• Malalamiko |
    • Anuani Zetu |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Kilwa District Council
Kilwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Mikakati ya Halmashauri
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Utumishi na Utawala
      • Elimu ya Msingi
      • Mipango na Takwimu
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Maliasili
    • Vitengo
      • Usafi na Mazingira
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ugavi
      • TEHAMA
      • Nyuki
      • Biashara
      • TASAF
      • Lishe
      • Uvuvi
    • Miji Midogo
      • Masoko
      • Kivinje
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Huduma za Uwekezaji
    • Biashara na Viwanda
    • Madini
    • Uvuvi
    • Utalii
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Mikopo kina Mama na Vijana
    • Huduma za Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Itakayo tekelezwa
  • Machapisho
    • Muongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Mifumo
    • PlanRep
    • FFARS
    • Prem
    • Salary Slip Portal

KATIBU MKUU WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI AWATAKA WAFUGAJI KUIMARISHA USHIRIKIANO NA SERIKALI KATIKA KUKABILIANA NA CHANGAMOTO ZA MIFUGO

Posted on: July 4th, 2025

Kilwa, Lindi – Julai 4, 2025

Katibu Mkuu, Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bi. Agnes Meena, ametoa wito kwa wafugaji wilayani Kilwa kushiriki kikamilifu katika juhudi za serikali za kuimarisha ushirikiano katika kutatua changamoto zinazoikumba mifugo yao.

Bi. Meena ametoa kauli hiyo wakati wa uzinduzi kampeni ya kitaifa ya chanjo na utambuzi wa mifugo uliofanyika katika kijiji cha Matandu, kata ya Kivinje. Lengo ni kutoa chanjo dhidi ya magonjwa hatari kwa mifugo ikiwemo Mdondo (Newcastle Disease), Mapafu ya Ng’ombe (CBPP) na Sotoka kwa Mbuzi na Kondoo.

“Kama ambavyo mkulima hawezi kuzalisha mwaka mzima bila chanzo thabiti cha maji, vivyo hivyo mfugaji hawezi kuwa na mifugo yenye afya bila miundombinu ya msingi kama vile visima na vituo vya huduma za mifugo. Ni wakati wa wafugaji wetu kushiriki kwa dhati katika uboreshaji wa huduma hizi,” amesema Bi. Meena.

Aidha, ameeleza kuwa serikali iko tayari kusaidia maeneo yenye changamoto kubwa, lakini masuala madogo yanayohitaji nguvu kazi au rasilimali kidogo yanapaswa kushughulikiwa kwa ushirikiano wa moja kwa moja kati ya jamii ya wafugaji na serikali za mitaa. Pia alibainisha kuwa chanjo kwa kuku zitatolewa bila malipo, lakini ng’ombe, mbuzi na kondoo mfugaji atachangia nusu ya gharama za chanjo husika. Pia amehimiza usimamizi madhubuti na ufuatiliaji wa wataalamu wa mifugo ili kuhakikisha chanjo zinatolewa kama ilivyokusudiwa.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Kilwa, Katibu Tawala wa Wilaya hiyo, Ndg. Yusuf Mwinyi, amewataka wafugaji kuchangamkia fursa ya chanjo za ruzuku ili kulinda mifugo dhidi ya magonjwa hatari yanayoathiri uzalishaji na soko la mifugo.

Naye Daktari wa Mifugo kutoka Halmasahuri hiyo Dkt. Nyalekwa Mashimo ameeleza kuwa tayari halmashauri imepokea jumla ya dozi 300,000 za chanjo ya mdondo kwa kuku, dozi 79,000 za CBPP kwa ng’ombe, na dozi 204,000 za chanjo ya sotoka kwa mbuzi na kondoo. Alibainisha kuwa tangu tarehe 30 Juni 2025 hadi sasa Halmasauri imefanikiwa kutoa chanjo 30,000 kwa kuku sawa na asilimia 10 ya dozi iliyotolewa.

Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU UTOAJI WA MIKOPO KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 04, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 11, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI. April 25, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • KILWA YAPOKEA PIKIPIKI 11 KWA AJILI YA CHANJO NA HUDUMA MBALIMBALI ZA MIFUGO.

    July 11, 2025
  • SERIKALI KUENDELEA KUWEKA MAZINGIRA WEZESHI KWA NGO's LINDI

    July 10, 2025
  • SERIKALI YAFANYA UKAGUZI WA MIRADI YA MASHIRIKA YASIYO YA KISERIKALI WILAYANI KILWA

    July 09, 2025
  • HALMASHAURI YA KILWA YADUMISHA USHIRIKIANO NA MASHIRIKA YASIYO YA KISERIKALI KUPITIA JUKWAA LA PAMOJA

    July 01, 2025
  • Tazama Zote

Video

Mkuu wa Wilaya ya Kilwa Akipokea Mwenge wa Uhuru.
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • TARURA GPN
  • Watumishi Portal
  • MIKOPO 10%
  • Mikopo ya Wanawake na Vijana
  • Huduma za Elimu

Tovuti Muhimu

  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ikulu
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu
  • Lindi

Idadi ya Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani Zetu

    Kilwa Masoko

    Anuani ya Posta: 160

    Simu: 0672365354

    Simu: 0672581557

    Barua pepe: ded@kilwadc.go.tz /ictsupport@kilwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Kanuni Binafsi
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa