• Malalamiko |
    • Anuani Zetu |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Kilwa District Council
Kilwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Mikakati ya Halmashauri
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Utumishi na Utawala
      • Elimu ya Msingi
      • Mipango na Takwimu
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Maliasili
    • Vitengo
      • Usafi na Mazingira
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ugavi
      • TEHAMA
      • Nyuki
      • Biashara
      • TASAF
      • Lishe
      • Uvuvi
    • Miji Midogo
      • Masoko
      • Kivinje
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Huduma za Uwekezaji
    • Biashara na Viwanda
    • Madini
    • Uvuvi
    • Utalii
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Mikopo kina Mama na Vijana
    • Huduma za Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Itakayo tekelezwa
  • Machapisho
    • Muongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Mifumo
    • PlanRep
    • FFARS
    • Prem
    • Salary Slip Portal

Dc Ngubiagai agawa Bidhaa zenye Thamani ya Milioni Arobaini na Tano kwa Jamii

Posted on: August 10th, 2018

Kilwa,

Mkuu wa wilaya ya kilwa Mheshimiwa Christopher Ngubiagai amegawa bidhaa zenye thamani ya zaidi ya Milioni Arobaini na Tano kwa Shule za Sekondari, Msingi, Taasisi za kiserikali, Vituo vya kulelea watoto Yatima na wenye Mahitaji maalumu.

Bidhaa hizo ni viroba Mia mbili na kumi na Sita vya sukari pamoja  na Madumu Mia Tatu Arobaini na Nane ya Mafuta ya kupikia ambazo ni miongoni mwa Viroba Mia Nne na Hamsini  na Dumu Elfu moja Mia Tatu arobaini na tisa yaliyokamatwa kwa kosa la kuingizwa Wilayani Kilwa kinyume na utaratibu kati ya mwezi  Februari na Juni.

Akizungumza wakati wa ugawaji wa Bidhaa hizo Mheshimiwa Ngubiagai amesema Serikali ya awamu ya Tano ina nia njema ya kuwasaidia Wafanyabiashara ili waweze kunufaika na wanachokifanya na kuwataka kuheshimu na kufuata utaratibu ambao umewekwa na Serikali.

Ngubiagai amesema Kamati ya ulinzi na Serikali kwa ujumla ipo Macho kuhakikisha inawakamata na kuwachukuliwa hatua za kisheria. wale wote ambao wanaingiza Bidhaa kinyemela kupitia bandari Bubu.

“Wafanyabiashara tushirikiane kulipa kodi na tozo mbalimbali ambazo zipo kisheria ili tuweze kupata mapato ambayo yatasaidia kuimarisha huduma mbalimbali za kijamii na kukuza viwanda vyetu

Serikali ipo Macho saa Ishirini na Nne kuhakikisha inawakamata wale wote ambao wanakwepa kulipa Kodi na Tozo mbalimbali na kuingiza Bidhaa kinyemela kupitia bandari Bubu, wanakamatwa na kuchukuliwa hatua za kisheria” alisema Ngubiagai

Mkuu wa Wilaya ya Kilwa Mhe. Christopher Ngubiagai  akizungumza na waandishi wa Habari mara baada ya  kukabidhi Bidhaa mbalimbali kwa Shule, taasisi za serikali na wenye mahitaji maalumu (Picha: Ally Ruambo).

Pia ameitaka jamii kushirikiana na serikali kwa kuwafichua Wafanyabiashara ambao wanaingiza Bidhaa zao kupitia bandari zisizo rasmi na kukwepa kulipa kodi.

Aidha amewata Walimu na Wasimamizi wa Makambi ya Wanafunzi wanaojiandaa na Mitihani yao mwisho kutumia Sukari na Mafuta waliyopatiwa kwa uangalifu na kwa manufaa ya wanafunzi.

“Hivi vitu tulivyotoa sio kwa niaba yenu walimu ni kwa ajili ya Wanafunzi, ni marufuku kuuza au kwenda kutumia nyumbani kwako, Tumetoa kwa ajili ya vijana wetu ambao wako Mashuleni na wale ambao wapo Makambini wakijiandaa na Mitihani ya mwisho

Wapelekeeni wakale washibe ili wapate nguvu ya Kusoma na hatimaye waweze kufanya vizuri katika Mitihani yao na Malengo yetu ya kupandisha Elimu Wilaya ya Kilwa yatimie, na Kikosi kazi kitakuja kutembela na kukagua kila Shule na Kambi kuona Maendeleo na Changamoto ambazo zipo huko” alihitimisha Ngubiagai.

Walimu na Viongozi kutoka Taasisi mbalimbali wakibeba Viroba vya Sukari baada ya kukabidhiwa na Mkuu wa Wilaya ya Kilwa Mheshimiwa Christopher Ngubiagai (Picha: Ally Ruambo)

Jumla ya Madumu Elfu Moja na Moja na viroba Mia mbili na Thelathini na Nne vilivyobaki katika mgawo huwo vinatarajiwa kugawanywa katika Wilaya Nne ambazo zinaunda Mkoa wa Lindi.


Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU UTOAJI WA MIKOPO KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 04, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 11, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI. April 25, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MAKALA APONGEZA JITIHADA ZA KURUDISHA MAWASILIANO SOMANGA

    April 10, 2025
  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa Mkono wa Eid kwa watoto wenye mahitaji Maalum Shule ya Msingi Mtanga Wilayani Kilwa.

    March 31, 2025
  • IDARA YA MAENDELEO YA JAMII YATOA MSAADA WA TELEVISHENI KWA GEREZA LA KILWA MASOKO

    April 28, 2025
  • MARAFIKI WA ELIMU WAWASILISHA TAARIFA YA UFUATILIAJI WA MAKUZI YA AWALI YA MTOTO KWA WADAU WA ELIMU KILWA.

    April 28, 2025
  • Tazama Zote

Video

Mkuu wa Wilaya ya Kilwa Akipokea Mwenge wa Uhuru.
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • TARURA GPN
  • Watumishi Portal
  • MIKOPO 10%
  • Mikopo ya Wanawake na Vijana
  • Huduma za Elimu

Tovuti Muhimu

  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ikulu
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu
  • Lindi

Idadi ya Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani Zetu

    Kilwa Masoko

    Anuani ya Posta: 160

    Simu: 0672365354

    Simu: 0672581557

    Barua pepe: ded@kilwadc.go.tz /ictsupport@kilwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Kanuni Binafsi
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa