• Malalamiko |
    • Anuani Zetu |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Kilwa District Council
Kilwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Mikakati ya Halmashauri
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Utumishi na Utawala
      • Elimu ya Msingi
      • Mipango na Takwimu
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Maliasili
    • Vitengo
      • Usafi na Mazingira
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ugavi
      • TEHAMA
      • Nyuki
      • Biashara
      • TASAF
      • Lishe
      • Uvuvi
    • Miji Midogo
      • Masoko
      • Kivinje
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Huduma za Uwekezaji
    • Biashara na Viwanda
    • Madini
    • Uvuvi
    • Utalii
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Mikopo kina Mama na Vijana
    • Huduma za Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Itakayo tekelezwa
  • Machapisho
    • Muongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Mifumo
    • PlanRep
    • FFARS
    • Prem
    • Salary Slip Portal

Mkurugenzi amwaga zawadi kwa wafanyakazi bora mei mosi 2021, awaasa waendelee kuchapa kazi

Posted on: May 1st, 2021


Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa Ndugu Renatus Mchau amewaasa watumishi wake kuendelea uchapa kazi katika maeneo yao mbali mbali ili kuleta tija kwa Halmashuari na taifa kwa ujumla.

Wito huo umetolewa ikiwa ni katika siku ya maadhimisho ya Wafanyakazi kote duniani ambapo kwa Mkoa wa Lindi siku hiyo iliadhimishwa katika viwanja vya Ilulu Katika Manispaa ya Lindi. ‘’Ndugu zangu, nyie mliopata zawadi ni sehemu ya watumishi wote, nawapongeza kwa kuwa kazi yenu imetambulika ila endeleeni kuchapa kazi Zaidi na zaidi’’ alisisitiza ndugu Mchau.

Mgeni rasmi katika maadhimisho hayo Kimkoa Mhe.Sara Chiwanga (Mkuu wa Wilaya ya Liwale) ambaye alimuwakilisha mkuu wa mkoa wa Lindi Mhe.Godfrey Zambi. Mgeni Rasmi aliwataka watumishi wote kuendelea kuchapa kazi ili taifa liweze kupiga hatua kimaendeleo. ‘’Nimesikiliza hotuba yenu, yale yaliyo ndani ya uwezo wetu naahidi kuyafanyia kazi mara moja na yale ya Kitaifa nitayafikisha kwa wahusika’’ aliongeza Mhe.Chiwanga.

Mgeni rasmi aliwapongeza waajiri waliowazawadia watumishi wao zawadi zenje tija huku akiwasisitiza waajiri wengine pia kuhakikisha wanawatambua watumishi wao bora na kuwapongeza.

Kwa upande wa Wilaya ya Kilwa wafanyakazi Hodari kumi na moja walitambukuwa na kuzadiwa zawadi ya fedha taslimi laki tano (500,000) kila mmoja pamoja na cheti kutoka vyama vya wafanyakazi.

Watumishi waliotambuliwa ni kutoka idara mbali mbali ndani ya halmashauri kuanzia wale waliopo ofisi kuu za Halmashauri na wale kutoka sehemu mbali mbali za kutolea huduma kama vituo vya Afya , shuleni , vijiji pamoja na kata.

Mkuu wa Idara ya Utumishi na Utawala Bi.Jovita Buyobe aliwataja watumishi hao na nagfasi zao katika mabano  kuwa ni Bi. Zuhurafu Mohamed Machenza(Katibu Muhtasi), Mohamed Litumbui (Mtendaji wa Kata ya Miguruwe),Bi.Tatu Kamtande(Mtendaji wa kata ya Kivinje) na Mwanahamii Omari (Mtendaji Kijiji ch Lihimalyao).

Idara ya Afya iliwakilishwa na watumishi watatu ambao ni Dr.Alfred Chinyeu(Kituo cha Afya Tingi) ,Bi.Getrude  Nyaki (Muuguzi-Hospitali ya Kinyonga) na Bi.Anna Kapungu ambaye ni muhudumu wa Afya katika Zahanati ya Mkarango.

Watumishi wengine waliozawadiwa ni Said Pilla (Afisa Kilimo), Mwl.Selemani Msofe (Mkuu wa shule ya sekondari Kivinje), Mwl.Francis Siaga (Shule ya Msingi Nangorombe) na Mwl.Rabia Kilindo kutoka shule ya Nasaya.

Bi Buyobe alieleza kuwa upatikanaji wa watumishi hao umezingatia vigezi vingi ikiwa ni pamoja na watumishi kupigiwa kura za wazi na za siri, mazingira yao ya utumishi lakini kikubwa wamepatikana kutokana na uchapakazi wao.

Mmoja wa viongozi wa chama cha wafanyakazi wa Serikali za Mitaa(TALGWU) ndugu Hajji Limba alimpongeza  Mkurugenzi Mtendaji kwa kuwatambua wafanyakazi hodari na kuwazawadia kwa wakati. ‘’Nadhani mmeona baadhi ya waajiri wamekuja pale na ahadi lakini sisi Mkurugenzi wetu Bw.Mchau alibeba kabisa fedha taslimu na kila mmoja amepata kile alichostahili,  sisi tuna Mkurugnzi Jembe na tunamuahidi tutaendelea kuchapa kazi’’  alimalizia Ndugu Limba.

Maadhimisho ya siku ya wafanyakazi kitafa yamefanyika katika Viwanja vya CCM –Kirumba jijini Mwanza ambapo Mgeni Rasmi alikuwa Mhe.Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU UTOAJI WA MIKOPO KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 04, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 11, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI. April 25, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MAKALA APONGEZA JITIHADA ZA KURUDISHA MAWASILIANO SOMANGA

    April 10, 2025
  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa Mkono wa Eid kwa watoto wenye mahitaji Maalum Shule ya Msingi Mtanga Wilayani Kilwa.

    March 31, 2025
  • IDARA YA MAENDELEO YA JAMII YATOA MSAADA WA TELEVISHENI KWA GEREZA LA KILWA MASOKO

    April 28, 2025
  • MARAFIKI WA ELIMU WAWASILISHA TAARIFA YA UFUATILIAJI WA MAKUZI YA AWALI YA MTOTO KWA WADAU WA ELIMU KILWA.

    April 28, 2025
  • Tazama Zote

Video

Mkuu wa Wilaya ya Kilwa Akipokea Mwenge wa Uhuru.
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • TARURA GPN
  • Watumishi Portal
  • MIKOPO 10%
  • Mikopo ya Wanawake na Vijana
  • Huduma za Elimu

Tovuti Muhimu

  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ikulu
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu
  • Lindi

Idadi ya Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani Zetu

    Kilwa Masoko

    Anuani ya Posta: 160

    Simu: 0672365354

    Simu: 0672581557

    Barua pepe: ded@kilwadc.go.tz /ictsupport@kilwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Kanuni Binafsi
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa