• Malalamiko |
    • Anuani Zetu |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Kilwa District Council
Kilwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Mikakati ya Halmashauri
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Utumishi na Utawala
      • Elimu ya Msingi
      • Mipango na Takwimu
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Maliasili
    • Vitengo
      • Usafi na Mazingira
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ugavi
      • TEHAMA
      • Nyuki
      • Biashara
      • TASAF
      • Lishe
      • Uvuvi
    • Miji Midogo
      • Masoko
      • Kivinje
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Huduma za Uwekezaji
    • Biashara na Viwanda
    • Madini
    • Uvuvi
    • Utalii
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Mikopo kina Mama na Vijana
    • Huduma za Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Itakayo tekelezwa
  • Machapisho
    • Muongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Mifumo
    • PlanRep
    • FFARS
    • Prem
    • Salary Slip Portal

WAZIRI MKUU AWATAKA WANANCHI KUHAMA MAENEO YA MABONDENI KUEPUKA MAAFA

Posted on: February 5th, 2020


Waziri mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Kassim Majaliwa amewataka wananchi wote nchini kuhama kutoka maeneo ambayo yameonekana ni hatarishi kwa makazi hasa katika kipindi hiki cha Mvua.

Mhe.Waziri Mkuu Majaliwa ameyasema hayo katika ziara yake ya kikazi ya siku moja wilayani Kilwa Mkoa wa Lindi. Ziara hiyo ya Waziri Mkuu ililenga kuwapa pole wahanga wote wa mafuriko katika mkoa wa Lindi kwa ujumla ambapo athari kubwa za mafuriko hayo yametokea katika Wilaya ya Kilwa yenye athari katika vijiji kumi na saba (17) ndani ya kata  saba za Wilaya ya Kilwa.

Akiwa Wilayani Kilwa Mhe.Waziri Mkuu alipata fursa ya kukagua athari za mafuriko kwa njia ya anga na kisha kufanya mikutano miwili ya adhara katika Vijiji vya Nakiu katika kata ya Nanjirinji na Kijiji cha Kipindimbi iliopo kata ya Njinjo.

Katika kata ya Njinjo, Mhe.Waziri Mkuu alitembelea eneo lililoathirika na kisha kukutana na wananchi ambapo alifikisha salamu pole za Serikali kutoka kwa Mhe.Dr.John Pombe Magufuli, Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania ambapo aliwahakikishia wananchi hao kuwa Mhe.Rais ameguswa na maafa ya watu 13 yaliyotokea katika Wilaya ya Kilwa pekee na Zaidi ya kaya 3774 zilizokosa makazi kutokana na mafuriko hayo yaliyoanza tarehe 26Januari 2020.

‘’Nimeona hali halisi ya mafuriko, ni janga kubwa ,nawasihi viongozi wa Wilaya na Mkoa mshirikiane kwa pamoja kuhakikisha wananchi hawa wanapatitiwa viwanja katika maeneo salama lakini pia hawarudi katika maeneo ya mabondeni’’ alisisitiza Mhe.Waziri Mkuu.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Kilwa Mhe.Christopher Ngubiagai alimhakikishia Mhee.Waziri Mkuu kuwa Ofisi yake itasimamia upatikanaji wa viwanja maeneo salama ambapo mpaka kufikia tarehe 5Januari 2020 jumla viwanja 670 vilishapimwa na kugawanywa kwa wananchi na tayari baadhi ya wananchi wameshaanza ujenzi katika maeneo hayo.

Mkuu wa Wilaya pia alitumia nafasi hiyo kumweleza Mhe.Waziri mkuu ukubwa wa maafa hayo ambapo Zaidi ya wananchi elfu tisa bado ni wahitaji wa huduma muhimu za kijamii kama chakula na malazi kwa sababu wengi wao walipoteza mali zao zote na kwa sasa pamoja na kupatiwa viwanja lakini mpaka sasa bado wanapatiwa msaada wa chakula na malazi kutoka Ofisi ya Wilaya kutokana na uharibifu uliotokea.

Mhe.Waziri Mkuu alimhakikishia Mkuu wa Wilaya kuwa ofisi yake imeshafanya tathmini na tayari imeshachukua hatua ya kuleta misaada ya kijamii.

Katika Wilaya ya Kilwa Mfuriko yalitokea kuanzia tarehe 26 Januari 2020 ambapo Jumla ya kaya 3774 yenye jumla ya wanannchi Zaidi ya 24,000 ziliathirika ambapo wananchi walipoteza mali zao, nyumba zao, mifugo pamoja na mazao.

Kata zilizoathirika Zaidi ni kata za Njinjo, Mitole, Kikole, Mandawa na Kiranjeranje. Kata zingine ni Nanjirinji  na Kivinje. Kati ya wananchi 24,000 waliothiriwa, wananchi 9860 wamekuwa wakiishi katika kambi na vituo mbalimbali  kwa kutegemea misaada yote ya kibinadamu na kijamii katika vituo hivyo na katika maeneo salama walipohamishiwa.

Naye Mwenyekiti wa Kamati ya Maafa Wilaya ya Kilwa ambaye pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa Ndg Renatus Mchau alimweleza Mhe.Waziri Mkuu kuwa Ofisi yake inaendelea kuratibu misaada yote inayotolewa na Serikali na  wadau mbali mbali na kuhakikisha kuwa misaada hiyo inawafikia walengwa ambao ni waathirika wa mafuriko kwa wakati.

Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU UTOAJI WA MIKOPO KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 04, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 11, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI. April 25, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • BANDARI YA UVUVI KILWA KUKAMILIKA MWEZI JUNI 2025

    May 08, 2025
  • KAMATI YA SIASA YA CCM MKOA WA LINDI YAIPONGEZA KILWA KWA UTEKELEZAJI WA ILANI

    May 07, 2025
  • KILWA YAPIGA HATUA KATIKA KUTOKOMEZA UKATILI WA KIJINSIA DHIDI YA WANAWAKE NA WATOTO

    May 06, 2025
  • WANANCHI, WANAFUNZI NA WATUMISHI KILWA WAJITOKEZA KWA MAZOEZI YA PAMOJA UWANJA WA MWENGE/TAIFA

    May 03, 2025
  • Tazama Zote

Video

Mkuu wa Wilaya ya Kilwa Akipokea Mwenge wa Uhuru.
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • TARURA GPN
  • Watumishi Portal
  • MIKOPO 10%
  • Mikopo ya Wanawake na Vijana
  • Huduma za Elimu

Tovuti Muhimu

  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ikulu
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu
  • Lindi

Idadi ya Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani Zetu

    Kilwa Masoko

    Anuani ya Posta: 160

    Simu: 0672365354

    Simu: 0672581557

    Barua pepe: ded@kilwadc.go.tz /ictsupport@kilwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Kanuni Binafsi
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa