• Malalamiko |
    • Anuani Zetu |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Kilwa District Council
Kilwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Mikakati ya Halmashauri
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Utumishi na Utawala
      • Elimu ya Msingi
      • Mipango na Takwimu
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Maliasili
    • Vitengo
      • Usafi na Mazingira
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ugavi
      • TEHAMA
      • Nyuki
      • Biashara
      • TASAF
      • Lishe
      • Uvuvi
    • Miji Midogo
      • Masoko
      • Kivinje
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Huduma za Uwekezaji
    • Biashara na Viwanda
    • Madini
    • Uvuvi
    • Utalii
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Mikopo kina Mama na Vijana
    • Huduma za Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Itakayo tekelezwa
  • Machapisho
    • Muongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Mifumo
    • PlanRep
    • FFARS
    • Prem
    • Salary Slip Portal

KILWA YASHIRIKI LINDI MINING EXPO 2025 KUTANGAZA FURSA ZA UWEKEZAJI

Posted on: June 13th, 2025

Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa imeshiriki kwa mafanikio makubwa katika Maonesho ya Madini na Fursa za Uwekezaji (LINDI MINING EXPO 2025), ambayo yamewaleta pamoja wadau wa maendeleo, wawekezaji na wananchi kutoka ndani na nje ya mkoa wa Lindi. Lengo kuu la ushiriki huo ni kutangaza kwa upana fursa mbalimbali za kiuchumi na utajiri wa maliasili zinazopatikana ndani ya Wilaya ya Kilwa.


Kupitia banda maalum lililoandaliwa kwa umahiri na kitaalamu, Halmashauri ya Kilwa imeonesha kwa vitendo ukubwa wa fursa zilizopo kwa ajili ya uwekezaji endelevu. Miongoni mwa fursa hizo ni pamoja na uwepo wa madini ya viwandani na vito katika maeneo mbalimbali; uchumi wa bluu unaojumuisha uvuvi wa kisasa, ufugaji wa samaki na uzalishaji wa mazao ya baharini kama mwani; kilimo cha mazao ya biashara ikiwemo korosho, mbaazi na ufuta kwa kutumia ardhi yenye rutuba; pamoja na fursa za uvuvi wa kisasa na uanzishaji wa viwanda vya kuchakata mazao ya uvuvi.


Pia, Wilaya ya Kilwa imebarikiwa kuwa na vivutio vya utalii wa kihistoria kama Kilwa Kisiwani na Songo Mnara pamoja na visiwa vyenye mandhari ya kuvutia; Bandari ya Kilwa Masoko ambayo ina nafasi kubwa ya kupanuliwa kwa ajili ya shughuli za biashara na usafirishaji; misitu ya asili na ya kupandwa kwa matumizi ya mbao na miradi ya uhifadhi wa mazingira; na visiwa vinavyofaa kwa uwekezaji katika sekta ya hoteli, mapumziko na utalii wa kiikolojia.


Aidha, kupitia maonesho haya, Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa imeendelea kuhamasisha wananchi kushiriki katika maendeleo ya taifa, ikiwemo kuhimiza ushiriki mpana katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025.

Kaulimbiu ya mwaka huu ni.


"Madini na Uwekezaji Fursa ya Kiuchumi Lindi.

Shiriki Uchaguzi Mkuu 2025."


Ushiriki wa Halmashauri ya Kilwa katika maonesho haya ni sehemu ya mkakati mpana wa kuitangaza Wilaya hiyo kama kitovu cha fursa za kiuchumi, chenye mazingira rafiki kwa uwekezaji, huku ikilenga kukuza ajira, uchumi wa mtu mmoja mmoja na maendeleo ya kijamii kwa ujumla.

Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU UTOAJI WA MIKOPO KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 04, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 11, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI. April 25, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI LINDI WATAKIWA KUTUMIA FURSA YA USHIRIKI WA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA KUJIFUNZA

    June 22, 2025
  • WADAU MBALIMBALI KATIKA BANDA LA MKOA WA LINDI KWENYE MAADHIMISHO YA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA DODOMA

    June 21, 2025
  • MADIWANI KILWA WAAGWA KWA HAFLA YA HESHIMA

    June 19, 2025
  • HONGERA HALMASHAURI YA WILAYA YA KILWA KWA KUPATA HATI SAFI YA CAG

    June 19, 2025
  • Tazama Zote

Video

Mkuu wa Wilaya ya Kilwa Akipokea Mwenge wa Uhuru.
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • TARURA GPN
  • Watumishi Portal
  • MIKOPO 10%
  • Mikopo ya Wanawake na Vijana
  • Huduma za Elimu

Tovuti Muhimu

  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ikulu
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu
  • Lindi

Idadi ya Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani Zetu

    Kilwa Masoko

    Anuani ya Posta: 160

    Simu: 0672365354

    Simu: 0672581557

    Barua pepe: ded@kilwadc.go.tz /ictsupport@kilwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Kanuni Binafsi
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa