• Malalamiko |
    • Anuani Zetu |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Kilwa District Council
Kilwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Mikakati ya Halmashauri
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Utumishi na Utawala
      • Elimu ya Msingi
      • Mipango na Takwimu
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Maliasili
    • Vitengo
      • Usafi na Mazingira
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ugavi
      • TEHAMA
      • Nyuki
      • Biashara
      • TASAF
      • Lishe
      • Uvuvi
    • Miji Midogo
      • Masoko
      • Kivinje
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Huduma za Uwekezaji
    • Biashara na Viwanda
    • Madini
    • Uvuvi
    • Utalii
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Mikopo kina Mama na Vijana
    • Huduma za Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Itakayo tekelezwa
  • Machapisho
    • Muongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Mifumo
    • PlanRep
    • FFARS
    • Prem
    • Salary Slip Portal

BALOZI WA CHINA ATEMBELEA BANDARI YA UVUVI KILWA AAHIDI USHIRIKIANO ZAIDI

Posted on: June 24th, 2025

Balozi wa Jamhuri ya Watu wa China nchini Tanzania, Mhe. Chen Mingjian, amefanya ziara ya ukaguzi wa maendeleo ya ujenzi wa Bandari ya Uvuvi katika Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa, mkoani Lindi, ikiwa ni sehemu ya kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na China katika sekta ya uchumi wa buluu.

Ziara hiyo imefanyika tarehe 24 Juni 2025, ambapo Balozi Chen ameambatana na Mkuu wa Wilaya ya Kilwa, Mhe. Mohamed Nyundo na kukagua hatua mbalimbali za ujenzi wa bandari hiyo maalum kwa ajili ya shughuli za uvuvi. Bandari hiyo ni sehemu ya juhudi za Serikali ya Tanzania kuimarisha miundombinu ya sekta ya uvuvi, kuinua kipato cha wavuvi wa ukanda wa pwani, na kuongeza mchango wa sekta hiyo kwenye pato la Taifa.

Akizungumza mara baada ya ukaguzi huo, Balozi Chen ameeleza kuridhishwa na maendeleo ya mradi na kuahidi kuwa Serikali ya China itaendelea kushirikiana na Tanzania katika kukuza sekta ya uvuvi na maendeleo ya kiuchumi kwa ujumla.

"Mradi huu una umuhimu mkubwa kwa wananchi wa Kilwa na kwa uchumi wa Tanzania kwa ujumla, China itaendelea kushirikiana na Serikali ya Tanzania katika kuhakikisha kuwa miradi ya kimkakati kama hii inakamilika kwa wakati na kwa ubora unaotakiwa," amesema Balozi Chen.

Nae Mkuu wa Wilaya ya Kilwa, Mhe. Mohamed Nyundo, amemshukuru Balozi Chen kwa ujio wake na mchango wa Serikali ya China katika kusaidia miradi ya maendeleo nchini, pia amesisitiza kuwa bandari hiyo itakuwa chachu ya maendeleo kwa wananchi wa Kilwa kwa kutoa ajira, kuimarisha biashara ya samaki, na kuongeza mapato ya halmashauri.

"Tunashukuru ushirikiano wetu na Serikali ya China kupitia mradi huu wa bandari ya uvuvi. Utekelezaji wake utaleta mapinduzi makubwa katika maisha ya wananchi wetu, hasa wavuvi na wafanyabiashara wadogo," alisema Mhe. Nyundo.

Ziara hiyo pia imeambatana na mazungumzo ya kuimarisha ushirikiano kati ya pande hizo mbili, ambapo ni masuala ya uwekezaji katika sekta ndogo ndogo, na elimu ya bahari kwa jamii za pwani yalipewa kipaumbele.

Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU UTOAJI WA MIKOPO KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 04, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 11, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI. April 25, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • SERIKALI KUENDELEA KUWEKA MAZINGIRA WEZESHI KWA NGO's LINDI

    July 10, 2025
  • SERIKALI YAFANYA UKAGUZI WA MIRADI YA MASHIRIKA YASIYO YA KISERIKALI WILAYANI KILWA

    July 09, 2025
  • HALMASHAURI YA KILWA YADUMISHA USHIRIKIANO NA MASHIRIKA YASIYO YA KISERIKALI KUPITIA JUKWAA LA PAMOJA

    July 01, 2025
  • KILWA YAPOKEA RUZUKU YA CHANJO ZA MIFUGO KWA AJILI YA KUKABILI MAGONJWA HATARI

    June 26, 2025
  • Tazama Zote

Video

Mkuu wa Wilaya ya Kilwa Akipokea Mwenge wa Uhuru.
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • TARURA GPN
  • Watumishi Portal
  • MIKOPO 10%
  • Mikopo ya Wanawake na Vijana
  • Huduma za Elimu

Tovuti Muhimu

  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ikulu
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu
  • Lindi

Idadi ya Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani Zetu

    Kilwa Masoko

    Anuani ya Posta: 160

    Simu: 0672365354

    Simu: 0672581557

    Barua pepe: ded@kilwadc.go.tz /ictsupport@kilwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Kanuni Binafsi
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa