• Malalamiko |
    • Anuani Zetu |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Kilwa District Council
Kilwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Mikakati ya Halmashauri
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Utumishi na Utawala
      • Elimu ya Msingi
      • Mipango na Takwimu
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Maliasili
    • Vitengo
      • Usafi na Mazingira
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ugavi
      • TEHAMA
      • Nyuki
      • Biashara
      • TASAF
      • Lishe
      • Uvuvi
    • Miji Midogo
      • Masoko
      • Kivinje
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Huduma za Uwekezaji
    • Biashara na Viwanda
    • Madini
    • Uvuvi
    • Utalii
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Mikopo kina Mama na Vijana
    • Huduma za Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Itakayo tekelezwa
  • Machapisho
    • Muongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Mifumo
    • PlanRep
    • FFARS
    • Prem
    • Salary Slip Portal

KILWA YAPOKEA RUZUKU YA CHANJO ZA MIFUGO KWA AJILI YA KUKABILI MAGONJWA HATARI

Posted on: June 26th, 2025

Katika juhudi za kuimarisha Afya ya mifugo na kuongeza uzalishaji wa mazao yake, Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa imepokea jumla ya dozi 79,000 za chanjo dhidi ya homa ya mapafu kwa ng’ombe na dozi 204,000 za chanjo dhidi ya ugonjwa wa Sotoka kwa mbuzi na kondoo, chanjo hizo zimetolewa na Wizara ya Mifugo na Uvuvi kama sehemu ya utekelezaji wa kampeni ya kitaifa ya chanjo za ruzuku kwa mwaka wa fedha 2024/2025, na zimepokelewa rasmi kupitia kitengo cha Mifugo cha Wilaya ya Kilwa.

Akizungumza wakati wa mapokezi ya chanjo hizo, Mkuu wa kitengo cha Mifugo wilayani Kilwa, Ndg. Sifael Mwanyhesi, amesema kuwa hatua hiyo inalenga kuwasaidia wafugaji kwa kupunguza gharama za upatikanaji wa huduma za chanjo, pia Ndg, Mwanyhesi amesema chanjo hizo zitatolewa kwa ruzuku ambapo kila ng’ombe atachanjwa kwa shilingi 500 tu badala ya shilingi 1,000, huku mbuzi na kondoo wakichanjwa kwa shilingi 300 badala ya shilingi 600.

“Hii ni fursa adhimu kwa wafugaji wetu. Kupitia bei hii ya ruzuku, tunatarajia kuona ushiriki mkubwa kutoka kwa jamii, hii itasaidia kupunguza vifo vya mifugo, kuongeza usalama wa chakula na kukuza uchumi wa kaya zinazotegemea ufugaji,” amesema Ndg. Mwanyhesi.

Ndg. Mwanyhesi. Ameeleza kuwa serikali inalenga kuchanja angalau asilimia 70% ya mifugo nchini ili kufikia viwango vya kimataifa vya afya ya mifugo, hatua itakayowezesha mifugo ya Tanzania kushindana kwenye soko la kimataifa kwa ubora.

Aidha, ametoa wito kwa wafugaji wote wilayani Kilwa kujiandaa kushiriki kikamilifu katika kampeni hiyo ya chanjo, akisisitiza kuwa Afya bora ya mifugo ni msingi wa ustawi wa jamii nzima.

Chanjo hizo zinatarajiwa kuanza kutolewa hivi karibuni katika vijiji mbalimbali vya Wilaya ya Kilwa kupitia ratiba maalum itakayopangwa na wataalamu wa mifugo wa halmashauri hiyo.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI HALMASHAURI YA WILAYA YA KILWA September 03, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU UTOAJI WA MIKOPO KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 04, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 11, 2024
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • KILWA DC YAANZA KWA KISHINDO SHIMISEMITA

    August 16, 2025
  • MTANDAO WA BMU WAELEZA FAIDA ZA ZIARA YA MAFUNZO MKOANI TANGA

    August 15, 2025
  • DED NA TIMU YA UFUATILIAJI KILWA WAFANYA UKAGUZI WA MIRADI YA MAENDELEO

    August 14, 2025
  • KAMATI ZA MAANDALIZI YA SHEREHE ZA MAJIMAJI KILWA ZAKUTANA KUJADILI MAANDALIZI YA SHEREHE HIZO

    August 13, 2025
  • Tazama Zote

Video

Mkuu wa Wilaya ya Kilwa Akipokea Mwenge wa Uhuru.
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • TARURA GPN
  • Watumishi Portal
  • MIKOPO 10%
  • Mikopo ya Wanawake na Vijana
  • Huduma za Elimu

Tovuti Muhimu

  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ikulu
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu
  • Lindi

Idadi ya Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani Zetu

    Kilwa Masoko

    Anuani ya Posta: 160

    Simu: 0672365354

    Simu: 0672581557

    Barua pepe: ded@kilwadc.go.tz /ictsupport@kilwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Kanuni Binafsi
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa