• Malalamiko |
    • Anuani Zetu |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
Kilwa District Council
Kilwa District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Mikakati ya Halmashauri
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Afya
      • Utumishi na Utawala
      • Elimu ya Msingi
      • Mipango na Takwimu
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Ujenzi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Mifugo na Uvuvi
      • Fedha na Biashara
      • Maliasili
    • Vitengo
      • Usafi na Mazingira
      • Sheria
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Ugavi
      • TEHAMA
      • Nyuki
      • Biashara
      • TASAF
      • Lishe
      • Uvuvi
    • Miji Midogo
      • Masoko
      • Kivinje
  • Fursa za Uwekezaji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Huduma za Uwekezaji
    • Biashara na Viwanda
    • Madini
    • Uvuvi
    • Utalii
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Mikopo kina Mama na Vijana
    • Huduma za Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Fedha Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Huduma za Jamii
      • Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
    • Ratiba ya Vikao vya Kisheria
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Itakayo tekelezwa
  • Machapisho
    • Muongozo
    • Utaratibu
    • Taarifa
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Mifumo
    • PlanRep
    • FFARS
    • Prem
    • Salary Slip Portal

Bodi ya afya Kilwa yazinduliwa rasmi

Posted on: June 7th, 2018

   Kilwa,     

         Wajumbe wa bodi ya afya Halmashauri ya wilaya ya kilwa wametakiwa kuboresha huduma za afya katika vituo vya kutolea huduma pamoja na kusimamia kikamilifu matumizi ya fedha kutoka serikalini na zinazokusanywa kutoka katika vyanzo mbalimbali.

Wito huo umetolewa na mkuu wa wilaya ya kilwa Mhe. Christopher Ngubiagai alipokua akizindu rasmi Bodi hiyo ofisini kwake Mjini Kilwa Masoko.

Ngubiagai amesema wananchi wanaimani kubwa na wajumbe hao na ndio mana wamewapatia nafasi ya kuwa wawakilishi wao  katika bodi hiyo.

“Majukumu muliyopewa ni makubwa sana wananchi wamewaamini na mimi nawaamini pia, imani yangu hamutawaangusha katika utendaji wenu kwa muda wote mtakao kuwa wajumbe wa bodi hii” alisema ngubiagai

Ngubiagai amewataka wajumbe kutekeleza majukumu yao kwa kuutanguliza uzalendo mbele kwani kwa kufanya hivyo kutawasaidia kufikia malengo ya kuiinua Sekta ya afya Wilayani Kilwa.

“Uzalendo ndio nguzo muhimu itakayofanya tupate matokeo chanya. kama tujuavyo tuna changamoto nyingi sana katika hizi bodi zetu ikiwemo ya rasilimali fedha, sitarajii kusikia mmeshindwa kufanya vikao kisa mmekosa Fedha ya kulipana  posho tunatakiwa kujitoa kwa moyo wote ikipatikana sawa ikikosekana sawa” alisistiza Ngubiagai

Mkuu wa Wilaya ya Kilwa Mhe. Christopher Ngubiagai akizungumza na Wajumbe wa Bodi ya Afya ya Wilaya ya Kilwa wakati wa uzinduzi wa Bodi hiyo (Picha:Ally Ruambo)

Pia amewataka wajumbe kuendeleza mema yaliyo achwa na wajumbe wa bodi iliyopita na kuongeza mengine ambayo yatakua yana tija kwa ustawi wa sekta ya afya.

Aidha Mhe. Ngubiagai  ameahidi kutoa ushirikiano wa hali mali kwa wajumbe wa Bodi hiyo

“Hongereni sana kwa mara nyingine kwa kuwa wajumbe wa Bodi hii tusiogopane muda wowote kukiwa na jambo mnakaribishwa na nina ahidi kuendelea kutoa ushirikiano wa mali na hali kama ambavyo tulikua tunashirikiana na kamati zilizopita” alihitimisha Ngubiagai

Kwa upande wake Mwenyekiti wa bodi ya afya Wilaya ya Kilwa Bw. Adjuti Alli Adjuti amemshukuru Mkuu wa Wilaya kwa nasaha zake na kuahidi kuyafanyia kazi yale yote ambayo wameelekezwa kuyafanya na kusistiza ushirikiano miongoni mwa wajumbe.

Wajumbe wa Bodi ya Afya ya Wilaya ya Kilwa wakifuatilia mazungumzo ya Mkuu wa wilaya  wakati wa uzinduzi wa Bodi hiyo (Picha:Ally Ruambo)

Awali akizungumza na wajumbe wa Bodi ya afya Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa Mkurugenzi mtendaji wa Halmsahuri ya Wilaya ya Kilwa Ndg. Zablon Bugingo amewataka wajumbe kuwa mstari wa mbele kuwaeleza Wananchi ukweli juu ya uzushi ambao umekua ukizushwa na baadhi ya watu.

“Ndugu zangu tunawategemea sana kwenda kuwaeleza wananchi ukweli pale panapotokea uzushi kwa kuwa mnatoka moja kwa moja katika jamii inayotuzunguka itakuwa rahisi ukweli kufika, kumekua na fununu nyingi sana ambazo kimsingi hazina ukweli wowote kwahiyo ninyi wajumbe mtusaidie kuwaeleza ukweli wa mambo yalivyo’ alisema Bugingo

Aidha Bugingo amewataka wajumbe kuielekeza jamii juu ya utaratibu wa kuwasilisha malalamiko yao sehemu husika pindi wanapoona kuna jambo halijaenda sawa.

“Mtusaidie kuwaelimisha wananchi kuhusu suala la malalamiko, kuna watu wanakutana na changamoto mbalimbali wanapoenda kupata huduma lakini hawasemi wanakaa nayo na kusubiri aje kiongozi ndio wayaseme na wengine wanayafikisha ngazi za juu bila kuanzia chini, kwahiyo tukawaelekeze kuwa kuna hatua za kuwasilisha hayo malalamiko’ alisisitiza bugingo.

Mkurugenzi wa Halmashauri wa ya Wilaya ya Kilwa Ndg. Zablon Bugingo akizungumza na wajumbe wa Bodi ya Afya Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa (Hawapo pichani)  kabla ya uzinduzi rasmi wa Bodi hiyo (Picha;Ally Ruambo)

Kabla ya kuzinduliwa kwa Bodi wajumbe walifanya uchaguzi na kumchagua Bw. Adjuti Alli Adjuti kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya afya Halmashauri ya wilaya ya Kilwa na Bi. Michaela Adeodatus Ngonyani kuwa Makamu mwenyekiti.


Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU UTOAJI WA MIKOPO KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU October 04, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI October 11, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI September 27, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI. April 25, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • DC KILWA AITAKA JAMII KUDHIBITI UTUMIAJI WA PLASTIKI ILI KUYALINDA MAZINGIRA.

    June 05, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAKIMBIZWA KILOMETA 173 NA KUTEMBELEA MIRADI 13 YENYE THAMANI YA TSH BILIONI 11 WILAYANI KILWA.

    May 31, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAWEKA JIWE LA MSINGI ZAHANATI YA NJINJO KILWA.

    May 31, 2025
  • MWENGE WA UHURU WAWEKA JIWE LA MSINGI KWENYE MRADI WA UJENZI WA MNADA WA MIFUGO KILWA

    May 31, 2025
  • Tazama Zote

Video

Mkuu wa Wilaya ya Kilwa Akipokea Mwenge wa Uhuru.
Video Zaidi

Kurasa za Haraka

  • TARURA GPN
  • Watumishi Portal
  • MIKOPO 10%
  • Mikopo ya Wanawake na Vijana
  • Huduma za Elimu

Tovuti Muhimu

  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ikulu
  • Wizara ya Fedha
  • Wizara ya Elimu
  • Lindi

Idadi ya Watembeleaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani Zetu

    Kilwa Masoko

    Anuani ya Posta: 160

    Simu: 0672365354

    Simu: 0672581557

    Barua pepe: ded@kilwadc.go.tz /ictsupport@kilwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Kanuni Binafsi
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa