• Malalamiko |
    • Anuani Zetu |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Kilwa District Council
Kilwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Mikakati ya Halmashauri
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Utumishi na Utawala
      • Elimu ya Msingi
      • Mipango na Takwimu
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Maliasili
    • Vitengo
      • Usafi na Mazingira
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ugavi
      • TEHAMA
      • Nyuki
      • Biashara
      • TASAF
      • Lishe
      • Uvuvi
    • Miji Midogo
      • Masoko
      • Kivinje
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Huduma za Uwekezaji
    • Biashara na Viwanda
    • Madini
    • Uvuvi
    • Utalii
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Mikopo kina Mama na Vijana
    • Huduma za Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Itakayo tekelezwa
  • Machapisho
    • Muongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Mifumo
    • PlanRep
    • FFARS
    • Prem
    • Salary Slip Portal

Dc Awataka Madiwani Kusimamia Halmashauri

Posted on: June 4th, 2021


Mkuu wa Wilaya ya Kilwa Mhe.Christopher Ngubiagai amewataka waheshimiwa madiwani kuhakikisha wanaisimamia Halmashauri kwa ukaribu ili kupunguza malalamiko ya wananchi. ‘’Waheshimiwa madiwani, nyie ndiyo wasimamizi wakuu wa Halmashauri, hakikisheni mnasimamia ukusanyaji wa mapato na pia kuhakikisha kile kinachokusanywa kinafanya kazi kulingana na bajeti, msipofanya hivyo haya malalamiko ya wananchi kuhusu huduma mbali mbali yataendelea kuwepo siku hadi siku’’ alisisitiza Mhe.Ngubiagai.

Mhe.Mkuu wa Wilaya pia aliwataka Wahe.madiwani katika maeneo yao kuhakikisha wanadhibiti uingizaji holela wa mifugo katika kata zao kwani ni changamoto mpya katika Wilaya yetu ambapo kumekuwa na wimbi kubwa la mifugo inayoingizwa kutoka mikoa mbali mbali. ‘’Wilaya yetu ni kubwa , hivyo bila kupata taarifa sahihi na kwa wakati kutoka kwenu hatuwezi kujua ni kijiji gani kuna changamoto ya mifugo ili wenye mamlaka tuweze kuchukua hatua kwa wakati’’ aliongeza Mhe.Mkuu wa Wilaya.

Mkuu wa Wilaya alisistiza kuwa kimsingi hawazuii mifugo kuingia katika Wilaya ya Kilwa isipokuwa ni lazima tujua ni mfugaji gani yupo wapi na idadi ya mifugo pia ilingane na maeneo yaliyotengwa.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa Mhe.Farida Kikoleka aliwahimiza wataalam wa Idara mbali mbali ndani ya Halmashauri kuhakikisha kila mmoja anawajibika katika nafasi yake bila kujali changamoto zilizopo. ‘’Najua mna changamoto mbali mbali hasa idara za Afya na Elimu kutokana na upungufu wa watumishi, lakini bado mna wajibu wa kufanya kazi kwa bidii kwa sababu wananchi wana matumaini makubwa na nyie’’ alisisitiza Mhe.Kikoleka.

Naye Kaimu Mkurugenzi Bw.Godfrey Jaffari aliwahakikishia waheshimiwa madiwani kuwa timu yake itaendelea kufanya kazi kwa weledi na kufuata maelezo ya Waheshimiwa madiwani na kushauri pale watakapohitajika kulingana na nafasi zao. ‘’ tumeyasikia maelekezo ya Mhe.Mkuu wa Wilaya , tumeyasikia maelezo ya waheshimiwa madiwani pia , nawaahidi tutayafanyika kazi’’ aliongeza Bw.Jaffari.

Katika baraza hilo kamati za kudumu ziliwasilisha taarifa zao katika kipindi cha miezi mitatu kuanzia Januari hadi Machi 2021 ambapo kamati ya fedha, Uongozi na Mipango iliwasilisha taarifa ya mapato na matumizi ambapo kiasi cha shilingi Bilioni 1.3 ilikusanywa kutoka vyanzo mbali mbali vya ndani, wafadhili na serikali kuu na mpaka Mchi 31 Jumla ya shilingi milioni 903 ilitumika katika matumizi ya kawaida na miradi mbali mbali kama ujenzi wa madarasa, vyoo, ununuzi wa madawati pamoja na utoaji wa ruzuku kwa kaya masikini chini ya mpango wa kunusuru kaya masikini-TASAF. Kamati zingine zilizowasilisha taarifa zao ni Kmati ya Uchumi , ujenzi na mazingira, Kamati ya Elimu, Afya na Maji pamoja na Kamati ya Kudhibiti Maambukizi ya Ukimwi.

Wilaya ya Kilwa inaundwa na Tarafa sita ,kata 23 pamoja na vijiji 91 ambapo vyanzo vikuu vinavyochangia mapato ya ndani ni uvuvi, kilimo cha Ufuta na Korosho pamoja na uchimbaji wa madini ya gypsum.

Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU UTOAJI WA MIKOPO KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 04, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 11, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI. April 25, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MAKALA APONGEZA JITIHADA ZA KURUDISHA MAWASILIANO SOMANGA

    April 10, 2025
  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa Mkono wa Eid kwa watoto wenye mahitaji Maalum Shule ya Msingi Mtanga Wilayani Kilwa.

    March 31, 2025
  • IDARA YA MAENDELEO YA JAMII YATOA MSAADA WA TELEVISHENI KWA GEREZA LA KILWA MASOKO

    April 28, 2025
  • MARAFIKI WA ELIMU WAWASILISHA TAARIFA YA UFUATILIAJI WA MAKUZI YA AWALI YA MTOTO KWA WADAU WA ELIMU KILWA.

    April 28, 2025
  • Tazama Zote

Video

Mkuu wa Wilaya ya Kilwa Akipokea Mwenge wa Uhuru.
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • TARURA GPN
  • Watumishi Portal
  • MIKOPO 10%
  • Mikopo ya Wanawake na Vijana
  • Huduma za Elimu

Tovuti Muhimu

  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ikulu
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu
  • Lindi

Idadi ya Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani Zetu

    Kilwa Masoko

    Anuani ya Posta: 160

    Simu: 0672365354

    Simu: 0672581557

    Barua pepe: ded@kilwadc.go.tz /ictsupport@kilwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Kanuni Binafsi
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa