• Malalamiko |
    • Anuani Zetu |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Kilwa District Council
Kilwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Mikakati ya Halmashauri
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Utumishi na Utawala
      • Elimu ya Msingi
      • Mipango na Takwimu
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Maliasili
    • Vitengo
      • Usafi na Mazingira
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ugavi
      • TEHAMA
      • Nyuki
      • Biashara
      • TASAF
      • Lishe
      • Uvuvi
    • Miji Midogo
      • Masoko
      • Kivinje
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Huduma za Uwekezaji
    • Biashara na Viwanda
    • Madini
    • Uvuvi
    • Utalii
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Mikopo kina Mama na Vijana
    • Huduma za Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Itakayo tekelezwa
  • Machapisho
    • Muongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Mifumo
    • PlanRep
    • FFARS
    • Prem
    • Salary Slip Portal

Vilio vya Bmu vyapatiwa majibu

Posted on: September 27th, 2018

Kilwa,

    Ikiwa imepita wiki moja toka vikundi vya usimamizi shirikishi wa rasilimali za bahari  wilaya ya Kilwa kuelekeza vilio vyao kwa Naibu waziri wa Mifugo na Uvuvi juu ya ukosefu wa Boti za kufanyia  doria Hatimaye vilio vyao vyapatiwa ufumbuzi.

Ufumbuzi huo umepatikana Septemba 26, baada ya Umoja wa Ulaya (EU) kwa kushirikiana na Shirika la Hifadhi mazingira (WWF) Tanzania kukabidhi msaada wa boti mbili zenye uzito wa tani 1.6 kila moja ambazo zimegharimu Dola za kimarekani 64,015 sawa na Shilingi 144,033,750 ikiwa pamoja na gharama ya injini zenye horsepower 40 kila moja na vifaa vya usalama majini kwa Vikundi vya Bmu vya wilaya ya kilwa (CFMA ya TIM4SI) na Wilaya ya mafia makabidhiano yaliyofanyika katika viwanja vya Maalim Seif Mjini Kilwa Kivinje.

Akizungumza katika makabidhiano ya Boti hizo Mkurugenzi wa Shirika la kuhifadhi Mazingira (WWF) Tanzania Dokta Amani Ngusaru amesema Boti zilizoltolewa ni kwa ajili ya ulinzi wa mazingira na rasilimali za uvuvi na kuvitaka vikundi hivyo kuzitumia kwa Malengo yaliyo kusudiwa.

“Hizi boti zikatumike kwa uangalifu na kwa malengo ambayo yamekusudiwa hizi boti ni kwa ajili ya kufanyia doria na si kwa ajili ya uvuvi’’ alihitimisha Dokta Ngusaru

Moja ya Boti zilizokabidhiwa kwa Vikundi vya usimamizi shirikishi wa rasilimali za Bahari wilaya ya Kilwa kwa ajili ya Doria

Naye Naibu waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega amewapongeza wananchi wa Kilwa Kivinje kwa kukubali kubadilika na kuachana na uvuvi haramu wa kutumia Mabomu na kuagiza vikundi vya usimamizi shirikishi wa rasilimali za bahari kuwakamata wote ambao wanajihusisha na uvuvi wa kutumia zana zilizo katazwa na kuwafikisha katika vyombo vya sheria bila kuwaonea huruma.

“Hao waliokuwa wanapiga mabomu ndio wamesababisha mapaka leo kuanzia tanga hadi Mtwara hakuna kiwanda cha samaki, nani anaweza kuwekeza sehemu ambayo hana uhakika wa malighafi atazipata wapi, Ninyi mpo kisheria fanyeni kazi zenu bila kuogopa vitisho kutoka kwa mtu yeyote. Kamateni wote ambao wanafanya uvuvi haramu na muwafikishe katika vyombo vya sheria mkishindwa kuwadhibiti nipeni taarifa” alisema Ulega

Aidha ameitaka Halmashauri kuvipa vikundi mamlaka ya kukusanya Ushuru ili vikundi hivyo viweze kujiendesha vyenyewe bila kuitegemea Halmashauri katika kujiendesha.

“Kabla ya kuja hapa nilikuwa Pangani Tanga na wameniambia kuwa Bmu zimepwa majukumu ya kukusanya ushuru na asilimia wanazozipata kama malipo zinatumika kujiendesha, kabla ya kupewa jukumu hilo makusanyo yalikuwa kati ya Milioni Thelathini lakini toka wapewe majukumu ya kukusanya yamepanda hadi Milioni Mia mbili sasa na hapa nataka muige huo mfano nikija tena mwezi wa kumi na moja nikute hilo limefanyika” alihitimisha Ulega.   

 Kwa upande wake kaimu mkurugenzi wa Halmashauri yaa wilaya ya kilwa Ndg. Pundile ameishukuru Shirika la kuhifadhi Mazingira (WWF) kwa msaada wa boti ambazo zitasaidia katika kuimarisha ulinzi katika bahari ambayo Halmashauri inaitegemea kama moja ya chanzo chake cha  mapato.


Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU UTOAJI WA MIKOPO KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 04, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 11, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI. April 25, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MAKALA APONGEZA JITIHADA ZA KURUDISHA MAWASILIANO SOMANGA

    April 10, 2025
  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa Mkono wa Eid kwa watoto wenye mahitaji Maalum Shule ya Msingi Mtanga Wilayani Kilwa.

    March 31, 2025
  • IDARA YA MAENDELEO YA JAMII YATOA MSAADA WA TELEVISHENI KWA GEREZA LA KILWA MASOKO

    April 28, 2025
  • MARAFIKI WA ELIMU WAWASILISHA TAARIFA YA UFUATILIAJI WA MAKUZI YA AWALI YA MTOTO KWA WADAU WA ELIMU KILWA.

    April 28, 2025
  • Tazama Zote

Video

Mkuu wa Wilaya ya Kilwa Akipokea Mwenge wa Uhuru.
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • TARURA GPN
  • Watumishi Portal
  • MIKOPO 10%
  • Mikopo ya Wanawake na Vijana
  • Huduma za Elimu

Tovuti Muhimu

  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ikulu
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu
  • Lindi

Idadi ya Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani Zetu

    Kilwa Masoko

    Anuani ya Posta: 160

    Simu: 0672365354

    Simu: 0672581557

    Barua pepe: ded@kilwadc.go.tz /ictsupport@kilwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Kanuni Binafsi
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa