• Malalamiko |
    • Anuani Zetu |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Kilwa District Council
Kilwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Mikakati ya Halmashauri
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Utumishi na Utawala
      • Elimu ya Msingi
      • Mipango na Takwimu
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Maliasili
    • Vitengo
      • Usafi na Mazingira
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ugavi
      • TEHAMA
      • Nyuki
      • Biashara
      • TASAF
      • Lishe
      • Uvuvi
    • Miji Midogo
      • Masoko
      • Kivinje
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Huduma za Uwekezaji
    • Biashara na Viwanda
    • Madini
    • Uvuvi
    • Utalii
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Mikopo kina Mama na Vijana
    • Huduma za Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Itakayo tekelezwa
  • Machapisho
    • Muongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Mifumo
    • PlanRep
    • FFARS
    • Prem
    • Salary Slip Portal

Mfuko wa Afya ya jamii (CHF) wafanyiwa maboresho

Posted on: May 7th, 2018

  Kilwa,

        Mfuko wa Afya ya jamii umeboresha huduma zake ikiwemo kuondoa ukomo wa kutoa huduma ya matibabu kwa mwanachama kutoka ngazi ya Halmashauri mpaka ngazi ya mkoa.

Hayo yamebainishwa jana na Kaimu Mkurugenzi wa Mfuko wa Afya ya jamii kutoka mfuko wa taifa wa bima ya afya makao makuu Ndg. Slivery Mgonza katika ufunguzi wa  mafunzo ya siku tatu kwa vituo vya kutolea huduma ya Afya yaliyafanyika katika ukumbi wa chuo cha maendeleo Mjini Kilwa Masoko.

Mgonza amesema kabla ya maboresho mfuko ulikua na changamoto mbalimbali ikiwemo ukomo wa wanachama kupata matibabu katika vituo vya kutolea huduma ambayo kwa sasa imeondolewa kwa kufanyiwa maboresho.

“Kabla ya maboresho mwanachama alikua anatibiwa pale alipochangia na kwenye baadhi ya halmashauri alikua anaweza kwenda hadi hospitali ya wilaya lakini alikua hawezi kutoka nje ya Halmashauri, lakini pia hata huduma alizokua anapta zilikua zimefinywa kwa sababu alikua haewezi kulazwa au kufanyiwa upasuaji lakini kwa sasa tumefanya maboresho mwanachama atafaidika na mafao mengine zaidi na ataweza kutibiwa mpaka Hospitali ya rufaa ya mkoa”. Alisema Mgonza

Kaimu Mkurugenzi wa Mfuko wa Afya ya jamii kutoka mfuko wa taifa wa bima ya afya makao makuu Ndg. Slivery Mgonza akizungumza na washiriki (awapo katika picha) katika ufunguzi wa  mafunzo ya siku tatu kwa vituo vya kutolea huduma ya Afya yaliyafanyika katika ukumbi wa chuo cha maendeleo Mjini Kilwa Masoko. ( Picha na Ally Ruambo)

Amesema sanjari na mfuko wa Afya ya jamii kufanya maboresho katika kutoa huduma pia umefanya maboresho katika Nyanja ya usimamizi ambapo usimamizi umetolewa kutoka ngazi ya wilaya mpaka mkoani na Katibu tawala wa mkoa husika ndio atakua msimamizi wa utoaji huduma.

Kwa upande wake Meneja wa Mfuko wa Afya ya jamii wilaya ya Kilwa Bw. Fred Mpondachuma amewataka wananchi ambao hawajajiunga na mfuko wa afya ya jamii wajiunge sasa ili waweze kunufaika na huduma na  kwa wale ambao ni wanachama wa mfuko wa afya ya jamii kuendelea kufurahia huduma za mfuko wa afya ya jamii na kujisajiri tena upya kwa gharama ya shilingi 30000 baada ya mkataba wao wa sasa kufikia mwisho.

Mmoja wa wakufunzi katika mafunzo kwa vituo vya kutolea huduma ya Afya Bi. Zabibu Uledi akielekeza jambo kwa washiriki wa mafunzo ya siku tatu kwa vituo vya kutolea huduma ya Afya yaliyafanyika katika ukumbi wa chuo cha maendeleo Mjini Kilwa Masoko. ( Picha na Ally Ruambo)

Awali akifungua mafunzo hayo Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya kilwa Bw. Zablon Bugingo amewataka wajumbe wa kamati na watendaji kushirikiana kwa pamoja katika kutekeleza majukumu yao ili kuleta  matokeo chanya ambayo yatasaidia kusukuma gurudumu la maendeleo.

Aidha amewataka watumishi kuandaa kwa usahihi  ripoti za kila mwezi na kuziwasilisha sehemu husika katika muda sahihi ili ziweze kufanyiwa kazi katika muda sahihi.

Mafunzo kwa vituo vya kutolea huduma ya Afya yamejumuisha watu mbalimbali ikiwemo  wauguzi, waganga wafawidhi kutoka Hospitali na vituo vya afya mbalimbali, mwenyeviti na wajumbe wa kamati za afya za vijiji, afisa mifumo na wengineo.

Baadhi ya washiriki wa mafunzo ya siku tatu kwa vituo vya kutolea huduma ya Afya yaliyafanyika katika ukumbi wa chuo cha maendeleo Mjini Kilwa Masoko. ( Picha na Ally Ruambo)

Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU UTOAJI WA MIKOPO KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 04, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 11, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI. April 25, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • BANDARI YA UVUVI KILWA KUKAMILIKA MWEZI JUNI 2025

    May 08, 2025
  • KAMATI YA SIASA YA CCM MKOA WA LINDI YAIPONGEZA KILWA KWA UTEKELEZAJI WA ILANI

    May 07, 2025
  • KILWA YAPIGA HATUA KATIKA KUTOKOMEZA UKATILI WA KIJINSIA DHIDI YA WANAWAKE NA WATOTO

    May 06, 2025
  • WANANCHI, WANAFUNZI NA WATUMISHI KILWA WAJITOKEZA KWA MAZOEZI YA PAMOJA UWANJA WA MWENGE/TAIFA

    May 03, 2025
  • Tazama Zote

Video

Mkuu wa Wilaya ya Kilwa Akipokea Mwenge wa Uhuru.
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • TARURA GPN
  • Watumishi Portal
  • MIKOPO 10%
  • Mikopo ya Wanawake na Vijana
  • Huduma za Elimu

Tovuti Muhimu

  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ikulu
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu
  • Lindi

Idadi ya Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani Zetu

    Kilwa Masoko

    Anuani ya Posta: 160

    Simu: 0672365354

    Simu: 0672581557

    Barua pepe: ded@kilwadc.go.tz /ictsupport@kilwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Kanuni Binafsi
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa