• Malalamiko |
    • Anuani Zetu |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Kilwa District Council
Kilwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Mikakati ya Halmashauri
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Utumishi na Utawala
      • Elimu ya Msingi
      • Mipango na Takwimu
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Maliasili
    • Vitengo
      • Usafi na Mazingira
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ugavi
      • TEHAMA
      • Nyuki
      • Biashara
      • TASAF
      • Lishe
      • Uvuvi
    • Miji Midogo
      • Masoko
      • Kivinje
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Huduma za Uwekezaji
    • Biashara na Viwanda
    • Madini
    • Uvuvi
    • Utalii
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Mikopo kina Mama na Vijana
    • Huduma za Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Itakayo tekelezwa
  • Machapisho
    • Muongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Mifumo
    • PlanRep
    • FFARS
    • Prem
    • Salary Slip Portal

Bodi ya michezo ya kubahatisha yateketeza mashine 63 wilayani kilwa

Posted on: September 20th, 2018

Kilwa,

             Kamati ya ulinzi na usalama Wilayani Kilwa kwa Kushirikiana na Bodi ya Michezo ya Kubahatisha imekamata na kuteketeza Mashine 63 ambazo zilikua zimewekwa  sehemu zisizo rasmi na kuendeshwa kinyume na sheria.

Akizungumza kabla ya kuteketeza Mashine hizo Afisa Mkaguzi wa Michezo ya Kubahatisha kutoka Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Ndg. Jehud Ngolo amesema Uongozi wa Wilaya ya Kilwa uliwasilisha barua kwa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha juu ya Kukithiri kwa michezo ya kubahatisha Wilayani Kilwa isiyozingatia taratibu na Sheria.  

“Sheria zilizokiukwa ni pamoja na Kutokuwa na Leseni za maeneo Husika kutoka Bodi ya Michezo ya Kubahatisha (Site Licences) na baadhi ya Mashine Kukosa Stika yaani Mashine Bandia” alisema Ngolo

Ngolo amesema Kifungu 82 cha Gaming Act, 2003 kama ilivyorekebishwa na Kifungu 82A cha Finance Act, 2015 kinaipa Mamlaka Bodi ya Michezo ya Kubahatisha (Gaming Board of Tanzania) kukamata na kuteketeza Mashine husika.

Amesema Kifungu 77 cha Sheria ya Michezo ya kubahatisha inawataka Waendeshaji wa michezo ya kubahatisha kuhakikisha Vifaaa (Mashine za Bahati nasibu) vimeidhinishwa na kusajiliwa kwani kinyume na hapo yanaweza kutokea Madhara ikiwemo Watoto kushiriki kwa kua hakuna uangalizi unaotambulika kisheria, Mashine zinazotumika zinaweza kuwa chini ya kiwango pamoja na kukosekana kwa usalama wa Wachezaji.

Jumla ya Mashime 63 zikiteketea kwa Moto baada  ya kukamatwa na Bodi ya Michezo ya kubahatisha kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi Wilayani Kilwa (Picha: Ally Ruambo)

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kilwa ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na usalama amempongeza Mkurugenzi wa Bodi ya Michezo ya kubahatisha kwa hatua alizochukua baada ya kupokea barua ya malalamiko juu ya utitiri wa Mashine za kubahatisha zilikuwa zikiendeshwa kinyume na sheria.

 Pia Ngubiagai amewataka vijana Wilayani Kilwa na Taifa kwa ujumla kujishughulisha na shughuli za kimaendeleo na kuacha mawazo ya kutegemea michezo ya bahati nasibu pekee katika kubadilisha maisha yao.

“Ingawa hii Michezo inajulikana Kisheria lakini ni vyema wakatumia muda wao mwingi katika shuguli za kimaendeleo, wafanye kazi halali kama ni kilimo, biashara, ujasiriamali nakadhalika ili kusudi waweze kupata mapato ambayo yatawasaidia katika kujenga masha yao na uchumi wa Taifa kwa ujumla”

Aidha Ngubiagai ameahidi kuendelea kutoa ushirikiano kwa Bodi ya Michezo ya kubahatisha na kumpongeza Mkuu wa Polisi Wilaya ya Kilwa na timu yake kwa ushirikiano walioutoa kwa Bodi ya Michezo ya kubahatisha kuanzia mwanzo mpaka mwisho wa zoezi na kuagiza zoezi hilo liwe endelevu.

Mkuu wa Wilaya ya Kilwa (Katikati) akizungumza na Waandishi wa Habari kabla ya zoezi la kuteketeza Mashine zilizokamtwa na Bodi ya Michezo ya kubahatisha kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi Wilayani Kilwa, wa kwanza kushoto Ndg. Bakari Maggid , kulia Ndg. Jehud Ngolo Maafisa ukaguzi wa michezo ya kubahatisha (Picha : Ally Ruambo)

Jumla ya mashine 63 zikiwemo 45 za kampuni ya Bonanza, 15 JX Betting na 3 Mashine Bandia zimekamatwa wilayani Kilwa zikiwa zimewekwa  maeneo yasiyo ruhusiwa kisheria, kwa mujibu wa Sheria Mashine hizo zinaruhusiwa sehemu za kuuzia vileo kama vile Baa,Pabu na kwenye grosari.

Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU UTOAJI WA MIKOPO KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 04, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 11, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI. April 25, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • BANDARI YA UVUVI KILWA KUKAMILIKA MWEZI JUNI 2025

    May 08, 2025
  • KAMATI YA SIASA YA CCM MKOA WA LINDI YAIPONGEZA KILWA KWA UTEKELEZAJI WA ILANI

    May 07, 2025
  • KILWA YAPIGA HATUA KATIKA KUTOKOMEZA UKATILI WA KIJINSIA DHIDI YA WANAWAKE NA WATOTO

    May 06, 2025
  • WANANCHI, WANAFUNZI NA WATUMISHI KILWA WAJITOKEZA KWA MAZOEZI YA PAMOJA UWANJA WA MWENGE/TAIFA

    May 03, 2025
  • Tazama Zote

Video

Mkuu wa Wilaya ya Kilwa Akipokea Mwenge wa Uhuru.
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • TARURA GPN
  • Watumishi Portal
  • MIKOPO 10%
  • Mikopo ya Wanawake na Vijana
  • Huduma za Elimu

Tovuti Muhimu

  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ikulu
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu
  • Lindi

Idadi ya Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani Zetu

    Kilwa Masoko

    Anuani ya Posta: 160

    Simu: 0672365354

    Simu: 0672581557

    Barua pepe: ded@kilwadc.go.tz /ictsupport@kilwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Kanuni Binafsi
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa