• Malalamiko |
    • Anuani Zetu |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Kilwa District Council
Kilwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Mikakati ya Halmashauri
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Utumishi na Utawala
      • Elimu ya Msingi
      • Mipango na Takwimu
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Maliasili
    • Vitengo
      • Usafi na Mazingira
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ugavi
      • TEHAMA
      • Nyuki
      • Biashara
      • TASAF
      • Lishe
      • Uvuvi
    • Miji Midogo
      • Masoko
      • Kivinje
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Huduma za Uwekezaji
    • Biashara na Viwanda
    • Madini
    • Uvuvi
    • Utalii
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Mikopo kina Mama na Vijana
    • Huduma za Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Itakayo tekelezwa
  • Machapisho
    • Muongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Mifumo
    • PlanRep
    • FFARS
    • Prem
    • Salary Slip Portal

Halmashauri kujenga stendi ya Mabasi Nangurukuru

Posted on: September 23rd, 2018

Kilwa,

               Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa iko mbioni kutekeleza mradi wa ujenzi wa Stendi ya Mabasi Nangurukuru.

Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Kilwa Ndg. Renatus Mchau alipokuwa akijibu swali la papo kwa papo la Diwani wa Viti Maalum Mhe. Amina Kaudunde katika kikao cha Baraza la Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa kilichofanyika katika ukumbi wa jumba la maendeleo Mjini Kilwa Masoko Septemba 22 lililohoji ni kwani nini ujenzi wa Stendi ya Nangurukuru unachelewa licha ya fidia kutolewa kwa waliokuwa wanamiliki eneo hilo.

Akijibu swali hilo Mchau alisema kuwa Mchoro na mchakato wa kumpata Mkandarasi ili kumsainisha mkataba ndio sababu kubwa iliyopelekea kuchelewa kwa zoezi la ujenzi wa stendi hiyo.

Mchau alisema Halmashauri imejipanga kuhakikisha Mradi wa ujenzi wa Stendi hiyo unakamilika haraka iwezekananavyo ili usaidie  kuiongezea Mapato Halmashauri ya wilaya ya Kilwa.

“Mheshimiwa Mwenyekiti napenda Kujibu swali la lililoulizwa na Mhe. Kudunde kuhusu kuchelewa  kwa ujenzi wa  Stendi ya Nangurukuru, Mhe Mwenyekiti Ujenzi wa Stendi umechelewa kidogo kuanza kwa sababu tulikua tuna hangaikia suala la mchoro na kumpata mkandarasi na kumsainisha mkataba ili anze shughuli ya ujenzi  na mchakato umeenda vizuri kwahiyo tunatarajia kuanza kutekeleza Mradi huo muda wowote baada ya vitu vingine kukamlika” Alisema Mchau.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashuri ya Wilaya ya kilwa Mhe. Abuu Mussa Mjaka amemtaka Mkurugenzi wa Halmasahuri ya Wilaya ya Kilwa kufuatilia na kutoa mrejesho katika Baraza la Madiwani juu ya umiliki  wa Ukumbi wa Jumba la maendeleo pamoja na Uwanja wa Mpira wa miguu wa Mwenge (Taifa) uliopo Mjini Kilwa Masoko.

Mjaka amesema siku za karibuni kumekuwa na sinto fahamu kwa Wananchi na viongozi juu ya umiliki wa Ukumbi wa Jumba la maendeleo pamoja na Uwanja wa Mpira wa miguu wa Mwenge (Taifa) baada ya Chama cha Mapinduzi kudai kua ndiye Mmiliki wa jengo hilo pamoja na uwanja.

“Kumekuwa na maswali mengi juu ya hili jambo, nakuagiza Mkurugenzi Fuatilia jambo hili kwa umakini na tupatiwe rejesho wa  nani mmiliki wa hivi vitu”

Aidha ametaka mkurugenzi kuendelea na utaratibu uliopangwa juu ya fedha zilizotelewa kiasi cha shillingi milioni Kumi kwa ajili ya ukarabati wa uwanja wa Mwenge (Taifa).

“Zile pesa ambazo tumezitenga kwa ajili ya uwanja wetu zitumike kama ilivyoelekezwa na hata kama itakuja kubainika kuwa ni kweli uwanja ni wa Chama cha mapinduzi ujenzi uendelee kwani sisi tunafanya kwa ajili ya Wananchi wa Kilwa” alihitimisha Mjaka.

Sanjari na ajenda mbalimbali kulifanyika uchaguzi wa Makamu mwenyekiti wa Halmashauri pamoja na wenyeviti wa kamati mbalimbali ambapo Mhe. Ibrahimu Msati Diwani wa kata ya Miteja (Cuf) aliibuka kidedea katika nafasi ya Makamu Mwenyekiti akimbwaga Mhe Ibrahimu Likao Diwani wa Kata ya Mingumbi (Ccm). Mhe Msati alipata  kura 22 kati ya 32 huku Mhe. Likao akipata kura 10.  


Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU UTOAJI WA MIKOPO KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 04, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 11, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI. April 25, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • BANDARI YA UVUVI KILWA KUKAMILIKA MWEZI JUNI 2025

    May 08, 2025
  • KAMATI YA SIASA YA CCM MKOA WA LINDI YAIPONGEZA KILWA KWA UTEKELEZAJI WA ILANI

    May 07, 2025
  • KILWA YAPIGA HATUA KATIKA KUTOKOMEZA UKATILI WA KIJINSIA DHIDI YA WANAWAKE NA WATOTO

    May 06, 2025
  • WANANCHI, WANAFUNZI NA WATUMISHI KILWA WAJITOKEZA KWA MAZOEZI YA PAMOJA UWANJA WA MWENGE/TAIFA

    May 03, 2025
  • Tazama Zote

Video

Mkuu wa Wilaya ya Kilwa Akipokea Mwenge wa Uhuru.
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • TARURA GPN
  • Watumishi Portal
  • MIKOPO 10%
  • Mikopo ya Wanawake na Vijana
  • Huduma za Elimu

Tovuti Muhimu

  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ikulu
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu
  • Lindi

Idadi ya Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani Zetu

    Kilwa Masoko

    Anuani ya Posta: 160

    Simu: 0672365354

    Simu: 0672581557

    Barua pepe: ded@kilwadc.go.tz /ictsupport@kilwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Kanuni Binafsi
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa