• Malalamiko |
    • Anuani Zetu |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Kilwa District Council
Kilwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Mikakati ya Halmashauri
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Utumishi na Utawala
      • Elimu ya Msingi
      • Mipango na Takwimu
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Maliasili
    • Vitengo
      • Usafi na Mazingira
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ugavi
      • TEHAMA
      • Nyuki
      • Biashara
      • TASAF
      • Lishe
      • Uvuvi
    • Miji Midogo
      • Masoko
      • Kivinje
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Huduma za Uwekezaji
    • Biashara na Viwanda
    • Madini
    • Uvuvi
    • Utalii
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Mikopo kina Mama na Vijana
    • Huduma za Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Itakayo tekelezwa
  • Machapisho
    • Muongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Mifumo
    • PlanRep
    • FFARS
    • Prem
    • Salary Slip Portal

KUMBUKIZI YA MIAKA 114 YA MAJIMAJI YAFANA KIPATIMU

Posted on: August 16th, 2019

KUMBUKIZI YA MIAKA 114 YA MAJIMAJI YAFANA KIPATIMU

Maadhimisho ya miaka 114 tangu kumalizika kwa vita vya majimaji vilivyopiganwa kati ya waafrika wa kusini mwa Tanganyika na Wajerumani yamefanyika katika kijiji Nandete kata ya Kipatimu Wilayani Kilwa.

Maadhimisho hayo ambayo kwa miaka kadhaa yamekuwa yakifanyika nje ya Wilaya ya Kilwa Mkoa wa Lindi yalihudhuriwa na wanannchi wengi wakiwemo wazee wa maeneo husika ambao walitoa historian a kueleza kuwa vita vya Maji maji chimbuko lake ni Kata ya Kipatimu Wilaya ya Kilwa na si vinginevyo kama ambavyo baadhi watu wanavyoeleza na kuelewa.

Mgeni rasmi katika kumbukizi hizo Mhe. Christopher Ngubiagai ambaye ni mkuu wa Wilaya ya Kilwa aliwapongeza wazee wa vijiji vinavyoznguka eneo hilo kwa kuendelea kutunza historia pamoja na mnara wa kumbukumbu wa vita hivyo iliyowekwa na Rais wa awamu ya nne Mhe.Dr.Jakaya Mrisho Kikwete mwaka 2010 katika kijiji cha Nandete katika kata ya Kipatimu. Mnara huo wenye majina ya wahanga wa vita hivyo ni sehemu muhimu ya historia  ambapo wadadisi mbalimbali wa mambo ya kale hufika katika eneo hilo kupata historia.

Akiongea kwenye maadhimisho hayo, Mhe.Ngubiagai aliwapongeza wazee wa eneo hilo na kuahidi kuendelea kushirikiana na wadau mbalimbali wa ndani na nje ya nchi katika kutangaza  historia hiyo kwa faida wakazi wa eneo hilo na taifa kwa ujumla.

Mmoja wa wazee wa Vijiji hivyo ambaye pia ni mwana historia mzee Batoli Mweo alitoa historia ya chanzo cha vita hivyo kuwa kitendo cha wakoloni wa Kijerumani waliofika katika eneo hilo kulazimisha kilimo cha zao la Pamba jambo ambalo liliwakasirisha wazee hao na kuamua kung’oa pamba na ndiyo ikawa chanzo cha vita hivyo vilivyodumu kwa miaka miwili kuanzia mwaka 1905 hadi 1907.

Katika kata ya Kipatimu pia kuna vivutio vingine kama mapango ya Nang’oma katika kijiji cha Nandembo ambayo yanasemekana kwa makubwa Zaidi barani Afrika yakiwa na urefu wa Zaidi ya kilomita saba ambacho  hakijatangazwa kiasi cha kutosha. Mzee Batoli anaeleza kuwa katika mapango hayo ambayo yanaaminika kutumika kama maficho ya waafika katika kipindi cha vita hivyo pamoja na kiongozi wao Kinjekitile Ngwale kuna kuna vivutio vingi na wageni kadhaa wamekuwa wakifika kujifunza ingawa ni kwa kiasi kidogo jambo ambalo linawanyima mapato lakini pia fursa ya kujulikana duniani kote tofauti na mapango kama ya Amboni mkoani Tanga ambayo ni madogo Zaidi ukilinganisha na mapango ya Nang’oma.

Maadhimisho hayo yalienda sambamba na sherehe za kijadi pamoja na uwekaji shada la maua na silaha za jadi zilizowekwa na viongozi wa serikali, viongozi wa jadi na viongozi wa dini.

Viongozi wengine waliohudhuria maadhimisho hayo ni pamoja na Mbunge wa Kilwa Kaskazini Mhe.Vedasto Ngombale,kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa Adv.Godfrey Jafari, waheshimiwa madiwani pamoja na wananchi kutoka ndani na nje ya Wilaya ya Kilwa.

Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU UTOAJI WA MIKOPO KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 04, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 11, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI. April 25, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • BANDARI YA UVUVI KILWA KUKAMILIKA MWEZI JUNI 2025

    May 08, 2025
  • KAMATI YA SIASA YA CCM MKOA WA LINDI YAIPONGEZA KILWA KWA UTEKELEZAJI WA ILANI

    May 07, 2025
  • KILWA YAPIGA HATUA KATIKA KUTOKOMEZA UKATILI WA KIJINSIA DHIDI YA WANAWAKE NA WATOTO

    May 06, 2025
  • WANANCHI, WANAFUNZI NA WATUMISHI KILWA WAJITOKEZA KWA MAZOEZI YA PAMOJA UWANJA WA MWENGE/TAIFA

    May 03, 2025
  • Tazama Zote

Video

Mkuu wa Wilaya ya Kilwa Akipokea Mwenge wa Uhuru.
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • TARURA GPN
  • Watumishi Portal
  • MIKOPO 10%
  • Mikopo ya Wanawake na Vijana
  • Huduma za Elimu

Tovuti Muhimu

  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ikulu
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu
  • Lindi

Idadi ya Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani Zetu

    Kilwa Masoko

    Anuani ya Posta: 160

    Simu: 0672365354

    Simu: 0672581557

    Barua pepe: ded@kilwadc.go.tz /ictsupport@kilwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Kanuni Binafsi
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa