• Malalamiko |
    • Anuani Zetu |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Kilwa District Council
Kilwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Mikakati ya Halmashauri
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Utumishi na Utawala
      • Elimu ya Msingi
      • Mipango na Takwimu
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Maliasili
    • Vitengo
      • Usafi na Mazingira
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ugavi
      • TEHAMA
      • Nyuki
      • Biashara
      • TASAF
      • Lishe
      • Uvuvi
    • Miji Midogo
      • Masoko
      • Kivinje
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Huduma za Uwekezaji
    • Biashara na Viwanda
    • Madini
    • Uvuvi
    • Utalii
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Mikopo kina Mama na Vijana
    • Huduma za Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Itakayo tekelezwa
  • Machapisho
    • Muongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Mifumo
    • PlanRep
    • FFARS
    • Prem
    • Salary Slip Portal

Kilwa yamuunga mkono Rais JPM kwa vitendo

Posted on: June 5th, 2018

  Kilwa,

        Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa imeendelea kuunga mkono kauli ya Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli ya kuifanya Tanzania kuwa Nchi ya viwanda.

Kauli hiyo imetekelezwa leo juni 5 baada ya Katibu tawala Mkoa wa Lindi Ndg. Ramadhani Kaswa kuweka jiwe la msingi katika  kiwanda cha kuchakata magogo cha Sound and Fair katika kijijji cha Nanjirinji wilayani kilwa kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Lindi Mhe. Godfrey Zambi. 

Akizungumza wakati wa uwekaji wa jiwe hilo la msingi Ndg. Kwasa amesema amefurahi kuona kampuni ya Sound and Fair inaunga mkono serikali ya awamu ya tano chini ya Mhe. Magufuli ya kuifanya Tanzania kuwa nchi ya viwanda na kuahidi kuendelea kutoa ushirikiano kwa kampuni hiyo na nyingine ambazo zinahitaji kuwekeza katika Mkoa wa Lindi.

“Nimefurahishwa na jitihada zenu za kuhakikisha kua Tanzania inakua nchi ya viwanda kwa kuanzisha kiwanda hiki cha kuchakata magogo, sisi kama mkoa tunaahidi kuendelea kuwapa ushirikiano na wale wengine ambao wanataka kuja kuwekeza katika Mkoa wa lindi tunawakaribisha” alisema Kaswa.

Katibu tawala Mkoa wa Lindi Ndg. Ramadhan Kaswa (wa pili kutoka kushoto) akikata utepe kuashiria kuwekwa rasmi kwa jiwe la Msingi katika Kiwanda cha Sound and Fair katika kijiji cha Nanjirinji, kutoka kulia ni Katibu tawala Wilaya ya Kilwa Ndg.Haji Mbaruku akifuatiwa na Mwenyekiti wa Kamati ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira Mhe. Msati.  

Pia ameipongeza Kampuni ya sound and fair kwa kutoa ajira kwa vijna wa kitanzania  pamoja na kuchangia pato la kijiji na taifa kwa ujumla kupitia kodi mbalimbali inayoendelea kuzilipa.

“Nimeona katika hotuba yenu kuwa hadi sasa mmekwisha lipa zaidi ya million 150 kutokana na kodi mbalimbali na mmetoa ajira kwa wataalamu mbalimbali kutoka hapa hapa Tanzania na wananchi kutoka vijiji vinavyo izunguka Nanjirinji na mnategemea kutoa ajira 60 za kudumu na zaidi ya 100 za muda mfupi jambo ambalo ni zuri kwani itasaidia sana kuongeza kipato cha vijana watakao ajiriwa” aliongeza Kaswa

Mkurugenzi wa kiwanda cha Sound and Fair Ndg. James Laizer (wa kwanza kulia) akitoa maelekezo kwa Katibu tawala Mkoa wa Lindi Ndg. Ramadhani Kaswa (katikati) na Mkuu wa Wilaya ya Kilwa Mhe. Christopher Ngubiagai (wa kwanza kushoto) ya jinsi mtambo unavyo fanya kazi walipo tembelea kiwandani hapo kuweka jiwe la msingi. 

Nae mkuu wa wilaya ya Kilwa mhe Christopher Ngubiagai ameishukuru kampuni ya Sound and fair kwa uamuzi wao wa kuwekeza wilayani kilwa na kuwataka wananchi waache kuharibu Mazingira kwa kukata Miti, kuharibu vyanzo vya Maji na maeneo mbalimbali yalitengwa kwa  ajiri ya hifadhi na kuahidi kuwachukulia hatua kali dhidi yao.

“Hatuwezi kuwafumbia macho ambao wanaharibu mazingira yetu kwa shughuli zao mbalimbali, kama nilivyosema jana wakati tunapanda Miti pale katika kijiji cha Makangaga kuwa serikali itawachukulia hatua kali ambao watakaidi agizo la kutoka sehemu zile ambazo haziruhuiswi kufanya shughuli yeyote ya kibinadamu” alisema ngubiagai

Katibu tawala Mkoa wa Lindi Ndg. Ramadhan Kaswa akipanda Mti katika kiunga cha Kiwanda cha Sound and Fair baada ya kuweka Jiwe la msingi. 

Kwa upande wake mkurugenzi wa kampuni ya sound and fair Ndg. James Laizer ameiomba serikali kupitia mkuu wa mkoa kuwasaidia katika kurekebisha barabara ya Kiranjeranje mpaka Nanjirinji  ambayo ndio muhimili mkubwa katika usafirishaji wa bidhaa ambazo zinaingia na kutoka kiwandani baada ya kuchakatwa.

Aidha Ndg. Laizer ameiomba serikali kuimarisha ushirikiano na wadau mbalimbali katika kutokomeza tatizo la uvunaji haramu wa mazao ya masitu ambayo imekua tishio kubwa kwa ustawi wa makampuni yanayojishughulisha na biashara ya mazao ya misitu.

Uwekaiji wa jiwa la msingi Katika kiwanda cha Sound and Fair ni miongoni mwa shughuli zilizofanyika katika kusindikiza maadhimisho wiki ya Mazingira duniani ngazi ya Mkoa, Mkoa wa Lindi ambayo yamefanyika katika kijiji cha nanjirinji.

Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU UTOAJI WA MIKOPO KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 04, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 11, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI. April 25, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MAONESHO YA MADINI RUANGWA 2025 YAWAPA WANANCHI FURSA MPYA ZA UWEKEZAJI

    June 11, 2025
  • KILWA NA FURSA ZA UWEKEZAJI KATIKA MAONESHO YA MADINI MKOANI LINDI

    June 11, 2025
  • WANAWAKE KATA YA TINGI WAANDAA DUA MAALUM KUMUOMBEA MHE. RAIS SAMIA

    June 08, 2025
  • DC KILWA AITAKA JAMII KUDHIBITI UTUMIAJI WA PLASTIKI ILI KUYALINDA MAZINGIRA.

    June 05, 2025
  • Tazama Zote

Video

Mkuu wa Wilaya ya Kilwa Akipokea Mwenge wa Uhuru.
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • TARURA GPN
  • Watumishi Portal
  • MIKOPO 10%
  • Mikopo ya Wanawake na Vijana
  • Huduma za Elimu

Tovuti Muhimu

  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ikulu
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu
  • Lindi

Idadi ya Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani Zetu

    Kilwa Masoko

    Anuani ya Posta: 160

    Simu: 0672365354

    Simu: 0672581557

    Barua pepe: ded@kilwadc.go.tz /ictsupport@kilwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Kanuni Binafsi
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa