• Malalamiko |
    • Anuani Zetu |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Kilwa District Council
Kilwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Mikakati ya Halmashauri
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Utumishi na Utawala
      • Elimu ya Msingi
      • Mipango na Takwimu
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Maliasili
    • Vitengo
      • Usafi na Mazingira
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ugavi
      • TEHAMA
      • Nyuki
      • Biashara
      • TASAF
      • Lishe
      • Uvuvi
    • Miji Midogo
      • Masoko
      • Kivinje
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Huduma za Uwekezaji
    • Biashara na Viwanda
    • Madini
    • Uvuvi
    • Utalii
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Mikopo kina Mama na Vijana
    • Huduma za Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Itakayo tekelezwa
  • Machapisho
    • Muongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Mifumo
    • PlanRep
    • FFARS
    • Prem
    • Salary Slip Portal

Mkuu wa Mkoa wa Lindi afikisha kilio Wizarani

Posted on: October 28th, 2018

Mkuu wa Mkoa wa lindi Mhe. Godfrey Zambi ameiomba Wizara ya maliasili na utalii kuutazama Mkoa wa Lindi kwa Jicho Tatu katika sekta ya utalii.

Ombi hilo ameliwasilisha  leo Oktoba 28 katika hitimisho la Tamasha la Ishirini na Tatu la Utamaduni wa Mtanzania ambalo kwa mwaka 2018 lilichagizwa na jamii ya watu wa Mkoa wa Lindi katika Kijiji cha Makumbusho Jijini Dar es salaam.

Zambi amesema Mkoa wa Lindi una Historia ya aina yake na Vivutio Vingi vya utalii lakini bado miundo mbinu ya kuvifikia vivutio hivyo siyo ya kuridhisha.

“Mhe. Naibu waziri Mkoa wa Lindi una vivutio vingi na vizuri sana kama wengi wetu hapa tunavyojua lakini bado miundo mbinu ya kuvifikia vivutio hivyo sio rafiki, kuna baadhi ya sehemu ukienda kwa kutumia Gari inakulazimu uliache mbali uanze kutembea kwa mguu” alisema Zambi

Pia Zambi amehoji juu ya Kumbukumbu ya Vita vya majimaji kufanyika Songea na si Kijiji cha Nandete wilayani  Kilwa ambapo ndiyo chimbuko la Vita vya majimaji.

“Ukisoma historia utaona jinsi vita ya majimaji ilivyokuwa na jinsi  waasisi  walivyapambana na wakolini lakini tunashangaa maadhimisho ya kumbukumbu za vita ya majimaji kila mwaka yanafanyika Songea badala ya Kilwa ambako ndio chimbuko lake” 

Akitolea ufafanuzi Hoja za Mkuu wa mkoa wa Lindi, Naibu waziri wa Maliasili na utalii (Mb) Mhe. Japhet Hasunga amesema serikali iko makini na inatambua changamoto zilizopo katika sekta ya utalii na kuahidi kuendelea kuzitatua kadri iwezekanavyo.

“Ndugu yangu Zambi tunatambua changamoto ni nyingi na serikali iko macho kuhakikisha inaendelea kuboresha sekta ya Utalii kwa kutatua changamoto ambazo zinaenekana kuikabili sekta ya Maliasili na utalii, pia nikutoe wasiwasi kuhusu suala la Nandete tunafahamu kuwa huko ndiyo chimbuko la vita ya majimaji.

Pia Hasunga amewataka waandaaji wa matamashaya utamaduni kuendelea kuandaa matamasha mengine na kuitaka Mikoa ambayo haijafanya Tamasha la utamaduni kufanya na kufungua milango kwa mikoa iliyokwishafanya kufanya tena kama watahitaji.

Naibu waziri wa Maliasili na utalii (Mb) Mhe. Japhet Hasunga akipata maelekezo kutoka kwa Mtaalamu katika Banda la Makumbusho ya Taifa kuhusu Samaki ambaye alipotea miaka milioni sitini na tano iliyopita na kuonekana tena mwaka 2003 katika kijiji cha Songo Mnara wilayani kilwa (Picha: Ally Ruambo)

Aidha Mhe. Hasunga amewataka Watanzania kujenga tabia ya kutembelea vivutio mbalimbali ambavyo vinapatika katika Mikoa mbalimbali nchini Tanzania.

“Msisubiri hadi sikukuu ndio muende huko panga muda wako nenda kale maisha, ukichukua likizo unaenda kafanye utalii, unakula maisha unarudi ukiwa na akili mpya ya kufanya kazi” alisema Hasunga

Katika hatua nyingine Naibu waziri ametoa maagizo kwa Mikoa yote ambayo haijajenga Nyumba za asili katika Kijiji cha Makumbusho kujenga Nyumba, Mkoa wa Lindi uchapishe Kitabu ambacho kitaelezea fursa zinazopatikana Mkoani humo na jinsi ya kuzifikia ili kiweze kutumika kama kitabu cha ziada kwa wanafunzi na watafiti mbalimbali, Mkoa wa Lindi ujenge makumbusho ambayo yatahifadhi historia na tamaduni za mkoa wa Lindi, Makumbusho kuandaa vitini vitavyoelezea sehemu na vifaa vya kujengea nyumba za asili katika kijiji cha makumbusho na kuvigawa Mikoani na taasisi ziendelee kujitokeza katika kuhifadhi na kutangaza tamaduni.

Awali akizungumza katika tamasha hilo Mkurugenzi mkuu wa makumbusho ya taifa Prof. Audax Mabula amemshukuru Waziri mkuu Mhe. Kassim Majaliwa kwa ushirikiano aliouonyesha katika kuhakikisha tamasha la utamaduni wa Watu wa Lindi mwaka 2018 Linafanikiwa.

Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU UTOAJI WA MIKOPO KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 04, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 11, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI. April 25, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MAKALA APONGEZA JITIHADA ZA KURUDISHA MAWASILIANO SOMANGA

    April 10, 2025
  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa Mkono wa Eid kwa watoto wenye mahitaji Maalum Shule ya Msingi Mtanga Wilayani Kilwa.

    March 31, 2025
  • IDARA YA MAENDELEO YA JAMII YATOA MSAADA WA TELEVISHENI KWA GEREZA LA KILWA MASOKO

    April 28, 2025
  • MARAFIKI WA ELIMU WAWASILISHA TAARIFA YA UFUATILIAJI WA MAKUZI YA AWALI YA MTOTO KWA WADAU WA ELIMU KILWA.

    April 28, 2025
  • Tazama Zote

Video

Mkuu wa Wilaya ya Kilwa Akipokea Mwenge wa Uhuru.
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • TARURA GPN
  • Watumishi Portal
  • MIKOPO 10%
  • Mikopo ya Wanawake na Vijana
  • Huduma za Elimu

Tovuti Muhimu

  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ikulu
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu
  • Lindi

Idadi ya Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani Zetu

    Kilwa Masoko

    Anuani ya Posta: 160

    Simu: 0672365354

    Simu: 0672581557

    Barua pepe: ded@kilwadc.go.tz /ictsupport@kilwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Kanuni Binafsi
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa