• Malalamiko |
    • Anuani Zetu |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Kilwa District Council
Kilwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Mikakati ya Halmashauri
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Utumishi na Utawala
      • Elimu ya Msingi
      • Mipango na Takwimu
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Maliasili
    • Vitengo
      • Usafi na Mazingira
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ugavi
      • TEHAMA
      • Nyuki
      • Biashara
      • TASAF
      • Lishe
      • Uvuvi
    • Miji Midogo
      • Masoko
      • Kivinje
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Huduma za Uwekezaji
    • Biashara na Viwanda
    • Madini
    • Uvuvi
    • Utalii
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Mikopo kina Mama na Vijana
    • Huduma za Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Itakayo tekelezwa
  • Machapisho
    • Muongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Mifumo
    • PlanRep
    • FFARS
    • Prem
    • Salary Slip Portal

"Tumejipanga kupambana na vitendo vya kikatili" - Katibu Tawala Kilwa

Posted on: March 8th, 2018

  Kilwa,  

       Wanawake nchini wametakiwa kuto fumbia macho vitendo vya kikatili vinavyofanywa dhidi yao badala yake watoe taarifa katika vyombo vya sheria na asasi zingine zinazo jishughulisha na kutetea haki za wanawake.

Wito huo umetolewa na Katibu tawala wilaya ya kilwa Bw. Haji Mbaruku Balozi alipokua akihutubia wananchi kwa niaba ya mkuu wa wilaya ya kilwa katika kilele cha maadhimisho ya siku ya wanawake duniani yaliyofanyika wilayani kilwa katika viwanja vya Garden Mkapa.

Bw. Balozi amesema iwapo vitendo vya kikatili dhidi ya wanawake vitaendelea kufumbiwa macho katika jamii basi madhara makubwa yataendelea kutokea ikiwemo kukosa haki zao za kimsingi ambazo zinapelekea kurudisha nyuma gurudumu la maendeleo.

Amesema serikali wilayani kilwa iko macho na imejipanga kuhakikisha inawachukulia hatua kali za kisheria wale wota ambao watabainika na kukutwa na hatia ya kutenda vitendo vya kikatili na unyanyasaji wa aina yeyote ile dhidi ya wanawake na watoto.

“Katibu wa jukwaa la wanawake naomba tushirikiane katika hili, lete matatizo ya wanawake  ambayo mmekua mkikutana nayo huko mnakopita ili kwa pamoja tuone ni jinsi gani tunawasaidia ”. Alisisitiza Bw. Balozi

Pia amewataka wanawake kuanzisha na kuvisajiri vikundi  katika mamlaka husika ikiwemo Mamlaka ya Mapato  (TRA) ili viweze kutambulika kisheria na kuahidi kuwaomba Mamlaka ya Uthibiti Ubora (TBS) kuja wilayani kilwa kwa dhumuni la kuvijengea uwezo vikundi ambavyo vimekua vikijishughulisha na usindikaji wa vyakula ili kuongeza thamani ya bidhaa zao.

Katibu Tawala Wilaya ya Kilwa Bw. Haji Mbaruku Balozi akihutubia wananchi katika kilele cha siku ya Wanawake Dunia iliyofanyika katika viwanja vya Garden Mkapa mjini Kilwa Masoko.

Aidha amewataka wanawake kujitokeze kwa wingi kugombea nafasi mbalimbali za uongozi katika chaguzi zinazotarajiwa kufanyika mwaka kesho na uchaguzi mkuu, kwani wanauwezo mkubwa wa kuongoza kama ambavyo wanawake wengine wamekua wakiongoza wizara mbalimbali.

Akisoma Risala ya maadhimisho ya siku ya wanawake Kwa niaba ya wanawake wa wilaya ya kilwa Bi. Nuru ameimba serikali kupitia mgeni rasmi kuwatafutia masoko ya uhakika kwa ajili ya kuuza bidhaa zao ambazo wanazitengeneza pamoja na kuimarishiwa miundo mbinu kwani miundo mbinu iliyopo sasa hairidhishi.

Nae muwakilishi kutoka Dawati la jinsia wilaya ya kilwa Wp. Mackrina ameiomba jamii ishirikiane na Dawati hilo kwa kuripoti vitendo vya kikatili dhidi ya wanawake na watoto na kuacha tabia ya kuficha vitendo hivyo au kumalizana kienyeji.

Awali akitoa salamu zake Katibu wa Jukwaa la wanawake Kilwa Bi. Pili Mohamedi amewataka wanawake waungane katika kupinga ukatili dhidi yao na kuzikabili changamoto mbalimbali katika kuleta ukombozi.

Pia ameishukuru idara ya maendeleo ya jamii wilayani kilwa kwa kuwajengea uwezo katika kufanikisha shughuli zao za kila siku katika kuhakikisha mwanamke anapata haki zake anazostahili.

Kila tarehe 8 machi Tanzania inaungana na nchi nyingine wanachama wa umoja wa mataifa kuadhimisha siku ya wanawake duniani. Kauli mbiu ya kitaifa kwa mwaka 2018 ni “Kuelekea Uchumi wa Viwanda, Tuimarishe Usawa wa Kijinsia na Uwezeshaji Wanawake Vijijini.

Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU UTOAJI WA MIKOPO KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 04, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 11, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI. April 25, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • MAKALA APONGEZA JITIHADA ZA KURUDISHA MAWASILIANO SOMANGA

    April 10, 2025
  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa Mkono wa Eid kwa watoto wenye mahitaji Maalum Shule ya Msingi Mtanga Wilayani Kilwa.

    March 31, 2025
  • IDARA YA MAENDELEO YA JAMII YATOA MSAADA WA TELEVISHENI KWA GEREZA LA KILWA MASOKO

    April 28, 2025
  • MARAFIKI WA ELIMU WAWASILISHA TAARIFA YA UFUATILIAJI WA MAKUZI YA AWALI YA MTOTO KWA WADAU WA ELIMU KILWA.

    April 28, 2025
  • Tazama Zote

Video

Mkuu wa Wilaya ya Kilwa Akipokea Mwenge wa Uhuru.
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • TARURA GPN
  • Watumishi Portal
  • MIKOPO 10%
  • Mikopo ya Wanawake na Vijana
  • Huduma za Elimu

Tovuti Muhimu

  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ikulu
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu
  • Lindi

Idadi ya Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani Zetu

    Kilwa Masoko

    Anuani ya Posta: 160

    Simu: 0672365354

    Simu: 0672581557

    Barua pepe: ded@kilwadc.go.tz /ictsupport@kilwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Kanuni Binafsi
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa