• Malalamiko |
    • Anuani Zetu |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Kilwa District Council
Kilwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Mikakati ya Halmashauri
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Utumishi na Utawala
      • Elimu ya Msingi
      • Mipango na Takwimu
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Maliasili
    • Vitengo
      • Usafi na Mazingira
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ugavi
      • TEHAMA
      • Nyuki
      • Biashara
      • TASAF
      • Lishe
      • Uvuvi
    • Miji Midogo
      • Masoko
      • Kivinje
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Huduma za Uwekezaji
    • Biashara na Viwanda
    • Madini
    • Uvuvi
    • Utalii
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Mikopo kina Mama na Vijana
    • Huduma za Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Itakayo tekelezwa
  • Machapisho
    • Muongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Mifumo
    • PlanRep
    • FFARS
    • Prem
    • Salary Slip Portal

Dc Kilwa avionya vijiji umilikishaji ardhi kwa wawekezaji

Posted on: October 1st, 2018

Mkuu wa Wilaya ya Kilwa Mkoani Lindi,Christopher Ngubiagai amewaonya viongozi na watendaji wa vijiji wilayani humu kuwa makini na mikataba ya ardhi wanayofanya na wawekezaji.

Ngubiagai alitoa wito jana alipozungumza na wananchi wa kijiji cha Mtukwao,kupitia mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji hicho kilichopo katika kata na tarafa ya Miteja.

Alisema serikali imevipa vijiji mamlaka kamili kuhusu ardhi kupitia sheria namba 5 ya ardhi ya mwaka 1999.Hata hivyo wananchi wasitumie uwezo huo vibaya na kusababishia vijiji kushindwa kunufaika na raslimali na maliasili hiyo iliyopo kwenye vijiji.Hali ambayo inasababishwa na viongozi wachache wanaoshirikiana na wawekezaji kuwadhulumu wananchi.

Alisema ni jambo la kusikitisha kuona vijiji na hata wilaya hiyo ikiwa taabani kiuchumi wakati vinazungukwa na maliasili nyingi.Huku mikataba inayofanywa na baadhi ya wawekezaji ikiwa haina tija kwa halmashauri wala wilaya hii.

Mkuu wa Wilaya ya Kilwa Mhe. Christopher Ngubiagai akizungumza na wananchi wa kijiji cha Mtukwao katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji hicho kilichopo katika kata na tarafa ya Miteja.

Alisema baadhi ya viongozi na watendaji wameingia mikataba na wawekezaji wababaishaji wasio na uwezo ambao wameshindwa kuendeleza maeneo waliyopewa.Huku vijiji vikiwa havipati chochote.

Aliwataka viongozi wa vijiji ambavyo wawekezaji wameshindwa kuendeleza maeneo waliyowapa,wahakikishe wanawaita na kuwapa muda wa kuyaendeleza.Iwapo watashindwa kuendeleza wanyang'anywe ili wapewe wawekezaji wenye uwezo.

"Nijambo la aibu kuona vijiji vimezungukwa na maliasili nyingi,lakini havina hata ofisi.Ukiangalia mikataba iliyofanyika haina tija," alisema Ngubiagai.

Aliwataka viongozi kuwa makini na mikataba ili wawapunguzie mzigo wa shida wananchi wao ambao wanahitaji maendeleo na kufaidika na maliasili zinazowazunguka.Ambazo ni tunu kutoka kwa Mungu.

Wananchi wa kijiji cha Mtukwao wakiwa katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji hicho kilichopo katika kata na tarafa ya Miteja.

Mbali na hayo Mkuu huyo wa Wilaya ya Kilwa aliwapongeza wananchi wa kijiji hicho kwa ushirikano wanaotoa kwa walimu na kamati ya shule.Ushirikaiano uliosababisha kuwa na kiwango cha 80% ya ufaulu.

Ngubiagai pia aliwapongeza wazazi na walezi wawanafunzi wanaosoma kwenye shule ya kijiji hicho kwa kuthibiti tatizo la mimba kwa wanafunzi wanaosoma kwenye shule hiyo.Huku akiweka wazi katika ziara atazofanya katika maeneo mengine atawahamasisha viongozi na wananchi wake kuiga yanayofanywa na wananchi na viongozi wa kijiji hicho.

Ngubiagai kwenye mkutano huo alihaidi kuchangia mifuko 20 ya saruji.Ikiwa ni mchango wake kwenye ujenzi wa ofisi ya serikali ya kijiji hicho cha Mtukwao.

Credit : Ahmad Mmow,Kilwa.

Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU UTOAJI WA MIKOPO KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 04, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 11, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI. April 25, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MAKALA APONGEZA JITIHADA ZA KURUDISHA MAWASILIANO SOMANGA

    April 10, 2025
  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa Mkono wa Eid kwa watoto wenye mahitaji Maalum Shule ya Msingi Mtanga Wilayani Kilwa.

    March 31, 2025
  • IDARA YA MAENDELEO YA JAMII YATOA MSAADA WA TELEVISHENI KWA GEREZA LA KILWA MASOKO

    April 28, 2025
  • MARAFIKI WA ELIMU WAWASILISHA TAARIFA YA UFUATILIAJI WA MAKUZI YA AWALI YA MTOTO KWA WADAU WA ELIMU KILWA.

    April 28, 2025
  • Tazama Zote

Video

Mkuu wa Wilaya ya Kilwa Akipokea Mwenge wa Uhuru.
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • TARURA GPN
  • Watumishi Portal
  • MIKOPO 10%
  • Mikopo ya Wanawake na Vijana
  • Huduma za Elimu

Tovuti Muhimu

  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ikulu
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu
  • Lindi

Idadi ya Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani Zetu

    Kilwa Masoko

    Anuani ya Posta: 160

    Simu: 0672365354

    Simu: 0672581557

    Barua pepe: ded@kilwadc.go.tz /ictsupport@kilwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Kanuni Binafsi
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa