• Malalamiko |
    • Anuani Zetu |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Kilwa District Council
Kilwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Mikakati ya Halmashauri
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Utumishi na Utawala
      • Elimu ya Msingi
      • Mipango na Takwimu
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Maliasili
    • Vitengo
      • Usafi na Mazingira
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ugavi
      • TEHAMA
      • Nyuki
      • Biashara
      • TASAF
      • Lishe
      • Uvuvi
    • Miji Midogo
      • Masoko
      • Kivinje
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Huduma za Uwekezaji
    • Biashara na Viwanda
    • Madini
    • Uvuvi
    • Utalii
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Mikopo kina Mama na Vijana
    • Huduma za Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Itakayo tekelezwa
  • Machapisho
    • Muongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Mifumo
    • PlanRep
    • FFARS
    • Prem
    • Salary Slip Portal

Dc Ngubiagai awapa siku 14 viongozi wa kijiji cha Nakiu, Awaasa Wananchi kujiunga na Mifuko ya afya

Posted on: August 29th, 2018

Mkuu wa Wilaya ya Kilwa Mkoa wa Lindi, Mhe. Christopher Ngubiagai amewaasa Wananchi Wilayani humo kujiunga na Mifuko ya afya ili wajiandae kutibiwa kirahisi pindi wakipata magonjwa.

Ngubiagai alitoa wito huo jana alipokuwa anazungumza na wananchi wa kijiji cha Nakiu kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji hicho kikichopo katika kata na tarafa ya Nanjirinji.

Mkuu huyo wa Wilaya alisema inashangaza kuona watu wengi wakitumia nguvu kubwa kufanya maandalizi ya sherehe.Ikiwamo harusi.Huku wengine wakiwa mahodari kuchangia rambirambi badala ya matibabu ya wagonjwa.

Alionya kuwa tabia hiyo haifai kufanywa na watu wanaojitambua.Badala yake wajenge utamaduni wa kujali afya zao kwa kuchukua tahadhari mapema.Ikiwamo kujiunga na mifuko ya afya ambayo itawafanya watibiwe wakati wote.Hivyo kuondoa usumbufu wa vikao vya kuchangishana fedha kwa ajili ya matibabu pindi wanaumwa.

Alisema hauzuii watu kufanya maandalizi ya sherehe wala kutoa fedha kwa ajili ya mazishi na rambirambi.Bali waanze kujali afya zao ili wawaondolee mzigo jamaa zao pindi wanapoumwa au wasitumie fedha nyingi kwa ajili ya matibabu wakati serikali imewarahishia upatikanaji huduma za matibabu kwa gharama nafuu.

Alisema katika kuthibitisha serikali imeamua kuboresha huduma za afya kwa ajili ya wananchi wake.Ikiwemo kuongeza dawa na vifaa tiba kwenye zahanati,vituo vya afya na hospitali.Huku bajeti ya wizara yenye dhamana ya afya inapanda kila mwaka.

"Wilaya ya Kilwa imepokea shilingi 1.5 bilioni kwa ajili ya ukarabati wa vituo vya afya.Pia inatarajia kupokea shilingi 500 milioni kwa kazi hiyo.Tayari tumeletewa watumishi 104 wa sekta ya afya.Hivi unawezaje kushindwa kujiunga na mifuko hiyo kwa gharama nafuu wakati huo unatumia fedha nyingi kuandaa harusi huku ukijua bibi harusi na bwana harusi wataumwa na kuhitaji tiba,"alisisitiza nakuhoji Ngubiagai.

Katika kuhakikisha wanaojiunga na mifuko hiyo(CHF na NHIF) wanafaidika.Ngubiagai amewaagiza watumishi wa idara ya afya kuwapa kipaumbele wagonjwa waliojiunga na mifuko hiyo.Badala ya wanaokwenda na fedha taslimu.Huku akitoa wito kwa wananchi kumpa taarifa za mwenendo wa upatikanaji huduma kwenye vituo vya afya,zahanati na hosipitali.

Kwa upande wake mratibu wa CHF wilaya ya Kilwa,Fred Mpondachuma aliwaondoa hofu wananchi kuhusu uhakika na ubora wa matibabu kwenye zahanati,vituo vya afya na hosipitali kwa watu waliojiunga na mifuko ya afya.Kwani zimeboreshwa na dawa zinapatikana kwa wingi.

Alisema uboreshwaji wa huduma za afya nchini umeondoa dhana yamuda mrefu ya kuamini hospitali za nje ya nchi.Kwasababu hata viongozi wa kitaifa na familia zao wameanza kutibiwa hapa nchini.Kwasababu hata baadhi ya magonjwa ambayo yalikuwa tiba zake zilikuwa zinapatikana nje ya nchi yameanza kutibiwa nchini.

Katika hatua nyingine Ngubiagai amewapa siku 14 viongozi wa serikali ya kijiji hicho wawewamempatia idadi ya wafugaji na mifugo iliyopo katika kijiji hicho ili amalize mgogoro baina ya wakulima na wafugaji katika kijijji hicho.Huku akiweka wazi kwamba baadhi ya watendaji na viongozi wa serikali wilayani humo wanachangia migogoro kwasababu ya kupindisha sheria kwasababu ya tamaa.


NEWS CREDIT : MUUNGWANA BLOG

Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU UTOAJI WA MIKOPO KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 04, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 11, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI. April 25, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MAKALA APONGEZA JITIHADA ZA KURUDISHA MAWASILIANO SOMANGA

    April 10, 2025
  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa Mkono wa Eid kwa watoto wenye mahitaji Maalum Shule ya Msingi Mtanga Wilayani Kilwa.

    March 31, 2025
  • IDARA YA MAENDELEO YA JAMII YATOA MSAADA WA TELEVISHENI KWA GEREZA LA KILWA MASOKO

    April 28, 2025
  • MARAFIKI WA ELIMU WAWASILISHA TAARIFA YA UFUATILIAJI WA MAKUZI YA AWALI YA MTOTO KWA WADAU WA ELIMU KILWA.

    April 28, 2025
  • Tazama Zote

Video

Mkuu wa Wilaya ya Kilwa Akipokea Mwenge wa Uhuru.
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • TARURA GPN
  • Watumishi Portal
  • MIKOPO 10%
  • Mikopo ya Wanawake na Vijana
  • Huduma za Elimu

Tovuti Muhimu

  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ikulu
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu
  • Lindi

Idadi ya Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani Zetu

    Kilwa Masoko

    Anuani ya Posta: 160

    Simu: 0672365354

    Simu: 0672581557

    Barua pepe: ded@kilwadc.go.tz /ictsupport@kilwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Kanuni Binafsi
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa