale – Nachingwea na barabara ya Tingi – Chumo – Kipatimu.


Aidha, Bashungwa ameeleza kuwa Serikali ipo katua za mwisho za kusaini mkataba na Mkandarasi kwa ajili ya kujenga upya barabara ya Mtwara - Lindi - Pwani hadi Dar es Salaam ambapo utekelezaji utaanza awamu ya kwanza kuanzia Mtwara - Mingoyo na baadaye kuendelea kutafuta fedha kwa ajili ya awamu ya pili kuanzia Mingoyo hadi Dar - es Salaam.


Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Zainab Telack ameahidi kutoa ushirikiano wa karibu na kuwasimamia Wakandarasi wote waliopata kazi za ujenzi wa madaraja 13 katika maeneo yote yaliyoathiriwa na mvua za El-Nino na Kimbunga Hidaya ili waweze kukamilisha kazi kwa wakati na ubora unaotakiwa.


Akitoa taarifa ya mradi, Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara (TANROADS) Mhandisi Mohamed Besta ameeleza kuwa kazi za ujenzi wa madaraja 13 yatatekelezwa kwa muda wa Miezi 10 kwa kufuata taratibu zote za kitaalam na kusimamiwa na Kitengo cha TECU kutoka kwa Wakala huo.

Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU UTOAJI WA MIKOPO KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 04, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 11, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI. April 25, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MAKALA APONGEZA JITIHADA ZA KURUDISHA MAWASILIANO SOMANGA

    April 10, 2025
  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa Mkono wa Eid kwa watoto wenye mahitaji Maalum Shule ya Msingi Mtanga Wilayani Kilwa.

    March 31, 2025
  • IDARA YA MAENDELEO YA JAMII YATOA MSAADA WA TELEVISHENI KWA GEREZA LA KILWA MASOKO

    April 28, 2025
  • MARAFIKI WA ELIMU WAWASILISHA TAARIFA YA UFUATILIAJI WA MAKUZI YA AWALI YA MTOTO KWA WADAU WA ELIMU KILWA.

    April 28, 2025
  • Tazama Zote

Video

Mkuu wa Wilaya ya Kilwa Akipokea Mwenge wa Uhuru.
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • TARURA GPN
  • Watumishi Portal
  • MIKOPO 10%
  • Mikopo ya Wanawake na Vijana
  • Huduma za Elimu

Tovuti Muhimu

  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ikulu
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu
  • Lindi

Idadi ya Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani Zetu

    Kilwa Masoko

    Anuani ya Posta: 160

    Simu: 0672365354

    Simu: 0672581557

    Barua pepe: ded@kilwadc.go.tz /ictsupport@kilwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Kanuni Binafsi
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa