• Malalamiko |
    • Anuani Zetu |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Kilwa District Council
Kilwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Mikakati ya Halmashauri
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Utumishi na Utawala
      • Elimu ya Msingi
      • Mipango na Takwimu
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Maliasili
    • Vitengo
      • Usafi na Mazingira
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ugavi
      • TEHAMA
      • Nyuki
      • Biashara
      • TASAF
      • Lishe
      • Uvuvi
    • Miji Midogo
      • Masoko
      • Kivinje
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Huduma za Uwekezaji
    • Biashara na Viwanda
    • Madini
    • Uvuvi
    • Utalii
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Mikopo kina Mama na Vijana
    • Huduma za Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Itakayo tekelezwa
  • Machapisho
    • Muongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Mifumo
    • PlanRep
    • FFARS
    • Prem
    • Salary Slip Portal

Kilwa yang'aa matumizi ya tovuti

Posted on: March 24th, 2018

  Kilwa, 

             Halmashauri ya wilaya ya kilwa imepongezwa kwa kua miongoni mwa halmashauri  zinazo ongoza kwa utoaji taarifa kupitia tovuti.

Pongezi  hizo  zimetolewa  na Mtafiti mwandamizi kutoka taasisi ya Urban Institute ya nchini Marekani Dokta Fenohasina Rakotondrazaka Maret, alipotembelea  halmashauri  hio  kukagua  maendeleo  ya  mradi  pamoja  na kusikiliza  changamoto zinazowakabili katika kutekeleza majukumu yao.

Dkt. Fenohasina amesema wao kama wasimamizi wa mradi wamefurahishwa na utendaji wa halmashauri ya wilaya ya kilwa katika swala zima la kuhabarisha  wananchi  kuhusiana na matukio na miradi mbalimbali inayotekelezwa na  halmashauri kupitia tovuti kama ilivyo agizwa na  Waziri wa nchi, Or- Tamisemi Mhe. Selemani Jafo kua tovuti ziwe majokofu ya habari na si magofu ya habari.

“Tumefurahishwa na muenendo wa halmashauri katika swala zima la matumizi ya tovuti katika kuwa habarisha wananchi juu ya mambo mbalimbali kuhusiana na halmashauri yenu

Sana sana tumefurahishwa na uwazi juu ya taarifa mbalimbali, mfano nimeona bajeti ya halmashauri kwa mwaka wa fedha 2017/18 ikiwa imewekwa katika tovuti ambapo kila mwananchi anaweza kuona lakini pia tumeona miradi mbalimbali inayotekelezwa na Halmashauri pamoja na thamani zake lakini tumefurahishwa zaidi na jinsi mnavyoitangaza tovuti yenu” alisema  Bi. Fenohasina

Aidha ameitaka halmashauri iendelee na kasi hio ili izidi kua mfano bora kwa tovuti zinginae za Mamlaka ya serikali za mitaa.

Kaimu mkuu wa kitengo cha teknolojia ya habari na mawasiliano  Bw. Yusuph Rajabu (Katikati) akifafanua jambo kwa wajumbe kutoka  Mradi wa uimarishaji Mifumo ya sekta za Umma (PS3) walipotembelea Halmashauri ya wilaya ya Kilwa kukagua maendeleo ya mradi pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili.

Akiwashukuru kwa ujio wao Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Kilwa Bw. Sylivester Mashema  amesema  amefurahi  na  anashukuru  kwa ujio wao na  kusikia  changamoto mbalimbali zinazowakabili  na kuahidi kuendelea kushirikiana na kitengo cha Tehama na idara zingine katika kuhakikisha wananchi wanapata habari sahihi na kwa muda sahihi.

“Nashukuru kwa uji wenu na kusikiliza changamoto zinazotukabili licha ya mafanikio tunayo yapata, na sisi kama halmashauri tutaendelea kushirikiana na kitengo cha Tehama kuhakikisha tunawahabarisha wanachi kuhusiana na mambo mbalimbali” alisema Mashema

Kwa upande wake Kaimu mkuu wa kitengo cha Teknolojia ya habari na mawasiliano (TEHAMA) Bw. Yusuph Rajabu amesema  wamejipanga kuhakikisha kua wananchi wana habarika kupitia tovuti ya halmashauri na vyanzo vingine vya habari vinavyo simamiwa na Halmashauri.

Pia amewataka wananchi kushirikiana na Halmashauri kwa kuwasilisha malalamiko yao kupitia tovuti ya Halmashauri ili yapatiwe ufumbuzi kwa maendeleo ya Wananchi.

“Tume anzisha mfumo wa kupokea malalamiko kupitia tovuti kwakua tumeona wananchi wengi walioko mbali na Ofisi za Halmashauri inakua ngumu kwao kuwasilisha malalamiko yao moja kwa moja au kupitia sanduku la maoni ambalo mara nyingi hupatikana maofisini tu

Mfano mtu alie kuepo Kipatimu huko anawezaje kufikisha malalamiko yake kwa urahisi ofisini kwa mkurugenzi? Itamlazimu atumie gharama kuja mpaka wilayani na kurudi kwa kuliona hilo tumeanzisha mfumo maalumu wa kupokea malalamiko yao ambapo ataenda kwenye simu yake au kompyuta iliyounganishwa na huduma ya intaneti na kuandika neno www.kilwadc.go.tz itafunguka katika muonekano huu

Baada ya hapo utabofya sehemu ya kwanza ilio andikwa Malalamiko na itafunguka  kama inavyo onekana hapo chini

Mlalamikaji ataweka malalamiko yake kwa kujaza taarifa na mwisho atamaliza kwa kuituma kwa kubofya sehemu ilio andikwa Send na malalamiko yake yatapokelewa moja kwa moja na kufanyiwa kazi.

Ila niwakumbushe tu kua malalamiko yawe na ukweli yasiwe ya uzushi kwa nia ya kuchafua mtu au idara fulani kwa sababu binafsi, isije kutokea mtu amekosana na mtumishi katika mambo yao binafsi akayaleta kama malalmiko kwa ajili ya kumkomoa au kumchafua" alisisitiza Bw. Yusuph.

Halmashauri ya wilaya ya kilwa ni Halmashauri ya kwanza  kwa kua na watembeleaji  wengi  katika tovuti katika mkoa wa lindi ikiwa na watembeleaji zaidi ya 2620 ikifuatiwa na halmashauri ya wilaya ya Ruangwa yenye watembeleaji 670.

Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU UTOAJI WA MIKOPO KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 04, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 11, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI. April 25, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • BANDARI YA UVUVI KILWA KUKAMILIKA MWEZI JUNI 2025

    May 08, 2025
  • KAMATI YA SIASA YA CCM MKOA WA LINDI YAIPONGEZA KILWA KWA UTEKELEZAJI WA ILANI

    May 07, 2025
  • KILWA YAPIGA HATUA KATIKA KUTOKOMEZA UKATILI WA KIJINSIA DHIDI YA WANAWAKE NA WATOTO

    May 06, 2025
  • WANANCHI, WANAFUNZI NA WATUMISHI KILWA WAJITOKEZA KWA MAZOEZI YA PAMOJA UWANJA WA MWENGE/TAIFA

    May 03, 2025
  • Tazama Zote

Video

Mkuu wa Wilaya ya Kilwa Akipokea Mwenge wa Uhuru.
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • TARURA GPN
  • Watumishi Portal
  • MIKOPO 10%
  • Mikopo ya Wanawake na Vijana
  • Huduma za Elimu

Tovuti Muhimu

  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ikulu
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu
  • Lindi

Idadi ya Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani Zetu

    Kilwa Masoko

    Anuani ya Posta: 160

    Simu: 0672365354

    Simu: 0672581557

    Barua pepe: ded@kilwadc.go.tz /ictsupport@kilwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Kanuni Binafsi
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa