Kufuatia Mashindano ya Umoja wa Michezo Shule za Sekondari (UMISSETA) yakimkoa yatakayofanyika Tarehe 30/05/2025. Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa Ndg. Hemed S. Magaro ameahidi zawadi ya fedha Milioni 2 kwa Mshindi katika ngazi ya mkoa, huku akiitaka Timu ya Michezo UMISSETA ya Wilaya kuzingatia nidhamu na kujituma katika Mashindano yaliyo mbele yao, ili kupata ushindi mkubwa na kuiletea heshima Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa.
Ndg, Magaro ameyazungumza hayo tarehe 29 Mei 2025 katika Hafla ndogo ya kuipa Baraka na kuiaga timu hiyo iliyofanyika shule ya Kilwa Sekondari ambapo timu hiyo iliweka kambi ya siku tano (5) ili kujiandaa na mashindano ya Kimkoa.
Naye Afisa Elimu Sekondari Ndg.Kassim Mpanda amesema kuwa timu hiyo ipo tayari kwa maandalizi ya kuelekea Mashindao hayo ya Kimkoa, hivyo inatarajia kuanza safari yake tarehe 29 Mei 2025 kuelekea manispaa ya Lindi kwaajili ya mashindano.
Wakiwawakilisha wanamichezo wenzao Sofia Peter na Selemani Mwanya wameushukuru Uongozi wote kuanzia shule hadi Halmashauri kwa kuwasimamia katika michezo yote kuanzia ngazi ya wilaya hadi kuelekea mashindano ngazi ya mkoa, huku wakiahidi kuhakikisha wanarudisha ushindi mkubwa kwa kuzingatia nidhamu na kujituma kama walivyoelekezwa na viongozi wao.
Kilwa Masoko
Anuani ya Posta: 160
Simu: 0672365354
Simu: 0672581557
Barua pepe: ded@kilwadc.go.tz /ictsupport@kilwadc.go.tz
Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa